MKE Ana Tamaa!


Kwani ukiweka Mr & Mrs Ngoshwe ina maana mkiacha au kutengana hilo neno "MRS" linatakusaidia? Kama nilikuwa na ma "MRS" wengine chochi wakaibuka na kusema "mimi ndo MRS mwenyewe" utabisha kama jina lako halipo?. Cha msingi ni kuona kuwa mali na matakataka mengine yote ni ubatili tu na utu wa mtu ni zaidi ya hayo. Mke au Mume ambaye ana anza kuzungumizia masauala ya mali binafis katika ndoa ni hatari sana. Jaribu katika maisha yako yote kutafuta jambo liliko jema ambalo ni kuwaachia watoto urithi wa elimu ambayo haitapotea kamwe, nyumba na gari si urithi mwema!.

Ni busara pia hata kwenu wanawake, kutuhimiza tuzae watoto wa kutosha na kusomesha vizuri, manake ikiwa mtoto amesoma kama mumeo akikuona kimeo na kukuacha, mwanao msomi ataweza kukusaidia ikiwemo hata kukujengea hiyo nyumna na kukununulia hilo kwa jina lako!.
 


ikisemwa iandikwe majina ya watoto hamaanishi kwamba watoto ndio washapewa urithi wao kwa kila kitu, elimu yao ipo pale pale, kama wameanza kuwa na kautofauti hapo c bora waandike jina la mtoto bac....na watoto wa kutosha ni wangapi ngoshwe kama hutajali kuuliza kwa upande wako?
 

ni kweli na si kweli usemayo ngoswe. Nakubali urithi mzuri ni elimu kwa watoto lakini nijuavyo mie elimu ni urithi ni jukumu letu kama wazazi. urithi unawezaamua kuwaachia wanao au lah but elimu ni wajibu wako kuwapatia. Pili nakubaliana nawe kwenye thamani ya mtu, utu but hata mali ina nafasi yake hasa katika maisha ya siku hizi na ndio maana tunakesha na kukimbizana na maboss wakorofi ili tu tupate mali otherwise watu wangekuwa wanafanya kazi kizembe sana.

Najaribu kufikiria kilichopelekea huyu bwana kuleta hii mada hapa!! Pengine angetueleza naye alimjibu nini mkewe juu ya kumwandika jina lake kwa sababu kama alikazania kusema ni nyumba yake aliijenga kabla hawajaoana basi kuna tatizo sehemu flani. Otherwise mh. Ngoswe imagine umeishi na mkeo miaka yoooote hiyo na watoto mmeozesha nawe umestaafu unakula pension tu tuseme ya nyumba zako za kupanga mguu juu kwenye nyumba yako ya Mebzi. Then ghafla kurasa inageuka upside down mnakorofishana na mama yoyoo then bam- mali zote za mama yoyooo - anakutimua sijui ndo wenda kijijini au kwa ndugu yako?? najua kwa wanaume si rahis picha hii ikawaingia kwa kuwa haya yanawatokea wanawake zaidi.
 

hiyo ya kuandika Mr and Mrs nafikiri haijalishi mko wangapi na ndio maana kuna vyeti vya ndoa na kuna ile sehemu ya aina ya ndoa- mke mmoja; wake wengi au huwenda ikawa ya wake wengi. As long as ulitick mke mmoja- hata wapange msururu bado haki yako itakuwa yako kama mke halali wa marehemu oh hayati.
 
Mi naungana na wazo la mkeo. ila sio lazima kwa nyumba hii aliyokukuta nayo,mkiweza kujenga nyingine itakuwa wazo zuri kusovu hii tatizo.nimeona wengi wakifanya hivyo wanandika majina ya wake zao kwenye mali zao. sababu kubwa ni kulinda future yao ikitokea wewe unatangulia mbele ya haki. atakuwa salama kwani ndugu zako hawata mgasi.ikitokea yeye ndo katangulia, hakuna mtu atakuja kutaka kujua mali zenu mlizochuma na mkeo. ila ukitangulia wewe lazima mali zitagawanywa na yeye ndo atakuwa looser.Hivyo mfikirie. kama unaona ni ngumu, basi mwabie asubiri nyumba mtakayojenga nyingine, hii aiache.
 

Bw. Boflo ukicheka na nyani utavuna mabua. Ni wakati muafaka sasa wa kutunga na kumfafanulia mke wako sheria na taratibu za nyumbani kwako na kumwambia kuwa zile za baba yake hazikuhusu.
 

Bw. Ben kwa mujibu wa mwandishi, mapendekezo hayo ya mkewe yalitolewa baada ya "CHAKULA CHA USIKU". Labda mwandishi angefafanua zaidi kama hiki ni chakula cha aina gani. Ni hiki cha ugali na mchuzi au ni lugha tu ya maumbo ikimaanisha kitu kingine.
 
 
Bro unaliwa sasa hivi!! kwani kuna tatizo gani kama nyumba ikibaki kwa jina lako? hata kama mngekua mliijenga wote kama anabusara angependekeza iwe na jina lako ila kitendo cha kuitaka hata hyoo ambayo hana jasho nayo iwe kwa jina lake tyari ni ishara ya ubinafsi. Bro leo mmejadili mkiwa dina angalia siku moja msijadili mkiwa mahakamani!!.

Kama kazoea ya kwa baba yake mwambie mwanmbie awsahau baba na mama yake kwa sasa yupo kwako (kwenu) ambapo sio lazima maisha yafuate mfumo wa huko kwa baba yake.

TAKE CARE BRADA!! UPO MTEGONI.
 
Baada ya kuulizwa hilo swali ungempiga kichwa kama hicho Zidane alichompa Matterazzi.

By the way hii issue iko serious sana, husikubali tu kumwandikisha mwanamke mali kwa jina lake pasipo sababu za msingi.
 
Mpe kichwa kama hicho Zidani anachompa Materazi kwenye avatar yako
 
Maumivu ya kichwa huanza poooole pole na kisha maumivu makali kupita kiasi. Imeandikwa, " ... Mwanamke ataachana na nyumba ya baba yake naye ataambatana na mumewe nao watakuwa mwili mmoja..." sasa kaka kwanini huyu mkeo hataki kuachana na nyumba ya baba yake ( kwa kukutaka wewe ufuate sheria za baba yake)! Mwenye macho haambiwi tazama! Words are enough for the wise!
 
Duu huyu mwanamke yuko in transit si mkaaji hapo brooo.. stuka kaa naye kwa machale huyo
 

1.mwandike tu jina lake au ukubali uuawe.
2.sheria ya ardhi inasema hiyo ni mali yenu wote nini jina?lisikutishe. Ili mladi huyo ni mkeo/mmeo ni mali yake pia,anajisumbua tu.
3.kwani nyie wagumba? Nyumba ya mama watoto wako sio ya wanao?
4.kwanza hiyo itaokoa kudhurumiwa mkeo na ndugu zako waroho pindi ukifa?
5.ndugu zako na mkeo unadhani nani anawapenda zaidi wanao?..ni mkeo...mwandike jina.
6.kumbuka ndugu zako wanaipigia mahesabu nyumba yako,wanawaza utakufa lini.dunia hii ndugu yangu,ukimwandika yeye na wakajua, saaafi,utaitwa zoba ok,mkeo watamchukia ok,utaambiwa umeolewa ok,lakini mali ipo salama hata baada ya kufa. fikiri kwa makini
7.sio unakufa halafu unamwachia matatizo kibaaao.
 
Kawaida ni..... Chako wewe BABA, ni CHENU, Lakini cha MKE ni CHAKE!!!!, Kwa hivyo, ukipeana hio nyumba , nawe utaiona PAAA!!!!!!
 

nasikia kuna makabila hapa tz ukishajiimarisha kidogo tu mama anaa-kukill ili abaki anaitwa mama mwenye nyumba. watch out. Hii ni shari kamili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…