Mke wangu ameniudhi tena

Mke wangu ameniudhi tena

Sikununu

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2015
Posts
341
Reaction score
101
Juzi nilileta taarifa ya mke wangu kutojua usafi na kupika dagaa kila siku nilipanga kumfungisha virago but kutokana na huruma ya wanajukwaa nimemuweka chini nmempa tuition na tume draft ratiba ya chakula kwa wiki nzima nikamsamee.

Sasa kama wiki ya pili kuna suala ambalo tunalishughulikia kwa pamoja na nimemshirikisha wife kwa 100% ingawa mie ndio ninayeangaika nalo.

Mke wangu aliponiudhi ni pale alipo mwambia baba yake yaani baba mkwe wangu,jana amenipigia simu na kunieleza yale yote ambayo yapo mezani kwetu tuliyopanga na mke wangu na amesisitizia ilo suala ni gumu na anajitolea kutusaidia.

Nilikosa jibu la kumpa na kuhisi wife amenidhalilisha, ukizingatia mkwe wangu ni muhafidhina sana mpaka nahisi labda anaona mwanae hayupo eneo sahihi.

Nimekasirika sana mpaka nahisi kukimbia kabisa nisionekane tena,my take wanawake msipende kushirikisha watu kwenye mambo yenu wawili hata kama baba ako ni tajiri ana uwezo wa kusolve iyo problem.

Natoa taarifa ya mke wangu kuniuzi tena,over 2015.


 
MMmmh !! Kaka mpendwa usiwe Mkali over mkali!! Dunia haistahili mahasira, utajisibu na magonjwa...just calm down na chukulia mambo kwa moyo wa amani!! hakukusudia kutanagaza ya siri au ya nyumabi. Play cool mkuu!
 
Matatizo huyo dada sio size yako kwa kweli...mtoto wa kitajiri hajui kupika au kupangilia mambo ya nyumbani kwake. Na daddy wake ndo superman na saviour wake.....kwahiyo wewe tegemea kila siku wakwe zako kuna na uamuzi kwenye maisha yenu.

Unataka heshma ndani....kaa uyazungumze, mpe list ya vitu huvipendi ikiwemo hilo, nahisi bado hamjafahamiana kiuzaidi.
 
Mke wako umemwambia hilo suala? na amekuambia sabab gani zimemfanya amwambie baba yake hili suala lenu? maana watu mmeweka mitandao kama sehemu ya kutatua matatizo yenu ya ndani yaani mtu kabla haujachukua hata hatua za kutatua tatzo unalileta huku muda mwingine ni kudhalilishana, maana yake hapo unamaanisha mkeo hana uwezo wa kutunza siri za ndani, pengine aliona hilo mnalotaka kufanya huna uwezo nalo ndo maana akaomba msaada kwa baba yake ili awasaidie kutatua kwanini umeshindwa kuiamini, kwani mkwe wako si mzazi wako kana kwamba pale mnapo kwama anashindwa kutoa msaada????
 
Huyo mkeo yupo humu?Na mfahidhina inamaanisha nini?
 
Juzi nilileta taarifa ya wife kutojua usafi na kupika dagaa kila siku nilipanga kumfungisha virago but kutokana na huruma ya wanajukwaa nimemuweka chini nmempa tuition na tumedraft ratiba ya chakula kwa wiki nzima nkamsamee.

Sasa kama wiki ya pili kuna suala ambalo tunalishughulikia kwa pamoja na nmemshirikisha wife kwa 100% ingawa mie ndio ninayeangaika nalo.
Wife aliponiudhi ni pale alipo mwambia baba yake yaani baba mkwe wangu,Jana amenipigia simu na kunieleza yale yote ambayo yapo mezani kwetu tuliyopanga na wife.....na amesisitizia ilo suala ni gumu na anajitolea kutusaidia..nilikosa jibu la kumpa na kuhisi wife amenidhalilisha
Ukizingatia mkwe wangu ni muhafidhina sana mpaka nahisi labda anaona mwanae hayupo eneo sahihi

Nmekasirika sana mpaka nahisi kukimbia kabisa nisionekane tena.

My take....wanawake msipende kushirikisha watu kwenye mambo yenu wawili hata kama baba ako ni tajiri ana uwezo wa kusolve iyo problem.

Natoa taarifa ya wife kuniudhi tena ndani ya 2015...over
Huu nao ni udhalikishaji wa hali ya juu. Mtu badala ya kuzungumza na kutatua matatizo ya nyumbani unayaleta barabani, huo na ni udhalishaji pia. Nampa pole mwanamke aliyeolewa na mume huyu.
 
Huu nao ni udhalikishaji wa hali ya juu. Mtu badala ya kuzungumza na kutatua matatizo ya nyumbani unayaleta [barabani], huo na ni udhalishaji pia. Nampa pole mwanamke aliyeolewa na mume huyu.


The Home Of Great Thinker
 
Mmmh!! kazi kwel, ushauri wa familia unakukera, wajf unaufurahia. hapa tatizo naliona kwako, na namuonea huruma sana mkeo.
 
mi nashangaa mwanaume mzima umeshindwa kuhandle mke wako, au yeye ndo anayekulinda na pesa kila kitu yeye ndo anashughulikia? maana sijawahi ona mwanaume mnyenyekevu hivi kwa wife ambaye hajisomi... Be a man acha utoto
 
We mbona umelileta humu na wewe pia hujatulia ila inaonesha umeshaanza kuchepuka na unamtafutia kisa mkeo umdamp.
 
Mmmh!! kazi kwel, ushauri wa familia unakukera, wajf unaufurahia. hapa tatizo naliona kwako, na namuonea huruma sana mkeo.

Hauja muelewa,

huyu hafai kua mke kabisa, ndio mana wanaume wanawaficha wake zao mambo nyeti sababu ni huu upumb.avu
 
Ulikimbilia kuoa wakati hujajiandaa kisaikolojia sasa unalialia kwenye mitandao Kesho asipovaa pichu pia utakuja kuweka humu. huoni aibu. Watu hutaka ushauri wa mambo magumu si mke hajui kupika unakimbilia kutangaza
 
Mke wako umemwambia hilo suala? na amekuambia sabab gani zimemfanya amwambie baba yake hili suala lenu? maana watu mmeweka mitandao kama sehemu ya kutatua matatizo yenu ya ndani yaani mtu kabla haujachukua hata hatua za kutatua tatzo unalileta huku muda mwingine ni kudhalilishana, maana yake hapo unamaanisha mkeo hana uwezo wa kutunza siri za ndani, pengine aliona hilo mnalotaka kufanya huna uwezo nalo ndo maana akaomba msaada kwa baba yake ili awasaidie kutatua kwanini umeshindwa kuiamini, kwani mkwe wako si mzazi wako kana kwamba pale mnapo kwama anashindwa kutoa msaada????

Ndio nmemwambia na ameniomba nmsamehee kwa hilo.
Mie sijaleta tatizo langu hapa nipate soln coz she still my wife even though.....
Nmetoa taarifa tu ili kushare experience na watu wa rika langu.
Labda unifundishe ni habari gani ambayo inatakiwa iwepo....nakwani kuileta ndo kutaka ushauri...
 
Hauja muelewa,

huyu hafai kua mke kabisa, ndio mana wanaume wanawaficha wake zao mambo nyeti sababu ni huu upumb.avu

Huyu mwanaume mwenzenu nae ni tatizo, vimambo vidogo vidogo ndio hadi alete jf, hawezi kuwa baba kama hawezi kuhimili vimambo vidogo vidogo, sasa yeye anakimbilia jf, mkewe sijui kwao, hiyo nyumba mauzauza. kuna mambo mwanaume anapaswa kuamua kiume yeye kama baba. jifunzeni nyie watoto
 
Huyu mwanaume mwenzenu nae ni tatizo, vimambo vidogo vidogo ndio hadi alete jf, hawezi kuwa baba kama hawezi kuhimili vimambo vidogo vidogo, sasa yeye [anakimbilia jf], mkewe sijui kwao, hiyo nyumba mauzauza. kuna mambo mwanaume anapaswa kuamua kiume yeye kama baba. jifunzeni nyie watoto


[The home of Great Thinker]
 
Huu nao ni udhalikishaji wa hali ya juu. Mtu badala ya kuzungumza na kutatua matatizo ya nyumbani unayaleta barabani, huo na ni udhalishaji pia. Nampa pole mwanamke aliyeolewa na mume huyu.

Tumia japo akili ndogo mungu aliyekupa....hivi unafikilia ilo suala sijalizungumza na wife...ha ha ha
Hivi unajua maana ya kudhalilisha....ebu nijibu swali moja...ni nini dhamira ya jf kutumia fake id.
 
Back
Top Bottom