Mke, Mama na Muajiriwa - Unashika lipi?

Mke, Mama na Muajiriwa - Unashika lipi?

Nyleptha

Member
Joined
Jun 19, 2012
Posts
69
Reaction score
47
Habari wadau? Natumaini mna enjoy weekend yenu vizuri.
Kwa muda mrefu sana ninatafakari nafasi yangu kama mama katika familia, naona umuhimu wa mama kuwepo nyumbani muda mwingi ili kuangalia mambo yanavyokwenda hapo nyumbani yahusuyo afya ya watoto, mume, chakula, usafi wa nyumba n.k na nimeshuhudia familia nyingi ambazo mama anakuwepo muda mrefu zina maendeleo mazuri tu, ni mara chache kukuta watoto watukutu au wenye tabia za hovyo hovyo kwani mama anasimamia vema nidhamu ya familia. Japo zipo pia familia CHACHE hata mama ashinde masaa 24 mambo bado yatakuwa hovyo!

Sasa basi huu utandawazi umetushika pabaya wanawake, na sisi tunataka kutumia elimu zetu kwa kuajiriwa maofisini, binafsi naona hakuna ubaya hapo kwani ni kuongeza kipato kwa familia. Kinachonitatiza ni pale ambapo majukumu haya mawili yanapoingiliana na kuharibu mfumo mzima wa maisha. Mfano hai: Mimi ni mama na pia nimeajiriwa, najikuta niko njia panda wakati huu ambapo nina watoto wananihitaji nyumbani kuangalia maendeleo yao na mume pia angependa kuhudumiwa na mkewe na kufanyiwa mengine mengi badala ya kuajiri housegirl, na kazini ndio hivyo tena kuanzia asubuhi hadi jioni kama sio usiku, unaondoka watoto wamelala unarudi wamelala! Familia unaipenda na kazi unaitaka, hapo unajigawaje? Kuna mambo mengi sana yanatokea nyumbani tunapowaacha watoto wetu na housegirl kwani hawana uwezo wa ku-handle mambo hayo kama ambavyo mama angefanya.

Wenye situation kama hii plz tupeane mawazo, mnakabiliana vipi na majukumu haya yote mawili? hata wanaume pia mko katika msimamo upi, unataka mkeo aende kazini na kuacha nyumba mikononi mwa housegirl au abaki akusubiri ulete kila kitu (bila kumnyanyasa!).
NB: Najua wapo watakaozungumzia kujiajiri lakini huko nako pia nina mengine mengi ya kueleza.
 
Kwa ufupi sana nianze na preference zangu kuhusu uafadhali wa mke... Mwenye kipato lakini yupo available nyumbani > aliyepo available lakini hana kipato> mwenye kipato lakini hayupo available...
 
Kiukwel gharama za kuishi na watoto waliolelewa kiholela holela ni kubwa kuliko kuishi bila kipato...
 
Kiukwel gharama za kuishi na watoto waliolelewa kiholela holela ni kubwa kuliko kuishi bila kipato...

Nakubaliana nawe. Kwa hiyo wewe ungependelea wife asimame upande upi?
 
Nakubaliana nawe. Kwa hiyo wewe ungependelea wife asimame upande upi?

Bora asacrifice kaz yeyote itakayomuondolea uwepo walau kwa masaa 4 ya muda ambao watoto wanakuwa macho...
 
Hakuna cha kuchagua yote yanawezekana ku-work around it.., kwahio yoyote atakayepatikana (anachofanya) familia itaendeshwa kulingana na yeye anachofanya.., Specialization and Division of Labour.., kama mama anafanya kazi (busy) majukumu mengine anaweza kuchukua aliyopo nyumbani au msaidizi (by the way sidhani hata kama huyo mama yupo kazini anafanya kazi 24/7 ; 365 days a years
 
mimi kama mke, mama, na mwajiriwa lazima nipange muda wangu vzr wa kuwa na familia, mume na watoto. Mume pia

anajua kuwa mke wangu ni mwajiriwa hivyo hawezi kufanya kila kitu kama mama wa nyumban. kinachofanyika ni

kusaidina mimi na yy ktk malezi ya watoto wetu + uwepo wa HG. Kwakuwa tumeliona suala la mm kufanya kazi ni bora

zaidi hivyo tunajituma sn kuilea familia na kuelekezana pale tunapoona 1 ameanza kulega. Nashukuru mungu maisha

yanakwenda vzr, watt wana adabu, na afya njema.
 
Kwa mwenendo wa sasa wa maisha hatuna budi kukubali kuendeshwa na mfumo! Swala la ajira/kujiajiri ni muuhimu kwa ustawi wa family na uangalizi wa karibu wa family nao ni essential as well...Nionavyo ni kugawa vipaumbele vyema kwa maana ya muda gani unastahili kuwepo wapi na ukifanya nini...Thus all
 
''Mwanaume atakula kwa jasho na mwanamke atazaa kwa uchungu''

Ukirudi sana kwenye historia ya mwanadamu wa kale kwenye maandiko (Biblia) wanawake hawakuruhusiwa kufanya kazi kama wafanyazo leo, walibaki nyumbani kulea familia na kumtunza vyema mumewe.

kadiri maisha ambayo yamekuwa yakienda maisha yamekuwa yakibadilika na hii tamaduni imebaki kwa jamii flani flani hivi.
Wazazi hawakai tena na watoto wao, wanaplekwa ''day care'' au wanabaki na wafanyakazi wa ndani. Mama anatoka alifajiri, anarejea usiku, baba hivyo hivyo. weekend ndio zinzfanyika baadhi ya kazi nyumbani, wanaishia kwenye vikao na sherehe, week nyingine inaanza, mwaka ........

Hakuna muda wa kukukaa na familia, hakuna muda wa kumfundisha mtoto/watoto, hakuna muda wakujifunza neno la Mungu na familia, hakuna muda wa kupitia aliyofundishwa mtoto shuleni, hakuna muda wa kupumzika na mume, hapo bado hujaweka stress za makazini, sijui boss ananitaka mara nimekatalia anatak nifukuzwe kazi.... you name them. Full mateso.

Maisha bila kujipanga na kutafakari furaha yako iliko na kuipalilia, yatakuwa ni adhabu na ndivyo yanavyokuwa kwa wengi. Watato sio watoto tena, familia sio familia tena.

Ni changamoto kwangu kama bachelor, na kwako ulie kwenye ndoa, Tunaokoaje familia zetu? Hasa sisi WANAUME ambao ndio providers.
Kiukwel gharama za kuishi na watoto waliolelewa kiholela holela ni kubwa kuliko kuishi bila kipato...
 
Hongera sana.

Unadhani kama Mumeo angekuwa na uwezo wa kutosha (kila kitu chapatikana na una uhakika wa kesho)
Bado kazi ya kuajiriwa ingeendelea kuwa priority kwako?

mimi kama mke, mama, na mwajiriwa lazima nipange muda wangu vzr wa kuwa na familia, mume na watoto. Mume pia

anajua kuwa mke wangu ni mwajiriwa hivyo hawezi kufanya kila kitu kama mama wa nyumban. kinachofanyika ni

kusaidina mimi na yy ktk malezi ya watoto wetu + uwepo wa HG. Kwakuwa tumeliona suala la mm kufanya kazi ni bora

zaidi hivyo tunajituma sn kuilea familia na kuelekezana pale tunapoona 1 ameanza kulega. Nashukuru mungu maisha

yanakwenda vzr, watt wana adabu, na afya njema.
 
''Mwanaume atakula kwa jasho na mwanamke atazaa kwa uchungu''

Ukirudi sana kwenye historia ya mwanadamu wa kale kwenye maandiko (Biblia) wanawake hawakuruhusiwa kufanya kazi kama wafanyazo leo, walibaki nyumbani kulea familia na kumtunza vyema mumewe.

kadiri maisha ambayo yamekuwa yakienda maisha yamekuwa yakibadilika na hii tamaduni imebaki kwa jamii flani flani hivi.
Wazazi hawakai tena na watoto wao, wanaplekwa ''day care'' au wanabaki na wafanyakazi wa ndani. Mama anatoka alifajiri, anarejea usiku, baba hivyo hivyo. weekend ndio zinzfanyika baadhi ya kazi nyumbani, wanaishia kwenye vikao na sherehe, week nyingine inaanza, mwaka ........

Hakuna muda wa kukukaa na familia, hakuna muda wa kumfundisha mtoto/watoto, hakuna muda wakujifunza neno la Mungu na familia, hakuna muda wa kupitia aliyofundishwa mtoto shuleni, hakuna muda wa kupumzika na mume, hapo bado hujaweka stress za makazini, sijui boss ananitaka mara nimekatalia anatak nifukuzwe kazi.... you name them. Full mateso.

Maisha bila kujipanga na kutafakari furaha yako iliko na kuipalilia, yatakuwa ni adhabu na ndivyo yanavyokuwa kwa wengi. Watato sio watoto tena, familia sio familia tena.

Ni changamoto kwangu kama bachelor, na kwako ulie kwenye ndoa, Tunaokoaje familia zetu? Hasa sisi WANAUME ambao ndio providers.

Well said, ni utandawazi ndio unatufanya wanawake tuingie kwenye mambo mengine kibao ambaya wazee wetu zamani hawakuwa wakiyafanya, walitulea vizuri sana na tuliridhika na kipato. Watoto wetu wanapata tabu sana, wanalelewa na housegirls wasio na uzoefu wowote wanafanya lolote ili mradi mwajiri aridhike, mzazi anaona solution ni kupeleka katoto ka miaka miwili day care centre, huko kanajifunza kila kitu kibaya na kizuri, mwisho wa siku mzazi anakuja kushtuka mtoto ana kila aina ya tabia na haiwezekani tena kurekebishika!
Kwenu bachelors, kabla ya kuoa hakikisheni mmejipanga kuweza kuprovide mahitaji ya familia zenu na pia kukubaliana na mwenzi wako kama atakaa kulea watoto (japo wanawake tumekuwa wabishi sana siku hizi!loh) au utakubali aende kazini masaa 12 ndipo arudi nyumbani, au mkubaliane kabisa kuwa unafungua mradi atakauendesha ambao hautamcost masaa yake 12 mbali na nyumbani! Familia nyingi huishia kulaumiana kwa matendo mabaya ya watoto kwamba mama au baba ndio amesababisha kumbe chanzo ni hiki, baba na mama wako busy kutafuta hela huku watoto wanajilea wenyewe!
 
Hongera sana.

Unadhani kama Mumeo angekuwa na uwezo wa kutosha (kila kitu chapatikana na una uhakika wa kesho)
Bado kazi ya kuajiriwa ingeendelea kuwa priority kwako?

wewe acha tu, wakati mwingine hatuendi kazini kwaajili ya mshahara tu, sababu nyingine ni 'status'! wengi tunadhani nikionekana nimeajiriwa sehemu fulani basi mimi ni tofauti na yule anayekaa nyumbani, anaonekana elimu yake haijamsadia, mimi nimesoma lazima nitumie elimu yangu, n.k n.k haya mambo ndio yanatucost sana. Wanawake tunapaswa kutafuta 'status' kwa namna nyingine, japo mara zote nyie wanaume ndio mnachangia, wewe bachelor hebu fikiria unataka kuoa na umekutana na warembo wawili, mmoja ameajiriwa mwingine yupo yupo tu home, wa kwanza kumfikiria atakuwa yupi? si utaona huyu kula kulala ni mvivu!
 
Asante sana, Kwa kwa juhudi zangu na Msaada wa Bwana, NItakuwa.

We are who we are from the daily choices and actions we make, If we dont change our actions and choices, hakuna chochote kitakachobadilika. Najifunza polepole kubadili choices na action zangu kwa kweli, Natamani familia yangu iwe first priority, hio ndio nyama katika nyama yangu na mfupa mfupani mwangu, Tutakuwa na cha kujibu mbele ya MUNGU kama hatutawalea watoto wetu ipasavyo. Asante kwa changamoto hii,inatujenga


Well said, ni utandawazi ndio unatufanya wanawake tuingie kwenye mambo mengine kibao ambaya wazee wetu zamani hawakuwa wakiyafanya, walitulea vizuri sana na tuliridhika na kipato. Watoto wetu wanapata tabu sana, wanalelewa na housegirls wasio na uzoefu wowote wanafanya lolote ili mradi mwajiri aridhike, mzazi anaona solution ni kupeleka katoto ka miaka miwili day care centre, huko kanajifunza kila kitu kibaya na kizuri, mwisho wa siku mzazi anakuja kushtuka mtoto ana kila aina ya tabia na haiwezekani tena kurekebishika!
Kwenu bachelors, kabla ya kuoa hakikisheni mmejipanga kuweza kuprovide mahitaji ya familia zenu na pia kukubaliana na mwenzi wako kama atakaa kulea watoto (japo wanawake tumekuwa wabishi sana siku hizi!loh) au utakubali aende kazini masaa 12 ndipo arudi nyumbani, au mkubaliane kabisa kuwa unafungua mradi atakauendesha ambao hautamcost masaa yake 12 mbali na nyumbani! Familia nyingi huishia kulaumiana kwa matendo mabaya ya watoto kwamba mama au baba ndio amesababisha kumbe chanzo ni hiki, baba na mama wako busy kutafuta hela huku watoto wanajilea wenyewe!
 
wewe acha tu, wakati mwingine hatuendi kazini kwaajili ya mshahara tu, sababu nyingine ni 'status'! wengi tunadhani nikionekana nimeajiriwa sehemu fulani basi mimi ni tofauti na yule anayekaa nyumbani, anaonekana elimu yake haijamsadia, mimi nimesoma lazima nitumie elimu yangu, n.k n.k haya mambo ndio yanatucost sana. Wanawake tunapaswa kutafuta 'status' kwa namna nyingine, japo mara zote nyie wanaume ndio mnachangia, wewe bachelor hebu fikiria unataka kuoa na umekutana na warembo wawili, mmoja ameajiriwa mwingine yupo yupo tu home, wa kwanza kumfikiria atakuwa yupi? si utaona huyu kula kulala ni mvivu!

Hizi zinaitwa busara za mwanamke wa ukweli..
BIG UP mamaa..
 
Hongera sana.

Unadhani kama Mumeo angekuwa na uwezo wa kutosha (kila kitu chapatikana na una uhakika wa kesho)
Bado kazi ya kuajiriwa ingeendelea kuwa priority kwako?

Mbona mume wangu ana uwezo wa kutosha kila kitu kipo. Mshahara wangu nautumiaga mwenyewe na yy huniongezea.

kazi kwangu ni muhimu bse, nimesoma na napenda kuwahudumia watu kwa elimu niliyoipata. Mfano, nimepata matatizo

job kwangu cjapata salary mume wangu kaniambia nitakupa huo mshahara na hela za matumizi pia.
 
wewe acha tu, wakati mwingine hatuendi kazini kwaajili ya mshahara tu, sababu nyingine ni 'status'! wengi tunadhani nikionekana nimeajiriwa sehemu fulani basi mimi ni tofauti na yule anayekaa nyumbani, anaonekana elimu yake haijamsadia, mimi nimesoma lazima nitumie elimu yangu, n.k n.k haya mambo ndio yanatucost sana. Wanawake tunapaswa kutafuta 'status' kwa namna nyingine, japo mara zote nyie wanaume ndio mnachangia, wewe bachelor hebu fikiria unataka kuoa na umekutana na warembo wawili, mmoja ameajiriwa mwingine yupo yupo tu home, wa kwanza kumfikiria atakuwa yupi? si utaona huyu kula kulala ni mvivu!

binafsi siendi job kwasababu ya status, wazazi wangu walinisomesha ili baadae niweze kuitumia elimu yangu ktk mambo

mbalimbali. najisikia faraja kuwahudumia wananchi wa hali ya chini kwa elimu yangu mkuu. nisipokwenda job ni kama

nimepungukiwa kitu muhimu sn bse kuna watu wanahitaji kusaidiwa na wasomi na mm ni mmoja wao.
 
Nimekupenda bure dada yangu Nyleptha.

Kwa kweli tumekuwa tukifanya maamuzi mengi sana ya mkumbo, Tumeshindwa kujua na kuthamini vile vya thamani sana kwetu. Wanaume tunahusika sana kwa upande wetu, na inatupasa kujipanga kusustain familia zetu.

Kwenye RED nachunga sana AMANI yangu ya ndani, napenda sana kusikiliza mtu wangu wa ndani. . (nilipomailiza chuo niiunga job, nikakaa 2 years bila hata kuomba kazi sehemu nyingine japo niliyokuwa nayo sikuipenda, zilitoka za TRA, NAO na nyingine nyingi, lakini katu mtu wa ndani hakunipa amani kuaply, one day nikaona tangazo kwenye gazeti nikapata amani ya kuaply, tulikuwa candidates 400+ tukapatikana 6)

Point yangu ni kuwa, Amani yetu ya ndani huwa haidanganyi, si kuwa ningeomba tra/nao na nyingine ningekosa,NO, am sure ningepata; lakini Kazi ni zaidi ya jina, mshahara na marupurupu (wachache watanielewa hapa) Same swala na mwenza, AMANI ya ndani ndio ya kuzingatia.

wewe acha tu, wakati mwingine hatuendi kazini kwaajili ya mshahara tu, sababu nyingine ni 'status'! wengi tunadhani nikionekana nimeajiriwa sehemu fulani basi mimi ni tofauti na yule anayekaa nyumbani, anaonekana elimu yake haijamsadia, mimi nimesoma lazima nitumie elimu yangu, n.k n.k haya mambo ndio yanatucost sana. Wanawake tunapaswa kutafuta 'status' kwa namna nyingine, japo mara zote nyie wanaume ndio mnachangia, wewe bachelor hebu fikiria unataka kuoa na umekutana na warembo wawili, mmoja ameajiriwa mwingine yupo yupo tu home, wa kwanza kumfikiria atakuwa yupi? si utaona huyu kula kulala ni mvivu!
 
Nyleptha mawazo yako ni mazuri sana mama kuwapa watoto wake malezi mema yanayositahili,lakini mimi napata shida kama huko tunakoenda itakuwaje kama akina mama watarajiwa ndo hao tunao walea kama mayai dada mkubwa hajui hata kupika kisa house girl atafanya kazi,nilipata kwenda field sehemu fulani na akinadada ajabu ni kwamba baadhi yao hawakuwa wanajua hata kupika ndo kuanza kufundishwa.

lakini ukiangalia hawa wanaotarajiwa kuja kulea familia zao ndo hao wanaovaa nusi uchi,maziwa njenje kupost picha za uchi facebook,wanaumme nao ndo hao kuvaa huku chupi ama ------ yakiachwa wazi, wanavua nguo na kubakiza chupi kisa anapagawisha mashabiki! ukiongea ukweli watakushambulia kwa matusi mazitomazito......kama wange kuwa na mtazamo kama wako watoto wasinge haribika....heri ni mmeo maana amepata mke mwema.
 
''Mwanaume atakula kwa jasho na mwanamke atazaa kwa uchungu''

Ukirudi sana kwenye historia ya mwanadamu wa kale kwenye maandiko (Biblia) wanawake hawakuruhusiwa kufanya kazi kama wafanyazo leo, walibaki nyumbani kulea familia na kumtunza vyema mumewe.

kadiri maisha ambayo yamekuwa yakienda maisha yamekuwa yakibadilika na hii tamaduni imebaki kwa jamii flani flani hivi.
Wazazi hawakai tena na watoto wao, wanaplekwa ''day care'' au wanabaki na wafanyakazi wa ndani. Mama anatoka alifajiri, anarejea usiku, baba hivyo hivyo. weekend ndio zinzfanyika baadhi ya kazi nyumbani, wanaishia kwenye vikao na sherehe, week nyingine inaanza, mwaka ........

Hakuna muda wa kukukaa na familia, hakuna muda wa kumfundisha mtoto/watoto, hakuna muda wakujifunza neno la Mungu na familia, hakuna muda wa kupitia aliyofundishwa mtoto shuleni, hakuna muda wa kupumzika na mume, hapo bado hujaweka stress za makazini, sijui boss ananitaka mara nimekatalia anatak nifukuzwe kazi.... you name them. Full mateso.

Maisha bila kujipanga na kutafakari furaha yako iliko na kuipalilia, yatakuwa ni adhabu na ndivyo yanavyokuwa kwa wengi. Watato sio watoto tena, familia sio familia tena.

Ni changamoto kwangu kama bachelor, na kwako ulie kwenye ndoa, Tunaokoaje familia zetu? Hasa sisi WANAUME ambao ndio providers.

Na mojawapo ya impacts zake, watoto waliolelewa katika mazingira ya hivyo baadae hawaoni umuhimu wa kuwa na familia. wanaishia kuwa watu wa vijiweni.. kuoe na kuolewa kwao inakuwa kitu kisicho na maana...
 
La! Nimejikuta nimelog in ghafla. Namuonea wivu mumemo maana kwa busara hizi ni wazi kua wewe ni mke mwema. Yaani kila siku zingekua zinajadiliwa mada kama hizi hapa basi maisha yetu yangebadilika sana na tungepiga hatua kubwa ya ukombozi wa kifikra ambao ungetuletea maendeleo zaidi.
BACK TO THE TOPIC!!
Mimi nadhani kuna watu wana mtazamo mdogo sana kuhusu elimu zao. Mtu anadai kua amesomeshwa na wazazi wake ili aje kuitumia hiyo elimu yake. Well,naunga mkono.Lakini huyu mtu hajajua kwamba hiyo elimu inapaswa kumsaidia kwanza katika malezi ya familia yake. Na ni kwamba sio lazima kamba ukisoma mpaka chuo kikuu ukaajiriwe, la hasha! Maana yake ni kwamba tumia hiyo elimu katika kung'amua mazingira yako ya kawaida ili uwe na maisha yenye furaha wewe na familia yako. Mfano; kuna mama mmoja aliamua kuacha kazi mahali ambapo kimsingi walikua wanalipa vizuri ila alikua busy asbh mpaka jioni hivyo akawa anakosa muda wa kukaa na familia yake na kuhamia sehemu nyingine ambapo alikua anatoka kazini saa tisa na kurudi kulea familia yake pamoja na mumewe. Huyu mama hapo alipohamiawalikua wanalipa kidogo ukilinganisha na alipotoka. Baada ya muda wa miezi kama mitano huyu mama alipandishwa cheo na kupata mshahara mkubwa zaidi. Huyu mama akawa ana faida kuu mbili;Analea familia yake vzuri na mshahara unatosha. Hapa binafsi nashauri tumieni elimu zenu ktk kuleta furaha mioyoni mwenu na ktk familia zenu.
 
Back
Top Bottom