Mke, Mama na Muajiriwa - Unashika lipi?

Mke, Mama na Muajiriwa - Unashika lipi?

Ndio maana mi nasema kama hakuna kazi inayoweza kumuhakikishia mke at least masaa manne nyumbani ambapo watoto wanakuwa macho, then bora asifanye kazi. Halafu kuna kina mama wengine sijui walilishwa miguu ya kuku?!... Vikao vya harusi vyote yumo, na vya send-off na kitchen party, yeye ndiye mtoa mada kwenye kila kitchen party, kwenye upatu yumo, saluni masaa sita kila wiki, sokoni masaa kumi kila wiki, sijui wapi na wapi!!! yaani hata kama kazi haimbani, lakini kutulia na watoto nyumbani kwake mwiko....
ha haaaa, umenikumbusha kitu hapa Tuko
 
Last edited by a moderator:
Habari wadau? Natumaini mna enjoy weekend yenu vizuri.
Kwa muda mrefu sana ninatafakari nafasi yangu kama mama katika familia, naona umuhimu wa mama kuwepo nyumbani muda mwingi ili kuangalia mambo yanavyokwenda hapo nyumbani yahusuyo afya ya watoto, mume, chakula, usafi wa nyumba n.k na nimeshuhudia familia nyingi ambazo mama anakuwepo muda mrefu zina maendeleo mazuri tu, ni mara chache kukuta watoto watukutu au wenye tabia za hovyo hovyo kwani mama anasimamia vema nidhamu ya familia. Japo zipo pia familia CHACHE hata mama ashinde masaa 24 mambo bado yatakuwa hovyo!

Sasa basi huu utandawazi umetushika pabaya wanawake, na sisi tunataka kutumia elimu zetu kwa kuajiriwa maofisini, binafsi naona hakuna ubaya hapo kwani ni kuongeza kipato kwa familia. Kinachonitatiza ni pale ambapo majukumu haya mawili yanapoingiliana na kuharibu mfumo mzima wa maisha. Mfano hai: Mimi ni mama na pia nimeajiriwa, najikuta niko njia panda wakati huu ambapo nina watoto wananihitaji nyumbani kuangalia maendeleo yao na mume pia angependa kuhudumiwa na mkewe na kufanyiwa mengine mengi badala ya kuajiri housegirl, na kazini ndio hivyo tena kuanzia asubuhi hadi jioni kama sio usiku, unaondoka watoto wamelala unarudi wamelala! Familia unaipenda na kazi unaitaka, hapo unajigawaje? Kuna mambo mengi sana yanatokea nyumbani tunapowaacha watoto wetu na housegirl kwani hawana uwezo wa ku-handle mambo hayo kama ambavyo mama angefanya.

Wenye situation kama hii plz tupeane mawazo, mnakabiliana vipi na majukumu haya yote mawili? hata wanaume pia mko katika msimamo upi, unataka mkeo aende kazini na kuacha nyumba mikononi mwa housegirl au abaki akusubiri ulete kila kitu (bila kumnyanyasa!).
NB: Najua wapo watakaozungumzia kujiajiri lakini huko nako pia nina mengine mengi ya kueleza.

Ningumu ila you have to accept the reality na kuona kua ndio part n parcel of ur life.
Cha msingi inabidi uwe panctual kama unatoka ofcn sa 11 jioni hakikisha mda huo unatoka kweli na moja kwa moja home sio unapitiapitia mahali. Pia weekend kama huendi kazini hakikisha u spend all the time wit ur family,usiwe na kutokatoka mara kwa huyu mara kule kama ni lazima sana toka na wanao na mmeo. so everytime ur free use it wit ur family not friends or kzurura. na unapokua home fanya majukumu yako acha kusema nimechoka au vipi coz naamini hubebi zege. ila kama mumeo mwelewa pia inakua rahisi unless unafanya kazi halaf humsaidii hapo hataona faida ya ww kuchelewa home.
"EVERY FREE MOMENT U GET SPEND WIT UR FFAMILY"
 
Kipi hicho dia?
hicho cha kuzura mchana kutwa, lol!
afadhali hata wamama wanaoenda ofisini utasema kashinda ofisini, kuna wamama wa nyumbani hawashindi home, kutwa mitaani
 
''mwanaume atakula kwa jasho na mwanamke atazaa kwa uchungu''

ukirudi sana kwenye historia ya mwanadamu wa kale kwenye maandiko (biblia) wanawake hawakuruhusiwa kufanya kazi kama wafanyazo leo, walibaki nyumbani kulea familia na kumtunza vyema mumewe.

Kadiri maisha ambayo yamekuwa yakienda maisha yamekuwa yakibadilika na hii tamaduni imebaki kwa jamii flani flani hivi.
Wazazi hawakai tena na watoto wao, wanaplekwa ''day care'' au wanabaki na wafanyakazi wa ndani. Mama anatoka alifajiri, anarejea usiku, baba hivyo hivyo. Weekend ndio zinzfanyika baadhi ya kazi nyumbani, wanaishia kwenye vikao na sherehe, week nyingine inaanza, mwaka ........

Hakuna muda wa kukukaa na familia, hakuna muda wa kumfundisha mtoto/watoto, hakuna muda wakujifunza neno la mungu na familia, hakuna muda wa kupitia aliyofundishwa mtoto shuleni, hakuna muda wa kupumzika na mume, hapo bado hujaweka stress za makazini, sijui boss ananitaka mara nimekatalia anatak nifukuzwe kazi.... You name them. Full mateso.

Maisha bila kujipanga na kutafakari furaha yako iliko na kuipalilia, yatakuwa ni adhabu na ndivyo yanavyokuwa kwa wengi. Watato sio watoto tena, familia sio familia tena.

Ni changamoto kwangu kama bachelor, na kwako ulie kwenye ndoa, tunaokoaje familia zetu? Hasa sisi wanaume ambao ndio providers.
yafikirieni sana kwa kina maisha yatakayoikumba familia yako iwapo wewe baba ambaye umemweka mkeo nyumbani goli kipa hajui kuitafuta hata sent tano maisha ya baada ya wewe kufa yatakwenda ??je mwanamke huyo ataimudu familia ???acheni utani jamani wacheni wanawake wafanye kazi na umjenge kuweza kuitunza familia ukiwa haipo familia isitetereke mpaka iwe gumzo mtaani!!
 
Nivea, kama umeichki kwa makini nimeeleza tulioanzia hadi tunakokwenda tokea mwanadamu wa kale. na kwanini kazi imekuja kuchukua muda wa malezi.

Nikuhakikishie, ukiishi maisha ya kuajiriwa pekee bila kufanya kitu kingine pembeni utaishia tu kuwa na hela ya kubadilisha mboga hadi mtu unazeeka na ka pensheni. idara nilyoko naona watu na vitambi vyao wanavyokuja kulilia mikopo ya ada na kodi ya nyumba pamoja na kulipwa mishahara mikubwa. so mshahara sio mkombozi bado bali naona kujiajiri mwenyewe inalipa na mtu unakuwa huru sana na muda na vitu vingine.

point yangu ni hii, kama shida ya kuajiriwa ni kutafuta pesa, ni bora mkapanga projects za nyumbani ambazo mke atasimamia na nyingine mme au wote kwa pamoja. unaweza kufikiri iko ki-theory zaidi, lakini those who believe on them selves wamefika and i have some few role models.

Bro wetu mmoja (alikuwa ameajiriwa) akalima eka 30 ya mpunga hapo morogoro, Mungu saidia akapata milioni zake kadhaa almost 200% faida kwa kila hekta. amefungua miradi yake, kaweka wafanyakazi na mke wake ndiye anaendesha mradi mmoja wapo tena kwa mafanikio sana. Mkewe alikuwa mtu wa masoko kabenk kamoja hapa mjini lakini aliacha kazi mwenyewe kuja kumpa nguvu mumewe, na sasa wameajiri watu zadi ya 10 (kwenye pesa points nazozijua bado wana miradi mingine) mke sasa hayupo confined na mastress ya kuajiriwa na anaweza panga mambo yake ya familia kwa uhuru zaidi so these things vipo kwa wachache wanaotaka kuwa hivyo.

Najua ni changamoto kubwa kwa kizazi cha leo, kwa binafsi yangu nachukia kuajiriwa lakini kwa sasa niko kwa ajira strategically (napenda kuwa huru) na naamini nikiweka juhudi naweza kufanya kile ninachokitamani na kukipanga.

yafikirieni sana kwa kina maisha yatakayoikumba familia yako iwapo wewe baba ambaye umemweka mkeo nyumbani goli kipa hajui kuitafuta hata sent tano maisha ya baada ya wewe kufa yatakwenda ??je mwanamke huyo ataimudu familia ???acheni utani jamani wacheni wanawake wafanye kazi na umjenge kuweza kuitunza familia ukiwa haipo familia isitetereke mpaka iwe gumzo mtaani!!
 
Nivea,
kama umeichki kwa makini nimeeleza tulioanzia hadi tunakokwenda tokea
mwanadamu wa kale. na kwanini kazi imekuja kuchukua muda wa malezi.

Nikuhakikishie, ukiishi maisha ya kuajiriwa pekee bila kufanya kitu
kingine pembeni utaishia tu kuwa na hela ya kubadilisha mboga hadi mtu
unazeeka na ka pensheni. idara nilyoko naona watu na vitambi vyao
wanavyokuja kulilia mikopo ya ada na kodi ya nyumba pamoja na kulipwa
mishahara mikubwa. so mshahara sio mkombozi bado bali naona kujiajiri
mwenyewe inalipa na mtu unakuwa huru sana na muda na vitu vingine.

point yangu ni hii, kama shida ya kuajiriwa ni kutafuta pesa, ni bora
mkapanga projects za nyumbani ambazo mke atasimamia na nyingine mme au
wote kwa pamoja. unaweza kufikiri iko ki-theory zaidi, lakini those who
believe on them selves wamefika and i have some few role models.

Bro wetu mmoja (alikuwa ameajiriwa) akalima eka 30 ya mpunga hapo
morogoro, Mungu saidia akapata milioni zake kadhaa almost 200% faida kwa
kila hekta. amefungua miradi yake, kaweka wafanyakazi na mke wake ndiye
anaendesha mradi mmoja wapo tena kwa mafanikio sana. Mkewe alikuwa mtu
wa masoko kabenk kamoja hapa mjini lakini aliacha kazi mwenyewe kuja
kumpa nguvu mumewe, na sasa wameajiri watu zadi ya 10 (kwenye pesa
points nazozijua bado wana miradi mingine) mke sasa hayupo confined na
mastress ya kuajiriwa na anaweza panga mambo yake ya familia kwa uhuru
zaidi so these things vipo kwa wachache wanaotaka kuwa hivyo.

Najua ni changamoto kubwa kwa kizazi cha leo, kwa binafsi yangu nachukia
kuajiriwa lakini kwa sasa niko kwa ajira strategically (napenda kuwa
huru) na naamini nikiweka juhudi naweza kufanya kile ninachokitamani na
kukipanga.

I like ur best ideas!
 
Back
Top Bottom