Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,443
Mkapa alipoingia madarakani alianzisha TACAIDS kwa madhumuni ya kupambana na janga la ukimwi Tanzania na alipoingia Kikwete alianzisha NACP kwa ajiri ya madhumuni hayo hayo na mbaya zaidi kwasasa baadhi ya watu waliopo TACAIDS wanahaha kwamba kifedha ni pagumu sana kufanyia kazi ukilinganisha na enzi za Mkapa, kwasababu mafungu mengi yanayohusiana na janga la ukimwi yanaelekezwa NACP. Wanaofahamu tofauti kati ya TACAIDS na NACP wanisaidie ili niondokane na fikra zangu kwamba NACP imeanzishwa na Kikwete kwasababu ya maslahi ya watu fulani, hasa ukifikiria kwamba Rais hawezi akaanzisha chombo kinachoshughulikia suala fulani ambalo tayali kuna chombo kinachoshughulikia suala hilohilo kilichoanzishwa na mtangulizi wake.
TACAIDS=TANZANIA COMMISSION FOR AIDS (MKAPA)
NACP=NATIONAL AIDS CONTROL PROGRAMME (KIKWETE)
TACAIDS=TANZANIA COMMISSION FOR AIDS (MKAPA)
NACP=NATIONAL AIDS CONTROL PROGRAMME (KIKWETE)