Mke wangu anamwambia mama yake kuwa kanishika, wanatangaza mtaani na maneno tunayojadili ndani mimi na yeye nayakuta nje

malembeka18

JF-Expert Member
Jan 26, 2018
2,780
2,712
Habari wakuu,

Nipeni ushauri juu ya huyu mke amekuwa na tabia kuwa jambo tunalojadili mimi na yeye kisha yeye kumpelekea mama yake na mama yake kuyasema kwa ndugu zake.

Ndugu hao hao wa ndani wanayaleta na ukiangalia ni kweli kabisa Jambo nilijadili mimi tu na mke.

Pasi na hivyo hayo yote anayojadili na mama yake ni ya kujitapa kuwa wamenishika na bado Sasa maneno yananifikia na ni ya kweli kabisa maana ni mambo ambayo nakua nimejadili mimi na mke tu

Sasa hao wengine wanayajuaje naamini mke ndie anaemwambia mama yake!
 
Kakushikaje kwanza?kama kakushika kwa kufanya wajibu wake km mke basi ni vizuri ila kama katumia nje zake binafsi za waganga wa ista na wa bagamaoyo basi hapo ni balaaa...


Kuhusu kutangaza ni udhaifu wa wanawake wengi,wakipata mwanaume anayeonekana wa maana machoni pake na kwa watu basi wachache sana wanaweza kuvumilia kutotangaza mahusiano yao kwa watu Baki.Asipo tangaza utaona anavyoringa na kujiona wa thamani kuliko wenzake

We unadhani wanaume wanaokaa na marafiki kupanga mipango ya maendeleo ni wajinga???walisoma mchezo wakaona mke wa kutunza mambo sina na ndo nishamuoa hivyo ni mwendo wa kufanya maendeleo ya kustukizana tu.Ukitaka kununua kiwanja we unamwambia tu juma pili kuna sehemu tunaenda,ikifika j2 asubuh unamwambia tunaenda kununua kiwanja na hapo ukitoka tu kwenda kuoga, utakuta keshapiga simu kwa Shoga ake ile safari mume wangu aliyoniambia tunaenda,kumbe ya kwenda kununua kiwanja’Mapema sana kifua Hana

Ishi nao kwa Akili,mapungufu ya mwanamke siku zote ni madogo machoni pao na machoni pa jamii lkn makubwa machoni petu wanaume.

Unakuja na million 5 ndani tayari keshatuma Msg.Shooooo baba michael leo kaja na maburungutu ya hela sijui kayatoa wapiii yaani nyumba inanuka hela tu,Yule nae kamsimulia mumewe jambazi,mmevamia mnapigwa mmeporwa.

Mwanamke asiye na siri atasababisha ulogwe,uibiwe,udhulumiwe,udharauliwe,utongozwe hovyo yaani ni mtihani sheheee
 
Kuna tatizo gani mkeo 'akikushika'?
Kama yale mnayoongea ndani anapeleka nje, dawa ni rahisi sana, hakuna kuongea mambo usiyotaka kutoka nje mkiwa ndani. Pigeni story zingine tu na mkiwa faragha mpige miti haswaa. Baada ya muda atakwenda kusimulia huko nje namna unavyompiga miti kisawa sawa.
 
Kakushikaje kwanza?kama kakushika kwa kufanya wajibu wake km mke basi ni vizuri ila kama katumia nje zake binafsi za waganga wa ista na wa bagamaoyo basi hapo ni balaaa...


Kuhusu kutangaza ni udhaifu wa wanawake wengi,wakipata mwanaume anayeonekana wa maana machoni pake na kwa watu basi wachache sana wanaweza kuvumilia kutotangaza mahusiano yao kwa watu Baki.Asipo tangaza utaona anavyoringa na kujiona wa thamani kuliko wenzake

We unadhani wanaume wanaokaa na marafiki kupanga mipango ya maendeleo ni wajinga???walisoma mchezo wakaona mke wa kutunza mambo sina na ndo nishamuoa hivyo ni mwendo wa kufanya maendeleo ya kustukizana tu.Ukitaka kununua kiwanja we unamwambia tu juma pili kuna sehemu tunaenda,ikifika j2 asubuh unamwambia tunaenda kununua kiwanja na hapo ukitoka tu kwenda kuoga, utakuta keshapiga simu kwa Shoga ake ile safari mume wangu aliyoniambia tunaenda,kumbe ya kwenda kununua kiwanja’Mapema sana kifua Hana

Ishi nao kwa Akili,mapungufu ya mwanamke siku zote ni madogo machoni pao na machoni pa jamii lkn makubwa machoni petu wanaume.

Unakuja na million 5 ndani tayari keshatuma Msg.Shooooo baba michael leo kaja na maburungutu ya hela sijui kayatoa wapiii yaani nyumba inanuka hela tu,Yule nae kamsimulia mumewe jambazi,mmevamia mnapigwa mmeporwa.

Mwanamke asiye na siri atasababisha ulogwe,uibiwe,udhulumiwe,udharauliwe,utongozwe hovyo yaani ni mtihani sheheee
hii ni kweli kabisa tuishi nao kwa akili zaidi

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Habari wakuu, nipeni ushauri juu ya huyu mke amekua na tabia jambo nalojadili mimi na yeye kisha yeye kumpelekea mama yake na mama yake kuyasema kwa ndgu zake, ndugu hao hao wa ndani wanayaleta na ukiangalia ni kweli kabisa Jambo nilijadili mimi tu na mke.

Pasi na hivyo hayo yote anayojadili na mama yake ni ya kujitapa kuwa wamenishika na bado Sasa maneno yananifikia na ni ya kweli kabisa maana ni mambo ambayo nakua nimejadili mimi na mke tu Sasa hao wengine wanayajuaje naamini mke ndie anaemwambia mama yake.
Kama huyo mkeo hakusaliti hakuendeshi basi furahia maana hiyo ndoa yako itadumu. Mama mkwe ni kiungo mhimu kudumisha ndoa za watoto wao. Kuhusu kukuongea mtaani ni kwamba wanakuona unathamani kwao. Kama unataka kujua kuwa umebarikiwa basi waulize wale ambao wakwe zao wanawachukulia kama shamba boy fulani hivi.
 
Atakuwa kakushika kweli maana angekuwa hajakushika,usingekuwa haujajua Cha kufanya mpaka Sasa maana Mambo mengine ni madogomadogo ambayo hayahitaji elimu hata ya chekechea kuyatatua.
 
Habari wakuu, nipeni ushauri juu ya huyu mke amekua na tabia jambo nalojadili mimi na yeye kisha yeye kumpelekea mama yake na mama yake kuyasema kwa ndgu zake, ndugu hao hao wa ndani wanayaleta na ukiangalia ni kweli kabisa Jambo nilijadili mimi tu na mke.

Pasi na hivyo hayo yote anayojadili na mama yake ni ya kujitapa kuwa wamenishika na bado Sasa maneno yananifikia na ni ya kweli kabisa maana ni mambo ambayo nakua nimejadili mimi na mke tu Sasa hao wengine wanayajuaje naamini mke ndie anaemwambia mama yake.
Hao ni wale wanawake wasiojua ndoa na thamani yake,kila mnachofanya anaenda kukipeleka kwao,matokeo yake unakuta ndoa yako inakuwa remotely controlled na ukweni,kifupi ni kuwa huyo hajielewi au ni wale wanaoamua kuolewa ili tu aonekana na yeye ana mume lakini mwishowe anajikuta anachemsha...
 
Back
Top Bottom