Mkapa: Najuta

Nakiri sijawahi kusoma comment ya uongo kama hii! Hivi huamini kuwa uongo ni dhambi na utahukumiwa juu ya uongo??
 
Alikuwa na lundo la washauri nguli wa masuala mbalimbali. Alikuwa na mawaziri, wabunge, RC's & DC's et al.
Kwanin aombe msamaha yeye? Ina maana hakufuata alichokuwa anashauriwa?
 
Sipendeleagi kusema haya but nimelazimika kuyasema walau kidogo; tokea nchi imepata Uhuru Magufuli ni rais 5 kukaa Ikulu na anafanya kua rais 3 Mkristo.

Hawa 4 (Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete) ni 2 tu ndio nimewahi kuwasikia kwa masikio yangu na kuwasoma wakiomba msamaha mahali walipokosea, tena wote wameomba msamaha zaidi ya mara 1 na wamefanya hivyo hadharani; ni Nyerere na Mkapa.

Sijui ni kwasababu ya malezi ya dini zao kwamba lazima mtu atubie makosa na maovu yao au ni unyenyekevu (ambao nao still umekaa kimalazi ya Kikristo zaidi).

Sina kumbukumbu kama nimwahi kumsikia Mwinyi na Kikwete kuomba msamaha (Mwenye kumbukumbu anikumbushe).

Swali ninalo jiuliza, hivi hawa wengine ni kwasababu ya malezi ya kidini au misimamo ya dini zao au imetokea tu kama coincidence? Mwenye uelewa tafadhari.
 
haya buana ngoja tumsubiri HB wa msoga kama na yeye ataomba radhi,maana ule mchakato wa katiba ulikula pesa nyingi sana.
 
Shetani akizeeka anakuwa malaika .... kumbuka kauli hii toka mmoja wa wale alokuwa nao kwenye uongozi
"Ndege ya rais lazima inunuliwe hata kama wananchi watakula nyasi"
 

Ni coincidence tu mkuu. Hakuna dini isiyofundisha kuomba msamaha au kufanya toba baada ya kukosea
 
Naumbuka aliiuza nbc kwa bei ya kukata tamaaa na sijui ni kitu gani kilimpata huyo achimwene
 
Umeelezea vema mkuu, lkn kwa mfumo wetu huu tulio nao wa watawala kwenda kwenda kwenye majukwaa na huku wamezungukwa mitutu huo ujasiri wa kuwahoji na kuwataka waeleze nini wametufanyia tunaweza kuupata wapi?
 
Nakumbuka alikuwa mbishi ka nini eti Leo ndo anaomba msamaha basi tutarajie na jk kuomba msamaha baada ya miaka kadhaa mbele.
Hakuna cha kuomba msamaha huyo ni muongo mbona hajaomba msamaha kwa watanzania alio waita malofa?hivi huo msamaha anawaomba hao hao malofa au kuna watanzania welevu wamezaliwa?
 
Mkuu binadamu wengi wanajisahu sana, hawa watawala wakiona wamezungukwa na walinzi na mitutu na magari ya delaya wanadhani hakuna hukumu ya mungu
 

Wewe umenena
 
MH. MKAPA: Wasomi WAACHE KULALAMIKA NA KUJIKITA KWENYE TAFITI ZAIDI.
Raisi mastaafu Mh. Benjamini William Mkapa amewataka wasomi kuacha tabia ya kulalamika na badala yake wajikite zaidi kwenye tafiti zikakazo saidia nchi. Pamoja na hayo mh. Mkapa pia ametolea ufafanuzi mada mbalimbali ikiwemo swala la ubinafsishaji na katiba.
 
Kuomba msamaha sio kitu kibaya bali ni njia mojawapo ya kujutia kosa ingawa wakati mwingine msamaha unaweza kuwa wa kinafiki tu.
 
Kuomba msamaha sio kitu kibaya bali ni njia mojawapo ya kujutia kosa ingawa wakati mwingine msamaha unaweza kuwa wa kinafiki tu.
Hata muomba msamaha inaweza kuwa mnafiki pia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…