Hilo ni balaa Ndugu yangu, hakikisha unamtoa kwenye hiyo imani mpya na arudi Lutheran. Mimi jambo hili lilimikuta mpaka nililazimika kuachana mke wangu niliyezaa naye watoto wawili.
Ilianza hivyohivyo Kama utani, aliacha kusali katoliki na kujiunga na hayo makanisa ya kilolole, akawa na ratiba za kila siku kwenda kanisani, usiku anaamka na kuanza kuomba kwa sauti, nikampiga marufuku kuomba usiku kwa sababu ulikuwa ni usumbufu mkubwa na nilikuwa nashindwa kulala, akaamia sebuleni kuendelea kuomba kila siku usiku wa saa nane na kuendelea.
Kero ilizidi na ikawa siku nyingine anasema wana mfungo na wanalala hukohuko kanisani kwao, ukimkataza kwenda kulala huko kunakuwa na ugomvi mkubwa na ndani maelewano hakuna.
Kiujumla alibadilika sana tabia yake na akawa jeuri Sana, mbaya zaidi Kama wewe mwamaume utakuwa mbali na hilo kanisa analosali utapigwa vita kutoka huko kanisani kwao.
Mimi niliambiwa kuwa amembiwa na mchungaji wake kuwa sio chaguo sahihi na MUNGU atamletea mume sahihi, nilishangaa Sana, kwa ujumla matatizo yalikuwa mengi na yote siwezi kuyaelezea hapa, ila mimi nakushauri mapema Kama unataka ndoa yenu idumu, ama na wewe uingie hilo kanisa au yeye atoke hilo kanisa na arudi Lutheran.
Ilianza hivyohivyo Kama utani, aliacha kusali katoliki na kujiunga na hayo makanisa ya kilolole, akawa na ratiba za kila siku kwenda kanisani, usiku anaamka na kuanza kuomba kwa sauti, nikampiga marufuku kuomba usiku kwa sababu ulikuwa ni usumbufu mkubwa na nilikuwa nashindwa kulala, akaamia sebuleni kuendelea kuomba kila siku usiku wa saa nane na kuendelea.
Kero ilizidi na ikawa siku nyingine anasema wana mfungo na wanalala hukohuko kanisani kwao, ukimkataza kwenda kulala huko kunakuwa na ugomvi mkubwa na ndani maelewano hakuna.
Kiujumla alibadilika sana tabia yake na akawa jeuri Sana, mbaya zaidi Kama wewe mwamaume utakuwa mbali na hilo kanisa analosali utapigwa vita kutoka huko kanisani kwao.
Mimi niliambiwa kuwa amembiwa na mchungaji wake kuwa sio chaguo sahihi na MUNGU atamletea mume sahihi, nilishangaa Sana, kwa ujumla matatizo yalikuwa mengi na yote siwezi kuyaelezea hapa, ila mimi nakushauri mapema Kama unataka ndoa yenu idumu, ama na wewe uingie hilo kanisa au yeye atoke hilo kanisa na arudi Lutheran.