Mke aliniibia katoroka leo anaomba msamaha arudi

Mke aliniibia katoroka leo anaomba msamaha arudi

Yaani mtu kafanya kosa na kukimbia, anarudi kuomba msamaha kwa vitisho still umefumbwa macho na masikio huna??? Kwani mtoto nini bhana...! Hafai hata kwa mchuzi huyo, sema keshaona wewe bwe.ge tu..!!
 
Msamehe ili uwe huru ILA USIRUDIANE nae,atakutesa nakukumiza,mwanamke ambaye anashikiwa akili na mwingine huyo hafai hata kidogo...na anatumia gear ya mtoto ili umrudishe,kwan mwanzo hakuliona hili??kumsamehe haimanaanishi ndio umrudie,msamehe aendelee na maisha aliyochagua...wewe leo mtoto,ikiwezekana tafuta mwanamke mwingine...
 
Yaani mtu kafanya kosa na kukimbia, anarudi kuomba msamaha kwa vitisho still umefumbwa macho na masikio huna??? Kwani mtoto nini bhana...! Hafai hata kwa mchuzi huyo, sema keshaona wewe bwe.ge tu..!!

Eti love is blind
 
Mfyuuuuu

Aende salama. Kuiba kaiba.. karudi wala si kujutia kosa, bali huko atokako yamemshinda. Haitoshi hyo bado anakuja na mikwara!!!

dadekiiii..mleta mada kwani wewe ni Mario????

hebu mwache aende bana kaa
 
Tunafundishwa kusamehe bila kushurutishwa. Kama anakushurutisha ina maana kashajua udhaifu wako, simama imara vitisho siyo mpango katika maisha ya ndoa.
 
Mimi mtoto hatakuja kuwa sababu ya mtu kufanya ujinga akitegemea nitamsamehe ili tulee watoto. Wapo wengi wamelelewa bila Baba, mimi ukiniibia afu umnganganie mtoto utaenda nae tena bila kuzuiwa
 
niliishi na mwanamke tukapata mtoto mmoja ikatokea cku moja nipo kazini kasomba vitu vyote katoroka siku hizi anabembeleza eti nimsamehe shoga yake ndo alimwambia atoroke karudi na mwanangu kwangu nikimfukuza ataondoka na mtoto anadai sitakuja kumpata huyo mtoto tena .kwa upande wa sheria bado anaharali ya kubaki na mtoto yaani mtt yk chini ya miaka saba naombeni ushauri nimtimue mtoto atakuja baadaye kunitafuta au nimsikilizie wakati namlea mtoto wangu? ushauri tafadha

Msamehe tu na yeye ni binadamu shetani kamjaribu ye ye akaingia miguu yote. La msingi nendeni mkapime vvu kabla hujafanya uamuzi huo. Mtoto isiwe kigezo cha maamuzi yako
 
Dawa ya mwanamke ni mwanamke mwenzie...leta kitu kipya ndani,mwenyewe atajua no entry.....arudi huko anakotoka,,,,,,,mpe conditions kuwa mtoto utalea na mkeo mpya au alee utatuma matumizi,........kama ana akili na uchungu wa mwanae atachagua the latter,.......na kukuacha uendelee na maisha yako.....
 
Acha atembee mbele,angekuwa anajutia kosa asingeweka biti la kutomwona mwanao! Halafu, vitu alivyoiba viko wapi?
 
Hiyo muvi imemtokea jirani yangu inafanana sana na yako.

lakini yeye sasa kaoa mwanamke mwingine na maisha yanasonga mbele
 
Back
Top Bottom