Sabayi
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 2,310
- 1,003
Wadau naomba kuuliza kuhusu mkataba wa ushirikiano wa Kiulinzi wa A.Mashariki ambao Tanzania iligoma kuusaini.Mkataba huo ulikuwa unazitaka nchi zote za Afrika Mashariki kuingia vitani ikiwa nchi moja wapo itavamiwa au kuingia Vitani hadi mara ya mwisho kwa kumbukumbu zangu TZ tuligoma ku usaini kwa kuogopa kuingizwa vitani na maraisi wapenda vita kama M7 na Kagame kwa interest zao binafsi,na Kama tulisaini na mazungumzo ya Malawi yakaenda kombo (Kumbuka kuwa jana walijibu kauli ya membe kusimamisha tafiti za mafuta kwa kusema hawapo tayari kusimamisha kwa kuwa hilo ziwa lote ni lao hivyo hawawezi kupangiwa na nchi yeyote) na tukalazimika kuingia nao vitani je Kenya,Uganda,Rwanda na Burundi zitakuwa tayari kuingia vitani na sisi kadri ya mkataba huo? Naomba kuwasalisha