Mkasa Wa Kweli: Umasikini ulivyopelekea nifukue makaburi 100

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,446
Image may contain: sky, ocean, cloud, text and outdoor


Mtunzi:Abyas Mzigua
Sehemu ya kwanza.

"AANH ewe Mungu! Hivi nina mkosi gani mimi? Mbona watoto wa wenzangu wanafanya kazi na kuwalisha wazazi wao? Wa kwangu ana nini? Eti Zakayo, una nini wewe? Au unataka kuja kuolewa?"

"Daah...hapana mama!"

"Ndiyo. Maana kazi kufanya hutaki. Unategemea nini sasa?"

"Si kwamba sitaki , hali imebadilika mama yangu, hali ngumu mno!"

" Hali..nguu...muuu..!"aliigiza kwa kubana pua, kisha akaendelea kufoka,"yani mwanaume mzima, midevu mpaka kwenye viganja vya mikono,unasema kabisa hali ngumu? vijana wa mjini sijui mko vipi!"
Alimaliza na kuusukuma mlango kwa hasira, akatoka nje.

Kwa majina, naitwa Zakayo Mdaki. Ni mtoto wa pekee, wa Marehemu mzee Mdaki Zakayo, aliyefariki miaka kumi iliyopita, kwa ajali ya kugongwa na gari akiwa anaendesha baiskeli yake, jioni...akitokea kibaruani.

Kifo cha mzee wangu kilituacha wawili tu, mimi na mama yangu.
Ambaye alikosa uwezo wa kunipeleka sekondari, baada ya kumaliza darasa la saba. Na badala yake, niligeuka msaidizi katika kajimgahawa chake kidogo cha chakula, kilichokuwepo pembezoni mwa barabara, mitaa ya Magomeni, Mwembechai.

Nilifanya kazi kwa bidii mno, kwa kuwa mgongo wa ndoto zangu, ulishaegemea mgahawa ule.
Nilitamani siku moja ndoto yangu itimie:nipate pesa na kurejea tena shuleni.

Walakini, tamaa hubaki tamaa ikiwa Mungu hakupanga. Hata ukafanya jitihada za kuvuja jasho la damu!

Ndivyo kwangu ilivyokuwa...

Siku wagambo walipoamua kutuvunjia, wakaharibu kila kilicho ndani.
Pesa, vyakula na vyombo vya thamani-walivibeba wakaondoka navyo.

Tulijaribu kufungua mashitaka.
Bila kukumbuka kuwa, 'kila mbuzi hula kwa urefu wa kambaye'.
Hakuna tulichoambulia. Zaidi, tuliuvaa usumbufu wa 'nenda-rudi'.
Mwishowe, tulikata shauri, tukaachana nao.
Kuanzia hapo, mama hakuwa na shughuli nyingine yo yote.
Nikajitwika utoto, ukaka na ubaba...kutafuta vibarua mitaani, walau tupate cha kutupia kinywani.
Mambo yakawa yanasonga.

Tofauti na siku zilizopita!
Maisha ya hivi karibuni, yamegeuka kichwa chini, miguu juu.
Kila ninapojaribu kupapasa-hola!
Na mama ndiyo hivyo,'Ananiona m'bwetekaji tu'.

JIONI moja, nikiwa katika randaranda zangu, nilikutana na rafiki, rafiki wa kitambo sana! Tangu shule ya msingi. Haikuwa rahisi kwangu kumkumbuka.
Alibadilika sana!
Mavazi, muonekano na gari aliyokuwa anaendesha, iliakisi ubora na hadhi yake.
Mwenzangu alinikumbuka vema kabisa.
Labda kutokana na kutobadilika.
Yumkini umasikini ulinidumaza. Nikashindwa kuonesha utofauti;kati ya utoto, ujana na uzee.

Aliniomba tutafute sehemu, tukae ili tuzungumze kidogo. Maana ni muda mrefu hatukutiana machoni.
Hakuna masikini anayekaidi wito wa tajiri.Hakuna!
Au yupo asiyefahamu kuwa,'Mfuata nyuki hurejea na kibuyu chenye asali'?
Natumai hayupo!
Nilipanda garini mwake, tukaianza safari.

Si mbali kihivyo tulipoelekea.
Ilikuwa ni katika baa iliyopo mtaa wa tatu, tokea pale tulipoonana.
Soga za wakati huo, zilichukua nafasi kubwa baina yetu.
Tulicheka na kunywa pamoja.
Lakini, kooni mwangu nilikabwa na kifundo cha uchungu.
Hali ilivyozidi kunishika, niliamua nikifungue tu...

"Daah! jamaa yangu Mkojera, hivi umetobolea wapi yani?" niliuliza.

"Kivipi Zakayo?"

"Nazungumzia maisha, naona unang'aa sana siku hizi! Au umepata lishangazi linakulea?" nilijaribu kumchombeza kwa swali la kipuuzi.

"Hahahhhah, hamna bwana rafiki yangu. Kumbe hujaacha tu mambo yako!"

"Aaa'nh, tuambiane bwana ndugu yangu. Unaona wenzako tunavyopigika?"

"Hamna. Haya mambo mazito! Lazima uwe mwanaume ili upate vitu hivi ndugu yangu?"

"Dooh, sasa hayo matusi ya nguoni. Ina maana sie tusiokuwa navyo, ni wanawake au?"

"Simaanishi hivyo Zakayo, yapasa kujikaza sana ili uvipate!"

"Mradi hufi, mimi niko tayari Mkojera. kwa lolote!"

"Unamaanisha unachozungumza?", Mkojera aliongea kwa kunikazia macho, kuonesha kutaka uhakika kutoka kwangu.

"Ndiyo ndugu, hakuna anayetaka umasikini bwana!"nilijibu.

"Basi sawa,"aliafiki, akashusha pumzi na kuendelea,"Kesho tukutane saa kumi na mbili asubuhi. Palepale nilipokukuta leo. Kuna sehemu nitakupeleka!"

Nilimshukuru sana Mkojera. Sana!
Si tu kwa kuahidi kunisaidia. Bali pia, kuonesha dalili ya ukunjufu wa mtima wake, kwa kuniachia Shilingi elfu kumi mfukoni.
Niliipeka pesa ile, kama ilivyo nyumbani. Nikamkabidhi mama yangu.
Nampenda sana aisee!

Saa 10:15,
Ndivyo kulivyosomeka. Baada ya mboni zangu kugota ukutani, kulipo na mishale miwili: mrefu na mfupi, yenye kuzizunguka namba kwa zamu.
Tayari kulishakaribia kukucha.
Shauku ya safari na woga wa kuchelewa kuamka, ukanifanya nisilale mpaka ilipoingia alfajiri.

Nilijiandaa harakaharaka.
Sikutaka kumsumbua mama yangu, nilitoka nikiwa nimemuacha bado yu-ndotoni.

Njiani, kila hatua niliyopiga, ilijenga taswira mpya ya maisha yangu.
Nilianza kujiona nami ni mmojawapo ya wapanga foleni, huku wameshika sukani za magari yao, wakisubiri muwako wa taa ya kijani.
Mara, nikavuta picha nyingine. Kuwa nasugua kadi kwenye mashine ya benki, pesa zikichomoka kama uchafu.
Kila kitu, nilihisi kinaenda kubadilika chini ya pambazuko la siku hii.

Nilipuuzia kabisa waswahili, na kudai kwao kuwa,'Mafanikio hayana njia ya mkato.'
Sikutaka hata kidogo, kulifikiria hili!

......
Tukutane kesho.
 
Sehemu ya pili.

WAKATI tukiwa katikati ya safari, ndani ya gari la Mkojera, yeye akiwa anazungusha usukani na kubadili gia atakavyo,kuna maswali mengi yalikuwa yanazonga kichwa changu.

Pamoja na kuwepo mazungumzo mengine, bado hayakunitosheleza. Nilihitaji kujua!

"Daaah! Ina maana huko tunakoelekea, huyo jamaa ana hela sana eenh?" nilimuuliza.

Akanigeukia, kwa mshangao.
Mshangao uliotunga swali jingine tena kichwani mwangu.
Ila, nilisema hapana. Acha nijibiwe hili kwanza.

"Khaa! Kwanini uulize hivyo Zakayo?"
Badala ya kunijibu, naye alinisaili.

"Si umeniambia kuna sehemu tunakwenda, ambapo wewe ndipo ulipata pesa?" niliuliza, nikameza funda dogo la mate na kuendelea, " nd'o nakuuliza, huyo jamaa ni tajiri sana nini?"

"Kwani wewe unahisi kuna mtu anaenda kutupa pesa Zakayo?". aliongea bila ya kunitazama.

Kwanini ananijibu hivi?
Wasiwasi ukaanza kuniingia.
Hii mikasa ya watu kuchinjwa kwa kutolewa kafara, hata na ndugu zao wa damu-nimeisikia sana tu.
Sembuse huyu rafiki?
Lakini, si nilitaka mwenyewe?
Nikajituliza.

"Ndiyo," nilijibu kiupole. Tayari vitendawili vilivyokosa wategeuaji, vilitafuta ukumbi akilini, vikakaa!

"Hahaha hahaha haha!"
Aliicheka sana, mpaka akawa anapigapiga usukani...mie nilibaki namtazama tu.
Sikuelewa kipi kimchekeshacho!
Mwishowe alinyamaza. Akamalizia kutikisa kichwa kwa kusikitika.

" Khhh! sasa unanicheka au?" nilimuuliza. Ghadhabu zilianza tayari kunikumbatia.
Ni kweli, mimi ni masikini.
Ila, pesa zake zisimfanye anidharau.
Jamani! Lakini si anataka kunisaidia?
Kwani nimesahau kuwa, Ukiyakalia mtupu hapana budi kuyaoga?
Nikajituliza kwa mara nyingine.

"Hebu acha ushamba Zakayo, ndiyo maana jana nilikuuliza, hivi bado hujaacha mambo yako? Wewe unadhani ni mtu gani atakupa pesa bila ya kumfanyia chochote, akupe tu pesa?"

Tobaa! Nilianza kuona utabiri wa mama unaelekea kutimia. Kuolewa!
Kauli yake ilinifanya niishiwe pozi kabisa. Hasa hapa aliposema,"...ni mtu gani atakupa pesa bila ya kumfanyia chochote..."
Kwahiyo, huko tuelekeapo kuna kufanyiana chochote?
Hapana. Sitaki! Sitaki! Sitaki kabisa!

"Niambie bwana! Hebu kuwa muwazi Mkojera!" kujituliza kulifika kikomo. Nikaanza kufoka.

Bila ya kujishangaa!
Nafokea nini hasa? Kwanini sikuuliza kabla sijapanda garini?
Ni uzembe wangu tu. Sitakiwi kumlaumu.

Nilijishtukia. nikajishusha na kuuliza tena, kistaarabu, "au umenitafutia kibarua?"

"Hakuna cha kibarua wala nini!" Mkojera alifunguka,"unaikumbuka ile methali isemayo, mwenye shinda..."
Akaacha niimalizie.

Sikuimalizia methali yake!
Nilishamuelewa.
Nilishatambua wapi anataka kunipeleka. Sipataki huko! Sitamani kufa nikimkufuru Muumba wangu. Siwezi!

"Hapana Mkojera," nilimjibu.

"Hapana nini sasa?" aliniuliza kwa mshangao.

"Kwa mganga?" niliuliza, nikiwa nimeikunja sura yangu. Kumdhihirishia hisia nilizonazo:hasira!

Jamaa akapaki gari pembeni.

Haraka nikawa nafanya juhudi, nifungue mlango, nitoke garini mwake. Sikuweza!
Bado alikuwa hajaondoa loki.

"Unataka kuniteka sasa au?" niliongea kwa kumgeukia, macho yangu yakiwa yamejaa wekundu. Nilikuwa tayari kwa lolote. Kasoro kufa!

"Hebu tulia rafiki yangu!" aliongea huku akinishika bega la kulia,"Unaogopa nini sasa?"

"Sio kuogopa tu! Sitaki hata kupasikia!"

"Wewe unahisi huko kuna nini Zakayo? Huoni maisha yangu yanavyovutia. Hutaki kuwa kama mimi?"

"Ndiyo. Ndiyo Mkojera. Acha nife maskini tu, kuliko kwenda kutoa makafara huko!"

"Nani amekwambia kuhusu kafara kwani?" Mkojera alianza kunighilibu, ili niamini katika lile analotamani nilitekeleze. "Sikia nikwambie Zakayo..."

Pamoja na kuonesha msimamo, bado moyo wangu ulitamani mafanikio. Yawe ya halali, hata haramu.
Maisha ya pangu-pakavu, yalishanichosha!
Nilikaa kimya kumsikiliza.

"...Kule hakuna mambo hayo uwazayo. Sijui kafara sijui nini huko! Nakuahidi, ukiambiwa utoe kafara-tunaondoka. Hatutakubali!"

Siku zote, hakuna usawa kati ya wema na uovu katika mizani. Ni aidha ubaki mwema au ukatae, uwe muovu.
Mimi nilichagua uovu.
Nikajikuta nakubali, kwenda kwa mganga.
Gari likawashwa tena, safari ikaendelea!

***
HATUKUCHUA muda, tukawa tayari tumefika.
Tulifika mahali ambapo, ilitupasa tutumie miguu yetu, na si gari.
Wakati huo, jua lilishaanza kuchomoza. Asubuhi ya mishughuliko ilifika.

Tofauti na eneo hili.
Papo kimya mno. Labda ni kutokana na kujitenga kidogo na makazi ya watu.

Baada ya mwendo wa hatua kadhaa...
Mifereji ya pua zetu ilianza kulakiwa na harufu ya dawa za kienyeji. Zinakereketa!

Hakika, pazia lenye rangi nyekundu na nyeusi, liliniashiria kabisa-hapa ndiko kwa mganga!

Niliridhia kuja mwenyewe, wala sikubebwa.
Walakini, woga haukuacha kuusukuma moyo wangu, ukaufanya udunde almanusura kifua ukipasue. Kunatisha!

Tuliingia ndani, tukazungumza shida zetu, kuwa NAHITAJI UTAJIRI, UMASIKINI UMENICHOSHA.
Tukafanyiwa tiba, tukatoka.

Hapo nikaanza kumswadikisha Mkojera.
Niliona kabisa uzuri wa ihsani yake ulipo. Nikafuta ujinga wa walimwengu...eti masharti ya mganga ni mazito.
Kwa uzito upi labda?

Maana mimi, nilipewa kazi ndogo tu.
Nilikabidhiwa kuku mweusi, tena mganga mwenyewe, ndiye aliyemtoa. Hatukumnunua. Bure kabisa!
Nikaambiwa niende nyumbani, ikifika saa sita usiku, saa sita kamili!
Nimchinje.
Vivyo hivyo nitakuwa nayachinja matatizo yangu.
Hilo tu yani!

Nilimshukuru sana Mkojera, nilimuona ndiye rafiki wa haki, rafiki wa kweli, mwenye utu na kujali.
Kisha, alinirejesha nyumbani.
Kama jana alivyofanya, akaniachia pesa. Hapana, ni zaidi ya jana, leo ilikuwa elfu ishirini.
Maisha si ndiyo hayo bwana!

Nikaona nifanye kitu.
Kwakuwa ndiyo kwanza ilikuwa adhuhuri, nimfunge yule kuku kwa kamba pale nyumbani, nikapate chakula kwanza hotelini. Mama hakuwepo, nahisi alitoka.
Kisha nitarejea, ili baadaye usiku...niifanye shughuli.

Sikutambua kuwa, hiyo shughuli itakuwa shughuli kwelikweli. Sikudhania hilo!
Nikatoka...

Huko mgahawani, nilikula, chakula kikakwisha.
Ila, maongezi na mabishano ya kimpira huwa hayakwishi.
Yakanipumbaza, nikasahau kuwa kuna kuku nimemfunga nyumbani.

"Yule Ronaldo wenu, kwa Messi kuku tu!" Jamaa mmoja, katika ubishani ule alipayuka.

Kuku!
Nami ndiyo nikakumbuka. Haraka, nilikurupuka kama mkichaa...niwahi nyumbani.

Fuu-funua, fuu-funika!
Nilifika nyumbani.

Sikuamini kile kilicho mbele yangu.
Kamba imekatika, kuku hayupo!
Kaibiwa? Katoroka mwenyewe? Au mama kamchinja, kwa kujua nimeleta kitoweo?
Nilikosa jawabu.

....
Tukutane kesho.
 
Sehemu ya tatu.
0688589070.

Niliingia ndani, mama yuko wapi?
Hayupo. Alikuwa bado hajarudi.

Kichwa kilianza kuniuma. Mwili mzima ulianza kushika ubaridi, miguu yote ikikamata ganzi...namtafutia wapi huyu kuku jamani?
Nikatoka nje.

Sikutaka kutulia kabisa. Nawezaje sasa?
Ina maana ndiyo vile kusema, Mbuzi wa masikini hudumu tasa, hazai?
Hapana. Sikutaka kuimeza kasumba hii. Huyu kuku atakuwa yupo hapahapa mtaani tu. Kama hakutoroka, kuna aliyemwiba.
Lakini, tangu lini kukawa na wezi wa kuku mtaani mwetu? Hakuna tabia hiyo.
Sasa itakuwa kaenda wapi?
Niliendelea kutafakari.

Hatimaye, niliwazua la kufanya.
Nipite nyumba mojamoja, niulizie. Sitoweza kumkosa.
Nikaianza kazi hiyo...

"Kwahiyo, mimi nikae hapa kwangu, niangalie kuku na rangi zao wakipita, eenh?"
Hilo ndilo shushuo nililopokea nyumba ya kwanza tu, baada ya kuuliza, "Samahani anti. Umeona kuku mweusi akipita huku kwako?"
Sijui kosa lilikuwa wapi hapa!
Au ndiyo nongwa tu za waswahili?
Nilimpotezea, nikaendeleza msako.

Nilizunguka mpaka ilipotimu mishale ya saa moja jioni, chakula chote nilichokuwa nimekula mchana kiliyeyuka tumboni.
Hakuna nilikofanikiwa!
Nikarudi nyumbani, hoi bin taaban.
Sitambui la kufanya!

"Mbona mwenzetu umechoka hivyo?"
aliniuliza mama. Hata sikusikia swali lake hili, nilimpachika langu...

"Umemuona kuku mama?"

"Kuku-gani?"

Jibu lake lilinitosheleza.
Angemuona asingeuliza hivi.

Kwa kuwa sitaki maswali yawe mengi. Na akayafahamu yaliyojiri mchana wa leo, nilimdanganya, "Kuna kuku nilimkuta mchana anatangatanga maeneo haya. Ah! Itakuwa karudi kwao."

"Usije ukataka kuiba kuku wa watu wewe!" Mama alinishuku uhalifu.

"Hahaha," nilijichekesha, kuficha sintofahamu inayonisibu kichwani.

"Zakayo, uko sawa kweli?" Mama aliniuliza kwa mara nyingine.
Amaa kweli, mama ni mama. Nlijitahidi kuzificha hisia, ila haikumzuia kunishtukia.

Kimya!

Si kwamba sikumsikia. Bali nilikuwa njia panda, nimueleze nisimueleze?
Yote yalikubali na yote yalikataa!

"Enh! Naona umekuwa bubu leo." Mama aliongea huku akisimama na kuingia ndani. " Ngoja nisonge ugali, inaelekea saa mbili hii!"

Inaelekea saa mbili?
Mpaka saa sita? Masaa manne tu!
Hapana, sitaki kufeli, siwezi kujifananisha na samaki aliyekufa kwa kiu baharini. Ni ubwege!
Lazima nifanye kitu.
Niliinuka na kuondoka pale nyumbani. Sikumuaga mama yangu.

Mkojera!
Jina lilinijia kichwani.
Ndiyo, huu ni msaada wangu wa pekee, uliokuwa umesalia kwa wakati ule. Nikafanya utaratibu wa kumpigia simu.

Kama nilivyotegemea, alinilaumu sana.
Lakini, alikubali kunisaidia.
Huyu ndiyo rafiki wa kweli!

Aliniambia nifike Mwenge, kisha nimsh'tue anifuate kutokea pale, yeye anaishi Makumbusho. Ndiko alikojenga huko.

Atanipitia tuelekee Bunju, kule kwa mganga wa asubuhi. Alisema hakuna namna nyingine.
Bila kupenda wala kutarajia, narejea tena kwa mganga.
Dah!

Nilifanya kama alivyoniagiza, huku najuta.
Tayari yale yasemwayo na walimwengu, yalianza kunizodoa kwa majivuno: Si tulikwambia?

Tulifika kule kwa mganga.
Mwanzo, ilikuwa asubuhi, nikatetemeka nusu ya kudondoka.
Mara hii ni usiku, ushafahamu kilichotokea.
Kulikuwa kunatisha!

Kila hatua niliyoweka chini, nilihisi kuna mtu anatufwata.
Nilivyonyanyua nyingine, niliona kama ameshatufikia.
Kasi ya moyo wangu, ingelinganishwa na chui anayekimbiza kiwindo kwa wakati ule, bado ingemshinda.
Niliogopa sana.

Na hatimaye, tulifika kwa mganga.
Ilikuwa takribani ni saa tano usiku hivi.
Huwezi kuamini, yule mganga alikuwa bado yu-macho.
Anashughulika na mizimu.

Nasi tuliomba ruhusa, tukaingia.

Hayo niliyoelezwa huko ndani na mganga, yalinifanya nijute.
Si kujuta tu kuja kwake, hata kufahamiana na Mkojera.

Mganga aliniambia, "Kijana! Kijana! Umeharibu matakwa ya wakulu. Unchotakiwa kufanya sasa, Ukafukue makaburi 99... Narudia tena, makaburi 99, ukafukue makaburi 99, ufanye nayo ngono hadi ufike kileleni... Laa si hivyo, mama yako atapotea, KAMA ULIVYOMPOTEZA KUKU WETU."

"Hapana. Hapana, naombeni mnisamehe! Sijafanya kusudi." nilijaribu kujitetea, huku machozi yakianza kunijaa katika mashimo ya macho yangu.
Haikusaidia chochote!

Hii ilikuwa ni adhabu kwangu.
Kwani nimetenda kosa gani? Sikung'amua.

Leo mimi nikafanye uchafu na maiti? Mimi?
Si maiti tu, yani nikafukue waliozikwa!
Tena nifike hadi kileleni. Hapana!

Kwa hiyo, ndiyo nimuache mama yangu kipenzi apotee, pia hapana!

Nifanye nini sasa?

....
Tukutane kesho
 
Sehemu ya nne.
0688589070

Baada ya muafaka kutopatikana mule ndani mwa Mganga.
Tulirudi hadi tulipopaki gari, mimi na Mkojera.
Hakuna aliyetia neno tangu huko.
Nilikuwa sijielewi kabisa!
Kila nilichokiona mbele yangu nilikichukia.
Kwa mara ya kwanza, nilitamani kutokee kitu cho chote kiniue. Ndiyo, ilikuwa bora nife tu. Dunia nilishaikinai.

Kwenye gari hakukuingilika. Bado nilisimama nje kutafakari. Hadi pale liliponijia la kuamua.
Si kuamua tu, la kutenda kabisa!

"Mimi siendi kokote. Nirudishe nyumbami"
Niliongea kwa ujasiri. Sikutaka kuyumbisha maneno.

"Kuwa uko tayari kumpoteza mama?"
Mkojera aliniuliza.

Nilimkata jicho kali. Michirizi ya jasho ikiwa imeweka bwawa wajihini mwangu. Nilitota!
Nilitota kwa hofu na uchovu.
Nimesahau, na kwa ghadhabu pia!

Sura ya Mkojera ilinichefua kila nilipoitazama.
Kwanini kanifanyia hivi?
Halafu ananiuliza, niko tayari kumpoteza mama yangu... Kwa hiyo nia ni kumpoteza?
Nakemea pepo la mauti, lishindwe!

Khee, nakemea! Kwa jina la nani sasa?
Wakati Mungu nilishamsaliti, nikaamini yasiyompendeza yeye. Acha niteseke!

Nilijighafilisha kabisa ile ahadi ya "niko tayari kwa lolote", niliyomtamkia kwa ulimi wangu, siku ile mara ya kwanza kukutana. Nikaanza kumteremshia lawama, " Yote umenisababishia wewe, Mkojera!"

"Mimi tena?" aliuliza kwa butwaa.

"Ndiyo! Unazuga hufahamu au? Si nilikwambia kuwa SITAKI MAMBO YA WAGANGA? Ona sasa, nateseka kwa ajili yako," niliongea kwa hisia kali mno, hisia zilizojaa harufu ya majuto." Naomba uniache Mkojera. Baki na kila kilicho chako. Nampenda mama yangu, nampenda..."
Machozi yalianza kunitoka. Na kilio kikafuata.

Ila, sikumaliza kuongea, huku kwikwi ya uchungu ikiwa imenikamata, niliinua uso wangu tena, nikamtazama Mkojera na kumwambia,"Kuanzi...kuanzia le...leo usinijue Mkojera."

Nilipomaliza kuzungumza hayo nikageuka, nionde mahali pale. Nilitaka kurudi nyumbani mwenyewe. Hasira zilizidi tafakari yangu.
Mfukoni sikuwa na hata thumni.
Eti, nitembee kwa mguu kutoka Bunju mpaka Mwembechai!
Akili ilikuwa inakataa, moyo ambao ndiyo umejeruhiwa, uliliamini suala hili kwa asilimia mia, kama si zote.

"Sawa mimi sitokujua tena Zakayo, ila naomba tu nikurudishe kwenu basi. Huku tulipo ni mbali, na ni usiku sana. Kwa kulinda tu usalama wako. Tafadhali!"

Maneno aliyozungumza yaliniingia akilini kidogo. Nilirudi hadi garini mwake. Sura niliikunja kisawasawa. Nilitaka afahamu kuwa nimekasirika. Nikafula na kuzila zaidi!

Safari hii ya masaa mawili kasoro, ilikuwa ni ya kibubu! Hakuna aliyemuongelesha mwenzake ndani ya gari, mpaka tulipofika.

Nilishuka. Hakukuwa na kuagana siku hii, urafiki nilitaka uvunjike rasmi na moja kwa moja.
Walakini, nilisahau kuwa, urafiki ni hazina is'okwisha thamani yake. Daima!

Huko ndani, nikakutana na fadhaiko lingine...

"Mama! Mama! Mama...una nini?"
Nilimkuta mama yu-dhoo'fu l' hali. Yuko chini anatapatapa kama samaki, hajiwezi!

"Zakayo! Ngoja nikwambie, uwepo wako hapa ndani, utazidi kumpa hali mbaya mama yako. Twende ukatekeleze uliyoambiwa...utampoteza kweli."
Ghafla, nilimsikia Mkojera anazungumza nyuma yangu.

Ameingia muda gani?
Kwanini alinifuatilia?
Ina maana alijua nitakachokikuta?
Maswali hayo yote, sikuwa na muda ya kumuuliza.

Haraka niliinuka, mkuku-mkuku na Mkojera tulitoka.
Mashepeo yako wapi? Tuliyabeba.
Safari ya makaburini ikaanza.
Kwa maisha ya mama yangu. Hata kufa niko tayari!
Sembuse kufanya uchafu na wafu tu?

"Kwa hiyo, mama huku nyuma hali yake...si itazidi kuwa mbaya?"

"Ndiyo. Kadiri idadi ya makaburi utakayochimba ikiongezeka... Nafuu pia, ndiyo itashtadi kwake."

'Mkojera anajuaje mambo yote haya?'
Nilitamani kumuuliza, ila nikasita.
'Atanichukuliaje? Ataniona nina kisiriani, mchoyo wa shukurani.
Mambo yote haya anayonifanyia?
Muda huu usiku, inaelekea saa tisa, inabidi awe kapumzika kwake ila bado yuko na mimi... Wakati jambo limetokea kwa uzembe wangu tu.
Namimi naye, nisingempoteza kuku, yangetokea yote haya?

Ah, ila kuku nilimpoteza au alipotea mwenyewe?'
Nilizidi kuwaza.

***

IL'HALI giza lilikuwa katika utawala wake, niliweza kutambua pale tulipokuwepo. Ni makaburi ya Sinza. Sinza makuburini.
Naam, tulishafika eneo husika sasa!

Kelele za wadudu, mijongeo ya mimea, na mrindimo wa utotoro...vilifanya ngozi yangu isimamishe vinyweleo vyake vyote.
Hapa ndipo moyo ulijawa shauku ya kunipasua kifua changu. Ulidunda hasa!

Ila, kwa mapenzi yangu kwa mama, sikujali. Nikajitosa ndani.

Humo, tukapanga mkakati. Mkakati wa kifirauni, kama si umal'uuni.
Kuwa, tutafute makaburi ya siku za karibuni...ndanimwe yawe yamezikwa wanawake. Hao ndiyo 'nitashughulika' nao.

Kazi ya msako ikaanza. Tochi ya sikanu ya Mkojera ikageuka msaada mkubwa wakati huu. Tulimulika kusoma majina kwenye kila kaburi tulipitalo.

Hatujakaa sawa, wote tulishtushwa!
Nini hiko?
Ah, kumbu ni simu ya Mkojera ilikuwa inaita. Akaipokea.

Baada ya maongezi kuisha alikata.
Kisha akanigeukia...

"Sasa Mkojera, naomba nikuache."

"Uniache! Acha masihara."
Nilihisi ananifanyia utani.

"Hapana. Shemeji yako ni mjamzito... Hapa alipo amezidiwa. Hakuna mtu jirani, naomba nimuwahi."
Wakati Mkojera anaongea haya, hisia za macho yake, yalinipa tafsiri ya akiongeacho. Alikuwa hadanganyi!

Nilimuamini. Lakini si kwa kuniacha peke yangu bwana.
Yani aniache peke yangu?
Makaburini?
Tena usiku mkubwa hivi?
Niligoma.

"Basi twende wote Mkojera," nilimuomba.

"Si kwamba sitaki twende. Ila kazi tuliyonayo ni kubwa Zakayo. Kumbuka ni makaburi 99! Mama naye hali inazidi kuwa mbaya kule. Endelea na kazi kaka!"
Kitendo chake cha kumtaja mama, kilinipa ujasiri upya.
Mateso tul'omwacha nayo nyumbani, hayakunipa amani kabisa.
Ndiyo niendekeze woga, wakati mama anateseka?
Nikakubali kubaki mwenyewe.

"Dawa hii utapaka..."
Mkojera aliniachia dawa ya kupaka. Nilihisi ni dawa ya kuzuia mbu, nikaiweka ngozini - kama mafuta... Jamaa yeye ak'enda zake.

Nikasalia mwenyewe.
Hapo ndipo kasheshe ilipoanzia!

....
Tukutane kesho. Katika sehemu ya tano.
 
Sehemu ya tano.
0688589070

MWANZONI upepo ulikuwa unatembea kwa kawaida, miti nayo vivyo hivyo. Lakini, kadiri muda ulivyopiga hatua, hali ilianza kubadilika.

Wakati huo, bado niliendelea kutafuta kaburi la kuanza kufukua. Kila nililoliona, huruma ilinishisha, akili ikan'ambia acha!

Awali, sikuhofia kabisa mvumo ule wa upepo, kwa kukisia ni mabadiliko ya dakika chache tu.

Mara, miti nayo ikaanza kupelekwa huku na kule. Kwa nguvu!
Nikaacha nilichokuwa nakifanya-kutafuta kaburi.
"Nini tena hiki?" nilijiuliza mwenyewe.

Kabla sijapata jibu, nikaanza kuisikia michakato ya nyayo ikiwa inakuja upande niliokuwepo. Nikalishikilia vizuri shepeo, lolote lijalo nilikabili.

Bado sauti ya nyayo zile, ilizidi kuongezeka. Kuashiria uelekeo wake ni huku nilikowepo mimi.

"Mkojera," niliita.

Kimyaa!

Sikuitikiwa. Na hapohapo, upepo ulikata mvumo, kukawa tulii. Kama ilivyokuwa awali.
Nikashusha pumzi.
Huku bado nikiwa natafakari, "ni nani aliyekuwa anatembea?" bado niliwaza," Kwa hiyo ule upepo nao ...au ni jini? Hapana."
Nilijiziua kufikiria vitu vya kutisha.

Niliendelea na kutafuta, tamatiye nilifanikiwa kupata kaburi. Na hii, ni baada ya kuona muda unazidi kuyoyoma. Kusije kukawa Kukakucha bado hakuna lililofanywa.

MAGRETH GIDION, Ndiyo jina lililoandikwa msalabani kwa mfu huyu. Alikuwa ana siku tatu tu tangu azikwe.
Msichana wa watu alikufa na ujana wake masikini, miaka 24.
Haya yote yaliandikwa juu ya kaburi lile. Kaburi ambalo, halikuwa limejengewa, ubichiubichi nilikuwa nauhisi kabisa, pale nilivyokanyaga udongo wake kwa juu, kunithibitishia kuwa-ni juzi tu alizikwa kiumbe huyu. Leo mimi, nataka kumfukua!

Nilifumba macho, nikameza mate, yaliyopita kwa ugumu sana kooni. Yakaenda kupokelewa na tumbo, tumbo lililokuwa limekosa cho chote ndani mwake tangu adhuhuri iliyopita.
Kisha, nilianza kulifukua kaburi lile. Kila nilipochimba na kutupa michanga kwa pembeni... Ndipo matone ya machozi, yalikuwa yadondoka mikononi mwangu. Inauma!

Punde, zile hatua zilirudi tena!
Zilirudi kwa kasi sana, nilipojaribu kugeuka, nilishangaa kupigwa kikumbo kikubwa mno! Kuleee! Nilidondoka. Haraka nikainuka tena.
Nani aliyenipiga? Simuoni.
Katokea wapi? Sijui.
Kaelekea wapi? Sielewi.
Nilianza kuvurugwa sasa.

Hapohapo, nilianza kuhisi kizunguzungu, woga ulizidi, damu yangu ilisambaa mwilini kama shoti ya umeme.
Nikimbilie wapi? Sikutambua. Hata ningepajua, nisingeweza.
Mwili wangu uliishiwa nguvu. Nilianza kulegea, nikanyong'onyea, fahamu zikanipotea!

***

NILIKUJA kuzinduka, tayari kumeshakucha. Nikatazama pembeni... Nilimuona Mkojera. Kumbe alisharejea tayari.

Alikuwa amekaa chini, kachoka hoi! Mbele yake, nikaliona lile kaburi nililokuwa nalifukua, tayari alishalimalizia, peke yake!

"Kwanini anajitoa hivi?" nilijiuliza huku namtazama.
Alivyoona macho nimeyafumbua, aliinuka haraka na kunifuata.

Nami nilijivuta, huku nahisi maumivu makali ya kichwa...nikakaa kitako.

"Vipi, uko sawa? Nilikukuta umedondoka, nikahisi umeng'atwa na mdudu mkali," Mkojera alinizungumzisha, huku akinitazama kwa hali ya kujali.

"Kama ulijua nimeng'atwa kwanini hukunipeleka hospitali sasa?" nilijisemesha kimoyomoyo na kumtazama usoni mwake. Kisha, nilimjibu,"Hapana. Ni uchovu tu nahisi,"nilimficha kilichojiri.
Sikutaka ajue kabisa. Niliogopa kumtia woga mtu anayeonesha ujasiri mbele yangu. Yeye ndiye alikuwa msaada wangu kwa wakati ule.

Mkojera alisimama, akaenda mbele kidogo na kurejea amebeba begi. Hapo kabla sikuliona begi lile...

"Umetoka nalo nyumbani?" Nilimuuliza huku nikilitazama kwa umakini.

"Ndiyo," aliitika na kutoa vilivyokuwa ndanimwe.
Alitoa mihogo mibichi, mingi kidogo, ikafuata dawa, sikujua ya nini...mwishowe, alimalizia chakula.

"Kula, huenda ni njaa tu hiyo," Mkojera alinikabidhi poti lenye chakula, viazi vya kukaanga.

"Mkojera!" nilimuita.

Akanigeukia Kuashiria ameitikia. Niliingiwa tamaa ya kumuelezea kilichojiri jana ila niliona nipotezee tu, saa nyingine yalikuwa ni mauzauza.

Mie bwana, nachekesha sana!
Nasema mauzauza?
Mauzauza ya kupigwa kikumbo mpaka nidondoke?
Kuna kitu tu. Si bure.

"Vipi mkeo, anaendeleaje?" nilibadilisha fikra na kumuuliza swali hili.

"Kwema tu, kajifungua kidume," alinijibu huku nikiona tabasamu hafifu kinywani mwake. Alifurahia uzao wake!

Nilijikalifu, nikala chakula kile. Chote!
Nilijawa na njaa ya haja.

"Sasa tufanye kazi, tuanze na hili," Mkojera aliongea huku anaashiria lile kaburi alilokwisha kufukua.

"Tunafanya sasa hivi? Si tutaonwa hapa?" Nilihoji. Nilidhani tungesubiri mpaka giza litakapoingia tena.

" Usiwe na shaka Zakayo. Ile dawa jana si uliipaka?"

"Ndiyo," nilimjibu

"Basi hakuna kiumbe yeyote, atakayetuona!"

Hakuna kiumbe yeyote!
Yule wa jana usiku ni nini?
Yawezekana kaburi linalindwa na mizimu hili... Kama si hivyo, Mungu alituma jini au hata malaika, anizuie kufanya dhambi ile. Niliwaza.

"Labda nikwambie Mkojera, mimi naona sitoweza kufanya tena haya mambo."
Woga ulinituma, nikaongea maneno hayo.

"Kwa hiyo mama afe, sivyo?" aliniuliza.

"Ndiyo!" nilimjibu kwa uchungu.
 
Sehemu ya sita.
0688589070

NILICHUKUA uamuzi wa kusitisha zoezi lile. Sikutaka kuendelea kufanya kazi yenye utumwa kwa yangu nafsi.

Kuna nyakati, njia pekee ya kukuzuia usife kwa njaa ni kufa njaa tu. Maana yake, hakuna namna!

Hali hiyo ndiyo ilikuwa kwangu, sikuwa na m'badala. Pamoja na kutamani kuacha kufanya, bado niliogopa na kuhofia uhai wa mama yangu.
Hana kosa lolote maskini! Mimi ndiye nimemuingiza katika hatia angali mlengwa hajui kama yu-hatiani.

"Hivi unatambua ulitendalo lakini?" Mkojera alinisihi kuacha kutekeleza maamuzi hayo magumu niliyoyafikiria.

Kimyaa!
Sikujibu kitu. Nilimgeuka Mkojera kwa jazba. Sikuamini!
Macho yake yalikuwa yanatoa machozi. Alikuwa analia!

Iweje Mkojera, mtu ambaye si mama yake nafsi ikamate hisia za siha ya mama yangu mzazi, zaidi yangu?
Laana kubwa kiasi gani hii!
Mwili mzima ulinisisimka, haya na aibu vikanishika. Nilijiona mkosaji nisiyestahiki msamaha.

"Sasa tunafanya nini?" nilimuuliza Mkojera...huku nikijivika uso wangu muonekano wa kujuta na ujasiri kwa wakati mmoja.

Mkojera alilijongelea lile begi lake, akatoa mfuko, ndanimwe kulikuwa na maboksi ya kinga.
Ndiyo. Ingelihitaji moyo mgumu, wenye asili ya kiibilisi kufanya na mfu wa 'kavukavu'.

Hatukutaka kupoteza muda zaidi. Tuliinama na kuingia sote mule ndani ya kaburi. Tukalifungua jenezale!

Harufu na muonekano uliozaliwa baada ya kitendo kile, hakuna kati yetu aliyevumilia. Sote tuligeuza sura zetu pembeni!

Baada ya kuizoea, naweza sema hivyo...maana harufu hii haikuisha kabisa eneo lile.
Ndipo tukarejesha fikra zetu tena.

"Vaa kinga hii hapa,"
Alipatia pakiti moja ya kinga. Kwa roho nyeusi yenye kujawa ushetani, niliivaa.

Nilivua fulana yangu nikafunga puani, rihi ilikuwa bado inatoka kwa nguvu zote.

Moyo wangu ulikuwa kama umetiwa majini, nilihisi unayeyuka kwa woga na hofu iliyonijaa wakati ule.
Huku mikono yangu inatetemeka, macho yakiwa hayataki kutazama nikitendacho...akili ikogoma pia, nilisogezasogeza vazi alizozikwa nazo maiti ile ili nipapate 'panako'.

Sekunde chache, tayari alikuwa wazi. Hapo, harufu ilibadilika zaidi na ikawa mara mbili ya awali. Palitokota!

Inasemekana kuwa...
Mbuzi, ng'ombe na hata simba, wote hawa huitwa wanyama. Viumbe hivi, Mungu amejaalia kutokuwa na maarifa. Je, ni haki kumuita binadamu aliyetunukiwa akili, akafanya kusudi kutoitumia naye MNYAMA? Hapana, huyu ni zaidi ya mnyama.

Ndivyo nilivyokuwa mimi wakati huu. Nilipanda juu ya maiti ile nikaanza kufanya nayo ubaradhuli.
Nilikuwa nafahamu fika! Kuwa nadhulumu haki ya mtu yule... Ila nitafanye? Hakikuwepo cha kuniepusha.

Zilipita kama dakika tano hivi, bado ningali niko maitini. Jasho lilitirika na kumdondokea yeye. Nilivuta na kusukuma, hisia za kila aina nilizisogeza kichwani, hakuna kilicholeta mabadiliko. Nilihisi uchovu, uchovu uliojawa na kichefuchefu.

Mdomo ukazidisha uchachu, tumbo lilisusa, likaanza kurudisha kinywani vyote vilivyo ndani mwake, mwishowe nilitapika. Si kidogo, nilitapika sana!

"Jikaze Zakayo! Kaburi la kwanza tu hilo."
Mkojera alinisogelea na kunipigapiga mabegani kwa lengo la kunifariji na kunipa hamasa. Nijitahidi kufanya shughuli ile.

Kitendo hiki, kilizihamisha kumbukumbu zangu na kuzipeleka mbali. Sio hapo, mbali zaidi...

.....
SIKU HIYO jioni narejea toka michezoni. Nilikuwa niko darasa la tano. Sikutambua jingine, zaidi ya asubuhi shule, nikirudi kula, kucheza ; jioni kuja kukojoa nilale. Hiyo ndiyo ilikuwa ratiba yangu.

Shati likiwa limepishana vifungo, nimechafuka kwa kujitupa mavumbini,
nilifika nyumbani pakiwa pamebadilika mno, si kama kulivyokuwa siku zote, idadi ya watu waliongezeka. Pia, palitawala sauti ya vilio.
Kuna nini? Nilijiuliza bila ya kuelewa.

Nilifungua mlango na kuingia. Sura nilizokutana nazo hazikuwa ngeni kwangu, ni majirani zetu.
Wakina mama hawa, walimzunguka mwanamke mmoja aliyeinama huku analia kwa uchungu.
Sikujali sana.
Mama yangu yuko wapi? Sikumuona.
Kila nilipozidi kuwapitishia macho wanawake wale wengine, bado sikufanikiwa kumuona.

"Shikamooni," niliwaamkua.

Wote walinitazama. Hata yule mwanamke aliyeinamia pia aliinua uso wake, akanitazama. Sikuamini! Alikuwa ni mama yangu.
Kwa hali aliyokuwa nayo, macho yalimuiva, kamasi zilishindwa kujitofautisha na machozi wajihini mwake, aliishia tu kuniambia, "Zakayoo... Baba yako Zakayo, Zakayo mwanangu...ba..."
Kabla hajamaliza Mama Ashura, jirani yetu aliyekuwa pembeni yake, alimzuia.
"Basi Mama Zakayo. Huyo mtoto haambiwi..."

Haikuwa na haja ya kuambiwa, ili machozi nami yanitoke. Si machozi tu, na kilio chenye sauti kali ya juu!

Ndipo mama mwingine, kati ya wale waliokuwepo mule ndani, alisimama na kuja kunishikilia mabegani kunituliza.
Kama alivyokuwa anafanya siku hii Mkojera.

.....
Moyo uliingiwa nguvu mpya, nikaitazama maiti ile mule kaburini. Hali ikiwa mbaya zaidi. Tayari nilishaitapikia kwa juu.

Kichefuchefu kikaanza upya!

....
Mniwie radhi sana kwa lugha yenye ukakasi zaidi iliyotumika katika sehemu hii. Ahsanteni!
Tukutane kesho katika sehemu ya saba!
 
Sehemu ya saba.
0688589070

NILIJIKAZA, sikuruhusu nitapike tena. Nilikubali liwalo na liwe, nilipanda tena juu ya maiti ile. Safari hii nikiwa na ushupavu mkubwa. Ila, tatizo lilibaki moja tu, hisia.

Mkojera aliliona hilo. Nilishangaa simu ikiwa imewekwa usoni mwangu. Shida haikuwa ile simu, bali kilichokuwa ndani mwake. Ilikuwa ni video ya 'kikubwa'.

"Tumia hii kuvuta hisia!" aliniambia.

Nilimgeukia na kumtazama. Alijawa uchovu masikini rafiki yangu. Alitamani walau kazi ingekuwa ndiyo mwisho wake pale. Ilihali, ndiyo tunaianza.

Sikutaka kuleta ukaidi zaidi. Nilete ukaidi mbele ya msaada? Nitakuwa mtu gani tena!
Basi, niliitumia 'video' ile kisawasawa na dakika mbili tu, tayari wazungu walinitoka, kuashiria nimeshakwisha kuwasili kileleni.
Hapohapo, nilijitupa kando!
Pumzi zikinitoka na kuingia ndani kwa fujo...mithili ya aliyenusurika kuzama katika maji yenye kina kirefu.

Moyo wangu ulihisi wepesi wa muda. Na kujiona kama vile shujaa aliyetoka kupigana vita akabaki mwenyewe.
Je, ikizuka vita nyingine shujaa huyu atapigana tena mwenyewe?
Sidhani!

"Kwahiyo si tunalifukia hili?" nilimuuliza Mkojera huku najivuta kutoka ndani ya lile kaburi.

"Hapana," Mkojera alinijibu kirahisi.

"Hapana?" niliuliza kwa fadhaiko.

"Ndiyo, Ondoa shaka Zakayo!"

"Acha utani wako Mkojera bwana. Hebu tufufikie huko," niliongea huku nachukua shepeo nianze kurejesha mchanga.

"Nimekwambia acha!" Mkojera aliniwahi akanizuia kwa mkono wake wa kushoto. Ule wa kuumeni alishikilia dawa, akawa anaimimina mule kaburini.

"Unafanya nini tena?" nilimuuliza kuhitaji nifahamu akitendacho.

"Nd'o tunalifukia namna hii,"alinijibu huku anafunga kichupa cha dawa ile. Alishamaliza tayari.

Mkojera anayafahamu vipi mambo yote haya?
Tangu mwanzo, nilikuwa sielewi.
Ila, nilijikanya kuja kumuuliza. Akichukulia vibaya akaamua kuondoka je? Mama yangu si nd'o kifo kitamtembelea.
Nikajituliza.

Kazi iliendelea. Tulitafuta kaburi lingine na punde tukalipata.
Tulilifukua na kufikia jeneza. Ingawa hili lilikuwa ni la muda mrefu kidogo, tofauti na lile la mwanzo, uzoefu ulitubeba.
Kwa msaada wa simu na kinga, bila kusahau, nafsi ya kishetani - kazi haikuwa ngumu. Nikawa nimeshakanyaga vilele viwili.

Mwanzo mgumu, ndivyo waswahili wasemavyo. Nami, niliswadikisha kauli hiyo.
Makaburi yaliyofuata baada ya yale mawili ya mwazo, yalikuwa na urahisi mno kwangu. Sikupata shida hata!

Wafu waliozikwa ndiyo waligeuka wakawa wake zangu, nilioa, na baada ya tendo, nilitoa talaka. Sikumrejea hata mmoja baada ya kumtaliki, daima.

Mkojera alichukua nafasi kubwa sana katika kipindi hiki cha maisha yangu, maisha ya kaburini.
Yeye ndiye aliyekuwa ananiletea chakula, ili nipate nguvu. Aliniletea dawa za kimasai pia, ili nipate nguvu, ila za safari hii, ni tofauti na hizo za mwanzo.

Hofu ilibaki moja, mama mzima?
Nilipojaribu kumtuma jamaa akamtazame. Alinijibu anaendelea vizuri!
Nilimuamini.

Maisha yalisonga.

KABURI LA 34.

HAKUNA safari yenye unyoofu kutoka mwanzoni mpaka mwisho. Lazima utasabahiana na milima, bila kusahau mabonde, kabla haujaimaliza.
Kaburi la thelathini na nne, lilikuwa ni kimbembe!

Tayari nilishakuwa mkubuhu wa dhambi hii. Ilikuwa ni usiku. Mkojera alikwenda kununua chakula na kunibakiza mulemule makaburini.

Sikuwa muoga tena. Nilimalizia kaburi tulilokuwa tunafukua pamoja, mimi na jamaa. Mpaka nilipolifikia jeneza.

Tangu hapo, makaburi yote yaliyopita, jeneza nilikuwa nafungua nipo na Mkojera pembeni.
Siku hii, baada ya kuona anakawia kurejea, nilichukua jukumu la kuamalika mwenyewe. Sikutaka kumsubiri.

Nilichokikuta, kilifanya nihisi mwili wote unaenda kupooza!
Sikuendelea kufanya kitu, haraka yote ikanikata. Nilimsubiri Mkojera.

Siku zote tunakanywa kuwa, Tusihukumu yaliyomo kitabuni kwa jalada la nje. Hivi ukikihukumu kwa jina lake, utakuwa upo sahihi au?

Sisi, tulihukumu kilichopo ndani ya kaburi, kwa jina lililo juu yake.
Adhabu yake ndiyo hii...

"Vipi, mbona hauko sawa?" Baada ya Mkojera kurejea, aliniuliza kwa kuniona siko vema.

"Funua hilo...!" nilimuonesha jeneza.

Naye alishuka ndani ya kaburi. Giza lilimzuia kuona vizuri akawasha kurunzi. Kisha akafanya nilichomueleza - alifunua.

Kile alichokiona. Naye pia alishindwa kujizua. Akalifunga haraka!

....
Tukutane tena jumatatu. Katika sehemu ya nane.
 
Sehemu ya nane.
0688589070

KABURI lile alizikwa msichana mwenye ulemavu wa ngozi, Albino.
Mbaya zaidi, viungo vyake vilikuwa vimekatwa.
Sikutambua alikufa kwa kifo gani, lakini kilikuwa ni cha mateso.
Umauti ulimkuta kwa mateso, Nami nimfukue nimpe hayohayo? Hapana.

Sio mimi tu, hata Mkojera pia hakutaka nifanye chochote na maiti ile.

"Tuliambiwa makaburi tisini na tisa, tukiacha hili hatutakiuka masharti?" nilimuuliza Mkojera, akili yangu ikiwa imekwisha tapakaa ganzi ya kutoelewa la kutenda. Sauti niliyotoa ilijawa mtetemo wa huruma.

"Hapana," alinijibu. Bila ya kuongeza neno jingine.

"Kivipi sasa?" nilimuuliza.

"Kaburi linahesabika, pale tu, utakapofanya nalo tendo."

Hapo nikapata mwanga sasa. Nilishauri tufukue jingine, lile tuliache kwa kuogopa dhambi za bure.

Dhambi za bure..! Kwani hizo nyingine nanunua?
Nilipunguza dhambi tu. Ila kuzichuma niliendelea. Sikuacha!

Tukaanza kazi ya kutafuta kaburi jingine, lile hatukuliweka hesabuni, ila tulilifukia.

Ni rahisi sana kununua gazeti kwa KICHWA CHA HABARI. Ukikuta habari uliyotarajia ipo imewekwa sivyo ndivyo, Vipi utahisi? Utarudisha gazeti upewe jingine? Nalo likiwa nd'o yaleyale je?
Utafanya kazi ya kurudisha na kuchukua?
Usijali, utaelewa nini namaanisha...!

Baada ya masaa mawili kasoro, tulishalifikia jeneza la kaburi jingine. Lakini, Siku ya kufa nyani, miti yote hainati tena.
Ndivyo ilivyokuwa...
Kaburi hili nalo lilikuwa kisanga!

Ni mwanamke aliyekufa mjamzito. Nililitambua hili kwa jinsi tumbo lilivyokuwa limemvimba. Suala hili, liliibua mtafaruku mpya kati yetu...

"Watu wanakufa kwa namna tofauti Zakayo! Wapo wanaokufa macho wazi, midomo wazi, wewe mwenyewe pia umeshuhudia!
Wengine huvimba..."
Mkojera alidai ile si mimba, bali ni uvimbe wa umauti tu.

"Mkojera, tusifanyane watoto bwana. Huko tulikopita tulikutana na maiti ya aina hii?" nilimuuliza.

"Nd'o tumeikuta sasa!" alinijibu.

"Sawa. Tufukue kaburi jingine," nilipendeza.

"Basi leo tutakesha hapa," aliongea Mkojera huku anakaa chini. Alionesha uchovu, kama mtu aliyekata tamaa kwa yote.

Nilimtazama, nilimuonea huruma mno. Hata mie, ningalikuwa yeye nisingaliweza toa msaada wa kiasi chake. Alijitoa. Zaidi ya kujitoa, alinithamini sana Mkojera.

"Okay, nitafanya na huyu mwingine," nilikubali.

"Yupi?" aliniuliza kwa sauti yenye mshabaha na shauku.

Nilimwonesha lile la pili -aliyevimba tumbo. Lile la alibino, linahitaji ushetani wa ziadi mtimani ili kuweza kulikabili. Nami sina. Sio sina tu, siutaki kabisa!

Ndivyo ilivyokuwa. Tulitekeleza azma yetu na maiti ile mpaka lengo lilipofikiwa. Pale kalamu ya asili ilipokwisha kuutoa wino wake mweupe ndipo nilipojichomoa.
Ni dhambi ya aina gani hii nilikuwa naipata!

Hatimaye, siku hii nayo ilikwisha!

UKWELI WA YOTE..!

HAKUNA siri katika hili duara lenye pande kuu nne. Namaanisha dunia.

Hii ni siku ambayo nuru ya maisha mapya ilianza kuangaza. Baada ya kupoteza matumaini na kuishi bila amani kwa muda mrefu humu makaburini. Ukingo ulikuwa umewadia.

Lakini pia, waswahili husema mzigo huuma mwisho wa safari na haja hubana ukikaribia na choo.
Unalitambua hilo?

Lilibaki kaburi moja tu! Yafikie 99. Au yawe 100, ukihesabu na lile la albino tuliloliacha. Siku nyingi zilizopita.

Muda huo tuliamua kupumzika na kutafuna mihogo mibichi...

"Kisu kiko wapi?" Mkojera aliniuliza

"Mmnh! Sifahamu... Haujakiacha kule kweli?" nilimjibu kwa kumuonesha upande wa pili.

Aliinuka akakielekea. Mimi sikuwa na haja nacho. Meno yangu yalitosha kuitwa kisu kwa wakati huo.

Baada ya Mkojera kupotelea kichakani, alipokwenda kuchukua kisu, nilisikia sauti ya ukelele...

"Yalaaaaaaaa...!"

Niliinuka kwa kukurupuka,nikawahi.
Nilimkuta Mkojera chini, anagaagaa kwa maumivu.

"Kuna nini Mkojera, nini?" nilimuuliza.

Hakunijibu. Akawa anaelekeza mkono wake mguuni, kuashiria maumivu yapo pande zile.

Nilimtazama. Nikagundua aling'atwa na mdudu mwenye sumu kali, nyoka.

Nilimuinua chapuchapu, nikamuweka mkono begani mwangu...tulipofika mbele kidogo, nilimuweka chini.

Nilichana harakaharaka suruali yangu, nikamfunga kwa nguvu chini ya goti lake, kabla sijaendelea...

"Acha Zakayo. Usihangaike kitu!" alinikatza.

Sikumsikia. Hata kama ningemsikia, nisingekubali kuacha. Mkojera alikuwa kila kitu kwa kipindi kile. Iweje apotee machoni mwangu wakati nd'o tunaimalizia kazi. Hapana, nilikataa hilo.

Aliuvuta mguu wake kwa nguvu, mguu ule ulioumia.

"Unafanya nini?" nilimshangaa.

"Nimesema niache! Niache nife!"

"Unataka kufa?!" alizidi kunivuruga, nikamwambia, " unajua acha utani kaka. Nyoka huyu..."

"Sio nyoka!" Mkojera aliongea kwa hasira na uchungu. Aliugulia maumivu sana. Lakini hakutaka nimshike kabisa.

Hapohapo, mapovu yalianza kumtoka mdomoni.

....
Tukutane baadae jioni
 
Sehemu ya mwisho.
0688589070

"HAPANA...hapana..Mkojera, usiondoke ukaniacha...Mkojeraaa!"
Nilimlialia kwa uchungu sana.

"Beee...beegiii!" Hilo ndilo neno ambalo Mkojera alijitahidi, akajitahidi tena, mpaka akalitamka.
Akhiriye, roho iliacha mwili wake. Mwili wa rafiki mwenye upendo usio na tamthili.

Nilibaki mwenyewe pale makaburini.
Mkojera aliniachia kiwiliwili chake tu.
Sio kiwiliwili tu, na kitendawili juu.
Kwanini begi?

Niliinuka na kwenda kulifungua.

Baada ya kulifungua begi lile, nilikutana na karatasi iliyokunjwa vizuri mara nne. Niliifungua pia!

Hii ilikuwa ni barua, barua iliyoandikwa na Mkojera kwa mkono wake mwenyewe.
Pamoja na elimu yangu kuwa ndogo, darasa la saba.
Haikuwa sababu ya kushindwa mimi kusoma. Niliisoma!

Kiukweli, nilitamani angalikuwa hai, ningalimtandika vibao vingi sana vya hasira, kisha nimkumbatie kwa shukrani na upendo!
Ni barua iliyoniumiza.
Hapana, haikuniumiza tu, iliniliza kabisa.

Maumivu niliyopata wakati naisoma barua ile, naweza sema tangu niko katika uso wa sayari hii, sikuwahi kuyahisi.

Majuto yalioufinya moyo wangu kwa ghadhabu, yalinitupa chini na kulia kwa kupigapiga ardhi. Nililia kilio cha kusaga meno!

Barua ilisoma hivii...

"Habari yako Zakayo?
Pole sana kwa uchovu. Lakini pia nisamehe sana mimi. Usije ukajaribu kunishukuru. Mimi ni mshenzi wa kutupa!

Zakayo, mimi ndiye niliyekufanya mpaka leo upo katika hali hiyo.

Siku ile, siku tunakutana, ulivyoniuliza kuhusu utajiri wangu tu, niliona umenipa fursa kubwa sana!

Kile kilikuwa ni kipindi cha kutoa sadaka.
Usishangae!
Utajiri wangu ni wa mizimu rafiki yangu.

Na ulivyoniambia unaishi na mama pekee, nikamkusudia yeye. Ingawa mwanzoni, nilihitaji nikakutoe wewe.

Yule kuku, hakuwa kuku Zakayo. Bali ni zindiko letu tu. Zindiko toka kuzimu.
Na hakupotea, bali tumlimchukua sisi wenyewe!

Zakayo, Umasikini na utajiri zote ni hali za kifikra tu. Tafadhali ridhika na ulichonacho rafiki yangu...huku ukifanya jitihada kila siku ujikwamue!

Unampenda sana mama yako Zakayo, naonba usikome kufanya hivyo. Mungu atakubariki.
Nimeamua kufa badala yake.

Laiti usiku ule ningalikuacha uondoke urudi mwenyewe nyumbani, lengo langu lingalitimia...mama angekufa! Usingeweza kufanya kitu.

Nilitamani sana kukwambia kabla, lakini niliogopa. Utanichukuliaje..."
....

Kufikia eneo hili, nilizidisha kilio, karatasi ile iliyokuwa mikononi mwangu huku naisoma, ililowa kwa machozi! Nililia hasa!

Mimi niliogopa sana kuuliza, naye aliogopa kuniambia. Tuliogopana! Kwanini sana tuliogopana jamani, daah!

Niliendelea kusoma barua ile...

"Naomba nikuache uendelee na jukumu lako Zakayo.

Fahamu mimi ndiye niliyekusababishia hilo. Muokoe mama yako, ukimaliza tu, mama atarudi katika hali ya kawaida!

Kwaheri, Ngoja nikaendelee na adhabu zangu nilizozikuta huku rafiki yangu!"

Nilimaliza kuisoma barua ile niko hoi, mwili mzima ulinisisimka kwa uchungu, majonzi yakivuta hisia zangu na kuzipigiza majutoni. Narudia tena, nililia sana..!

Kwani barua kaiandika saa ngapi hii?
Alijuaje kama atakufa yeye?
Na mkewe ana kichanga, amemuachaje?
Au pia alinidanganya tu?
Maswali haya, majibu yake yaliondoka na uhai wa Mkojera.

Nilimalizia ile kazi kisha nilirejea nyumbani. Maiti ya Mkojera niliiacha kulekule makaburi. Sifahamu kama ilionekana au laa!
Haikuwa namna nyingine zaidi ya kumueleza mama yangu hali halisi. Nilimtaka radhi kwa yote!
Pia, nilimrejea Mungu wangu. Nikaomba msamaha na kutubu. Nina imani amenipokea.

Kwa sasa naishi katika wasia wa mkojera.
Napambana na hali yangu. Tayari nimejiajiri.
Nipo Ubungo, Kituo kikuu cha mabasi, nauza magazeti.
Kama yangu ipo, Mola atanihifadhia tu.
Nitaikuta!

MWISHO.

TANBIHI: Hadithi hii fupi ni ya kutunga tu. Majina na sehemu za kweli vimetumika ili kuweka uhalisia na funzo lipatikane!

Ulikuwa nami, Abyas Mzigua.
Mawasiliano: 0688589070
Tukutane tena katika kazi nyingine!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom