Jeanclaude
JF-Expert Member
- Aug 30, 2013
- 259
- 238
Wadau, kuna dada mdogo hivi wa miaka 21 mke wa mtu ambaye hunisumbua akitaka kampani yangu hata kunitembelea weekend kwa kuwa mimi sijaoa. Mwanzoni alikuja kwangu kuomba ushauri juu ya manyanyaso anayofanyiwa na mumewe lakini sasa amefikia hatua ya kunitamkia wazi wazi kuwa anataka nitoke naye. Nilimwambia siwezi kutoa ushauri wa maana kuhusu ndoa wakati mimi mwenyewe sijaingia huko, nikamshauri awatafute watu wazima wao watakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi kiushauri kuliko mimi. Nimekuja hapa kuomba ushauri namna ya kumuepuka maana tupo ofisi zinazopakana hivyo kuonana huwa mara kwa mara.