Mkapa amwokoa Kikwete, azima hoja ya kumng'oa madarakani

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,013
na Salehe Mohamed
Tanzania Daima


RAIS mstaafu Benjamin Mkapa, alimnusuru Rais Jakaya Kikwete kwenye kitanzi cha kung'olewa kwenye wadhifa wa uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima Jumapili limedokezwa.

Kwa mujibu wa wajumbe waliohudhuria kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) kilichomalizika Novemba 24 mwaka huu mkoani Dodoma, walibainisha kuwa baadhi ya wajumbe walijipanga kutoa hoja ya kumtaka Rais Kikwete kuachia wadhifa wake.

Wanasema kuwa walipanga kufanya hivyo kwa madai kuwa katika kipindi cha utawala wa Rais Kikwete chama kimekuwa na migogoro mikubwa na kuifanya serikali iyumbe kila kukicha.

Walibainisha kuwa fursa ya kutoa hoja hiyo haikupatikana baada ya Mkapa kumtaka Rais Kikwete kusitisha hoja ya kuvuana magamba, baada ya kuona upepo mbaya ulikuwa ukimvumia kiongozi huyo.

Inadaiwa Kikwete alikubali ‘msaada' huo wa Mkapa ambapo alisema hoja hiyo imetosha kwa kuwa suala hilo lilirejeshwa kwenye kamati ya maadili, ambayo itapokea ushahidi wa tuhuma za makada hao pamoja na kuwapa fursa ya kuwasikiliza watuhumiwa.

Kwa mujibu wa wajumbe hao wa NEC, waligawanyika makundi mawili, moja likitaka Lowassa atoswe kwenye uongozi huku jingine likipinga kwa madai kuwa tuhuma za kada huyo hazijathibitishwa.

Lowassa alipopata nafasi ya kuchangia hoja hiyo, alieleza kusikitishwa na ufisadi wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambapo alisema kila alichokuwa akikifanya Rais Kikwete alikuwa anakijua kama si kumtuma.


Aliongeza kuwa pamoja na kujua huko kwa Rais Kikwete juu ya kashfa hiyo, bado alishindwa kuwakemea watu waliokuwa wakimhusisha Lowassa na ufisadi wa Richmond, ambao inadaiwa ulifanywa na watendaji wa serikali.

Rais Kikwete na wasaidizi wake mara kadhaa wamekuwa wakikana kiongozi huyo mkuu wa nchi kuijua na kuhusika na mkataba wa Richmond ambao ulifanya Bunge kuunda kamati teule kuchunguza mchakato ulioipa ushindi zabuni ya kampuni hiyo.

Katika kikao hicho cha NEC, Lowassa alibainisha kuwa kama tuhuma zingekuwa zinamng'oa mtu madarakani bila kufanyiwa kazi, basi Rais Kikwete asingekalia kiti cha uenyekiti wa CCM kwani mwaka 2003 alizushiwa tuhuma za ukosefu wa maadili na kada mwenzao, Paul Sozigwa.

Mbunge huyo alisema kama si busara za Mwenyekiti wa CCM wakati huo, Benjamin Mkapa, Rais Kikwete asingeukwaa urais, hivyo ni vema chama kifuate utaratibu waliojiwekea wa kushughulikia tuhuma zinazoelekezwa kwa makada wake.

Baada ya Lowassa kutoa utetezi wake huo, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, alisema halikuwa jambo la busara kuwatuhumu watu na kutangaza tuhuma dhidi yao kabla ya kuthibitishwa kwa tuhuma zenyewe.

Sumaye alionekana kukerwa na ukimya wa Rais Kikwete juu ya kuchafuliwa kwa Lowassa kulikokuwa kukifanywa na Katibu wa Itikadi na Unezi, Nape Nnauye pamoja na Naibu Katibu Mkuu (Bara), John Chiligati.

Sumaye alihoji iwapo kamati ya maadili itabaini kuwa Lowassa hakuwa na hatia, hatua gani zitachukuliwa dhidi ya Chiligati na Nape waliosambaza tuhuma hizo.

Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa kuwa hoja ya kumng'oa Kikwete ilikuwa ikiungwa mkono kichini chini na vigogo wengi ambao hapo awali walikuwa wakidaiwa kumuunga mkono Rais Kikwete.

Vigogo hao inadaiwa hivi sasa wamekuwa wakikerwa na jinsi Rais Kikwete anavyoyashughulikia matatizo ya chama hicho kwa kuendekeza siasa za makundi yanayohasimiana.

Baadhi ya wajumbe wa NEC, wamelidokeza Tanzania Daima kuwa kama Rais Kikwete hatajirekebisha kwa jinsi anavyoshughulikia matatizo ya chama tishio la kung'olewa kwenye unyekiti wa chama hicho litaendelea kumuandamana.

Waliongeza kuwa kwa hali ilivyokuwa ndani ya kikao hicho, Lowassa anaonekana kuwa bado ni tishio kwa vigogo wanaotajwa tajwa kuwania urais mwaka 2015.

Walibainisha kuwa licha ya kuwepo mikakati ya kutaka kiongozi huyo asipate fursa ya kujenga mtandao wa kumsaidia kuingia ikulu, Lowassa anaonekana kuwa imara zaidi kukabiliana na wapinzani wake.

Kabla ya NEC

Awali kulikuwa na tetesi kuwa Rais Kikwete alipokea pendekezo ya kuwang'oa madarakani baadhi ya viongozi wa chama hicho wanaodaiwa kuwa ndio chanzo cha mitafaruku ndani ya CCM.

Miongoni mwa waliokuwa wakisemwa kung'olewa madarakani ni Lowassa, Sitta, Nape, Chiligati na Chenge.

Inadaiwa kuwa baadhi ya makada wa chama hicho walikodishiwa usafiri kutoka kwenye maeneo yao na kulipwa posho ili kwenda kushangilia Lowassa, Chenge na wengineo wanavulia madaraka.

Kundi jingine nalo linadaiwa kupelekwa mkoani Dodoma kwa lengo la kushangilia kung'olewa kwa Sitta, Nape na Chiligati.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaweka wazi kuwa uamuzi wa CCM kulirejesha suala la kujivua gamba kwa kamati kuu ambayo italipeleka suala hilo kwenye kamati ya maadili kutafutiwa ufumbuzi kutazidisha mtafaruku ndani ya chama hicho.

Wameweka wazi kuwa hivi sasa mpasuko utakuwa zaidi ndani ya chama hicho hasa baada ya taarifa kuwa Chiligati na Nape walikuwa wakiwashambulia makada wenzao tofauti na maagizo ya kikao cha NEC kilichofanyika Aprili mwaka huu. Wamedokeza kuwa sasa makundi hasimu yatajiimarisha ili kuhakikisha makada wanaowaunga mkono hawapati adhabu pindi itakapobainika wamekwenda kinyume na maadili ya chama hicho.
 
Kaole style at work, watafunika kombe mpaka lini?
Migongano si inaendelea kujengeka ? Usipokunywa krolokwini utaishia ICU . Any way bora iwe hivyo ili magamba yapasuke
 
Lowassa anaonekana kuwa bado ni tishio kwa vigogo wanaotajwa tajwa kuwania urais mwaka 2015.

Walibainisha kuwa licha ya kuwepo mikakati ya kutaka kiongozi huyo asipate fursa ya kujenga mtandao wa kumsaidia kuingia ikulu, Lowassa anaonekana kuwa imara zaidi kukabiliana na wapinzani wake.
Hili gazeti linazidi kupoteza muelekeo, Freeman asipomuondoa Kibanda kama mhariri mkuu na kumpa nafasi hiyo Ngurumo hili gazeti litapoteza umaarufu kama na kutoweka kama motomoto enzi za NCCR ya Mrema!

Matumizi ya Kibanda yanayofanywa na Lowassa yanaharibu sifa ya TANZANIA DAIMA, Gazeti limekuwa likifanya kazi za CCM Lowassa!
 
Unafika huwa una kikomo, na kikomo chake hakiachi fedheha nyuma. Kuhusu magamba sasa watavuana mpaka ngua za ndani wakifikiri ni magamba.
 
Ee Mungu eponye Tanzania, mi nashangaa ivi hawa watu wanatafuta nini kwenye nchi yetu pamoja na mapesa yote waliyo nayo, 2015 ni wakati Mungu kuiponya Tanzania hakika atatusaidia

Mzee Gomezi
 
Hamna jambo zuri litakalojenga mustakabali wa nchii hii kama kugombana hadharani na hatimaye kuvunjika urafiki kati ya EL na JK. Sasa hivi hii yote ni minong'ono na ugomvi wa chinichini, bado urafiki wao upo imara.
Think of all the repercussions, hizi si zama za Nyerere ukigombana naye unakimbilia nje au unapotea kabisa, siku hizi ni hapahapa.
 
na Salehe Mohamed
Tanzania Daima


RAIS mstaafu Benjamin Mkapa, alimnusuru Rais Jakaya Kikwete kwenye kitanzi cha kung’olewa kwenye wadhifa wa uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima Jumapili limedokezwa.

Kwa mujibu wa wajumbe waliohudhuria kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) kilichomalizika Novemba 24 mwaka huu mkoani Dodoma, walibainisha kuwa baadhi ya wajumbe walijipanga kutoa hoja ya kumtaka Rais Kikwete kuachia wadhifa wake.

Wanasema kuwa walipanga kufanya hivyo kwa madai kuwa katika kipindi cha utawala wa Rais Kikwete chama kimekuwa na migogoro mikubwa na kuifanya serikali iyumbe kila kukicha.

Walibainisha kuwa fursa ya kutoa hoja hiyo haikupatikana baada ya Mkapa kumtaka Rais Kikwete kusitisha hoja ya kuvuana magamba, baada ya kuona upepo mbaya ulikuwa ukimvumia kiongozi huyo.

Inadaiwa Kikwete alikubali ‘msaada’ huo wa Mkapa ambapo alisema hoja hiyo imetosha kwa kuwa suala hilo lilirejeshwa kwenye kamati ya maadili, ambayo itapokea ushahidi wa tuhuma za makada hao pamoja na kuwapa fursa ya kuwasikiliza watuhumiwa.

Kwa mujibu wa wajumbe hao wa NEC, waligawanyika makundi mawili, moja likitaka Lowassa atoswe kwenye uongozi huku jingine likipinga kwa madai kuwa tuhuma za kada huyo hazijathibitishwa.

Lowassa alipopata nafasi ya kuchangia hoja hiyo, alieleza kusikitishwa na ufisadi wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambapo alisema kila alichokuwa akikifanya Rais Kikwete alikuwa anakijua kama si kumtuma.


Aliongeza kuwa pamoja na kujua huko kwa Rais Kikwete juu ya kashfa hiyo, bado alishindwa kuwakemea watu waliokuwa wakimhusisha Lowassa na ufisadi wa Richmond, ambao inadaiwa ulifanywa na watendaji wa serikali.

Rais Kikwete na wasaidizi wake mara kadhaa wamekuwa wakikana kiongozi huyo mkuu wa nchi kuijua na kuhusika na mkataba wa Richmond ambao ulifanya Bunge kuunda kamati teule kuchunguza mchakato ulioipa ushindi zabuni ya kampuni hiyo.

Katika kikao hicho cha NEC, Lowassa alibainisha kuwa kama tuhuma zingekuwa zinamng’oa mtu madarakani bila kufanyiwa kazi, basi Rais Kikwete asingekalia kiti cha uenyekiti wa CCM kwani mwaka 2003 alizushiwa tuhuma za ukosefu wa maadili na kada mwenzao, Paul Sozigwa.

Mbunge huyo alisema kama si busara za Mwenyekiti wa CCM wakati huo, Benjamin Mkapa, Rais Kikwete asingeukwaa urais, hivyo ni vema chama kifuate utaratibu waliojiwekea wa kushughulikia tuhuma zinazoelekezwa kwa makada wake.

Baada ya Lowassa kutoa utetezi wake huo, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, alisema halikuwa jambo la busara kuwatuhumu watu na kutangaza tuhuma dhidi yao kabla ya kuthibitishwa kwa tuhuma zenyewe.

Sumaye alionekana kukerwa na ukimya wa Rais Kikwete juu ya kuchafuliwa kwa Lowassa kulikokuwa kukifanywa na Katibu wa Itikadi na Unezi, Nape Nnauye pamoja na Naibu Katibu Mkuu (Bara), John Chiligati.

Sumaye alihoji iwapo kamati ya maadili itabaini kuwa Lowassa hakuwa na hatia, hatua gani zitachukuliwa dhidi ya Chiligati na Nape waliosambaza tuhuma hizo.

Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa kuwa hoja ya kumng’oa Kikwete ilikuwa ikiungwa mkono kichini chini na vigogo wengi ambao hapo awali walikuwa wakidaiwa kumuunga mkono Rais Kikwete.

Vigogo hao inadaiwa hivi sasa wamekuwa wakikerwa na jinsi Rais Kikwete anavyoyashughulikia matatizo ya chama hicho kwa kuendekeza siasa za makundi yanayohasimiana.

Baadhi ya wajumbe wa NEC, wamelidokeza Tanzania Daima kuwa kama Rais Kikwete hatajirekebisha kwa jinsi anavyoshughulikia matatizo ya chama tishio la kung’olewa kwenye unyekiti wa chama hicho litaendelea kumuandamana.

Waliongeza kuwa kwa hali ilivyokuwa ndani ya kikao hicho, Lowassa anaonekana kuwa bado ni tishio kwa vigogo wanaotajwa tajwa kuwania urais mwaka 2015.

Walibainisha kuwa licha ya kuwepo mikakati ya kutaka kiongozi huyo asipate fursa ya kujenga mtandao wa kumsaidia kuingia ikulu, Lowassa anaonekana kuwa imara zaidi kukabiliana na wapinzani wake.

Kabla ya NEC

Awali kulikuwa na tetesi kuwa Rais Kikwete alipokea pendekezo ya kuwang’oa madarakani baadhi ya viongozi wa chama hicho wanaodaiwa kuwa ndio chanzo cha mitafaruku ndani ya CCM.

Miongoni mwa waliokuwa wakisemwa kung’olewa madarakani ni Lowassa, Sitta, Nape, Chiligati na Chenge.

Inadaiwa kuwa baadhi ya makada wa chama hicho walikodishiwa usafiri kutoka kwenye maeneo yao na kulipwa posho ili kwenda kushangilia Lowassa, Chenge na wengineo wanavulia madaraka.

Kundi jingine nalo linadaiwa kupelekwa mkoani Dodoma kwa lengo la kushangilia kung’olewa kwa Sitta, Nape na Chiligati.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaweka wazi kuwa uamuzi wa CCM kulirejesha suala la kujivua gamba kwa kamati kuu ambayo italipeleka suala hilo kwenye kamati ya maadili kutafutiwa ufumbuzi kutazidisha mtafaruku ndani ya chama hicho.

Wameweka wazi kuwa hivi sasa mpasuko utakuwa zaidi ndani ya chama hicho hasa baada ya taarifa kuwa Chiligati na Nape walikuwa wakiwashambulia makada wenzao tofauti na maagizo ya kikao cha NEC kilichofanyika Aprili mwaka huu. Wamedokeza kuwa sasa makundi hasimu yatajiimarisha ili kuhakikisha makada wanaowaunga mkono hawapati adhabu pindi itakapobainika wamekwenda kinyume na maadili ya chama hicho.

Hili zege limeshakorogwa lazima ukuta ujengwe
 
Lowassa ni wetu (hatujakutana barabarani, nooo), CCM ni yetu na Ikulu ni kwetu. Kelele za mlango hazi.....mkitaka kikao na mh. Rais dr.JK leteni barua ikulu mtasikilizwa, mbona mifano iko wazi jamani!
 
na Salehe Mohamed
Tanzania Daima


RAIS mstaafu Benjamin Mkapa, alimnusuru Rais Jakaya Kikwete kwenye kitanzi cha kung’olewa kwenye wadhifa wa uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima Jumapili limedokezwa.


Inadaiwa Kikwete alikubali ‘msaada’ huo wa Mkapa ambapo alisema hoja hiyo imetosha...........Lowassa alipopata nafasi ya kuchangia hoja hiyo, alieleza kusikitishwa na ufisadi wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambapo alisema kila alichokuwa akikifanya Rais Kikwete alikuwa anakijua kama si kumtuma.

Aliongeza kuwa pamoja na kujua huko kwa Rais Kikwete juu ya kashfa hiyo, bado alishindwa kuwakemea watu waliokuwa wakimhusisha Lowassa na ufisadi wa Richmond, ambao inadaiwa ulifanywa na watendaji wa serikali.

Rais Kikwete na wasaidizi wake mara kadhaa wamekuwa wakikana kiongozi huyo mkuu wa nchi kuijua na kuhusika na mkataba wa Richmond ambao ulifanya Bunge kuunda kamati teule kuchunguza mchakato ulioipa ushindi zabuni ya kampuni hiyo.

Katika kikao hicho cha NEC, Lowassa alibainisha kuwa kama tuhuma zingekuwa zinamng’oa mtu madarakani bila kufanyiwa kazi, basi Rais Kikwete asingekalia kiti cha uenyekiti wa CCM kwani mwaka 2003 alizushiwa tuhuma za ukosefu wa maadili na kada mwenzao, Paul Sozigwa.

Mbunge huyo alisema kama si busara za Mwenyekiti wa CCM wakati huo, Benjamin Mkapa, Rais Kikwete asingeukwaa urais, hivyo ni vema chama kifuate utaratibu waliojiwekea wa kushughulikia tuhuma zinazoelekezwa kwa makada wake.

.

Kama unachofanyiwa wewe Lowassa ni uzushi,na unasema hata JK alifanyiwa uzushi,basi kwangu mimi na Watanzania wengi tunaoona ni ukweli Basi wewe Lowassa na Kikwete wote hamna maana na mmekosa legitimacy ya kutuongoza kwa sababu kila kitu ni kweli juu yako, hivyo basi na kwake ilikuwa kweli(Hatukukutana barabarani EL,2010-2011pp.1).Kulingana na article hii "JK hana Maadili" (Sozigwa 2003).
Richmond inajulikana na Jakaya Kikwete (Edward Lowassa,2008-2011).
 
Hili gazeti linazidi kupoteza muelekeo, Freeman asipomuondoa Kibanda kama mhariri mkuu na kumpa nafasi hiyo Ngurumo hili gazeti litapoteza umaarufu kama na kutoweka kama motomoto enzi za NCCR ya Mrema!

Matumizi ya Kibanda yanayofanywa na Lowassa yanaharibu sifa ya TANZANIA DAIMA, Gazeti limekuwa likifanya kazi za CCM Lowassa!

uliishandanganywa na kujiaminisha

tulisema na tunasema huwezi kutofautisha, JK, EL, CDM, na Mbowe.........nje ya hapo ni ubishi na aibu!
 
na Salehe Mohamed
Tanzania Daima


RAIS mstaafu Benjamin Mkapa, alimnusuru Rais Jakaya Kikwete kwenye kitanzi cha kung'olewa kwenye wadhifa wa uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima Jumapili limedokezwa.

Kwa mujibu wa wajumbe waliohudhuria kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) kilichomalizika Novemba 24 mwaka huu mkoani Dodoma, walibainisha kuwa baadhi ya wajumbe walijipanga kutoa hoja ya kumtaka Rais Kikwete kuachia wadhifa wake.

Wanasema kuwa walipanga kufanya hivyo kwa madai kuwa katika kipindi cha utawala wa Rais Kikwete chama kimekuwa na migogoro mikubwa na kuifanya serikali iyumbe kila kukicha.

Walibainisha kuwa fursa ya kutoa hoja hiyo haikupatikana baada ya Mkapa kumtaka Rais Kikwete kusitisha hoja ya kuvuana magamba, baada ya kuona upepo mbaya ulikuwa ukimvumia kiongozi huyo.

Inadaiwa Kikwete alikubali ‘msaada' huo wa Mkapa ambapo alisema hoja hiyo imetosha kwa kuwa suala hilo lilirejeshwa kwenye kamati ya maadili, ambayo itapokea ushahidi wa tuhuma za makada hao pamoja na kuwapa fursa ya kuwasikiliza watuhumiwa.

Kwa mujibu wa wajumbe hao wa NEC, waligawanyika makundi mawili, moja likitaka Lowassa atoswe kwenye uongozi huku jingine likipinga kwa madai kuwa tuhuma za kada huyo hazijathibitishwa.

Lowassa alipopata nafasi ya kuchangia hoja hiyo, alieleza kusikitishwa na ufisadi wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambapo alisema kila alichokuwa akikifanya Rais Kikwete alikuwa anakijua kama si kumtuma.

Aliongeza kuwa pamoja na kujua huko kwa Rais Kikwete juu ya kashfa hiyo, bado alishindwa kuwakemea watu waliokuwa wakimhusisha Lowassa na ufisadi wa Richmond, ambao inadaiwa ulifanywa na watendaji wa serikali.

Rais Kikwete na wasaidizi wake mara kadhaa wamekuwa wakikana kiongozi huyo mkuu wa nchi kuijua na kuhusika na mkataba wa Richmond ambao ulifanya Bunge kuunda kamati teule kuchunguza mchakato ulioipa ushindi zabuni ya kampuni hiyo.

Katika kikao hicho cha NEC, Lowassa alibainisha kuwa kama tuhuma zingekuwa zinamng'oa mtu madarakani bila kufanyiwa kazi, basi Rais Kikwete asingekalia kiti cha uenyekiti wa CCM kwani mwaka 2003 alizushiwa tuhuma za ukosefu wa maadili na kada mwenzao, Paul Sozigwa.

Mbunge huyo alisema kama si busara za Mwenyekiti wa CCM wakati huo, Benjamin Mkapa, Rais Kikwete asingeukwaa urais, hivyo ni vema chama kifuate utaratibu waliojiwekea wa kushughulikia tuhuma zinazoelekezwa kwa makada wake.

Baada ya Lowassa kutoa utetezi wake huo, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, alisema halikuwa jambo la busara kuwatuhumu watu na kutangaza tuhuma dhidi yao kabla ya kuthibitishwa kwa tuhuma zenyewe.

Sumaye alionekana kukerwa na ukimya wa Rais Kikwete juu ya kuchafuliwa kwa Lowassa kulikokuwa kukifanywa na Katibu wa Itikadi na Unezi, Nape Nnauye pamoja na Naibu Katibu Mkuu (Bara), John Chiligati.

Sumaye alihoji iwapo kamati ya maadili itabaini kuwa Lowassa hakuwa na hatia, hatua gani zitachukuliwa dhidi ya Chiligati na Nape waliosambaza tuhuma hizo.

Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa kuwa hoja ya kumng'oa Kikwete ilikuwa ikiungwa mkono kichini chini na vigogo wengi ambao hapo awali walikuwa wakidaiwa kumuunga mkono Rais Kikwete.

Vigogo hao inadaiwa hivi sasa wamekuwa wakikerwa na jinsi Rais Kikwete anavyoyashughulikia matatizo ya chama hicho kwa kuendekeza siasa za makundi yanayohasimiana.

Baadhi ya wajumbe wa NEC, wamelidokeza Tanzania Daima kuwa kama Rais Kikwete hatajirekebisha kwa jinsi anavyoshughulikia matatizo ya chama tishio la kung'olewa kwenye unyekiti wa chama hicho litaendelea kumuandamana.

Waliongeza kuwa kwa hali ilivyokuwa ndani ya kikao hicho, Lowassa anaonekana kuwa bado ni tishio kwa vigogo wanaotajwa tajwa kuwania urais mwaka 2015.

Walibainisha kuwa licha ya kuwepo mikakati ya kutaka kiongozi huyo asipate fursa ya kujenga mtandao wa kumsaidia kuingia ikulu, Lowassa anaonekana kuwa imara zaidi kukabiliana na wapinzani wake.

Kabla ya NEC

Awali kulikuwa na tetesi kuwa Rais Kikwete alipokea pendekezo ya kuwang'oa madarakani baadhi ya viongozi wa chama hicho wanaodaiwa kuwa ndio chanzo cha mitafaruku ndani ya CCM.

Miongoni mwa waliokuwa wakisemwa kung'olewa madarakani ni Lowassa, Sitta, Nape, Chiligati na Chenge.

Inadaiwa kuwa baadhi ya makada wa chama hicho walikodishiwa usafiri kutoka kwenye maeneo yao na kulipwa posho ili kwenda kushangilia Lowassa, Chenge na wengineo wanavulia madaraka.

Kundi jingine nalo linadaiwa kupelekwa mkoani Dodoma kwa lengo la kushangilia kung'olewa kwa Sitta, Nape na Chiligati.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaweka wazi kuwa uamuzi wa CCM kulirejesha suala la kujivua gamba kwa kamati kuu ambayo italipeleka suala hilo kwenye kamati ya maadili kutafutiwa ufumbuzi kutazidisha mtafaruku ndani ya chama hicho.

Wameweka wazi kuwa hivi sasa mpasuko utakuwa zaidi ndani ya chama hicho hasa baada ya taarifa kuwa Chiligati na Nape walikuwa wakiwashambulia makada wenzao tofauti na maagizo ya kikao cha NEC kilichofanyika Aprili mwaka huu. Wamedokeza kuwa sasa makundi hasimu yatajiimarisha ili kuhakikisha makada wanaowaunga mkono hawapati adhabu pindi itakapobainika wamekwenda kinyume na maadili ya chama hicho.
Hizi ndizo thrd tunazozisahau leo hii na kuanza kusema tunakumisi. Leo hii tena kuna watu wanaomba Magufuli ang'olewe. Wapi!!
 
Hadithi ni hizi hizi kila awamu. Wengine wameamua kuwa washabiki wa kudumu wa hizi ngano. Watu wanapoteza muda sijui Membe au nani anamtoa JPM madarakani ...tusubiri vilio vile vile vya wizi wa kura hadi tutapopata kizazi serious ila sio chetu hiki kisicho na msimamo.
 
Kafanya lipi la maana zaidi ya unduli na udikteta!? Kudharau katiba, bunge, mahakama, ofisi ya CAG, wizi, ufisadi, dhuluma kwa wakulima, wafanyakazi na wafanyabiashara, ubadhirifu, uongo, utekaji, utesaji na UUAJI.

Janga kubwa la Taifa huyu na ni mkosi mkubwa sana kwa Watanzania kuwa na mwendawazimu eti ndiyo kiongozi wa nchi!!!

Hizi ndizo thrd tunazozisahau leo hii na kuanza kusema tunakumisi. Leo hii tena kuna watu wanaomba Magufuli ang'olewe. Wapi!!
 
Hili gazeti tangu zamani lilikuwa la kufungia maandazi
na Salehe Mohamed
Tanzania Daima


RAIS mstaafu Benjamin Mkapa, alimnusuru Rais Jakaya Kikwete kwenye kitanzi cha kung'olewa kwenye wadhifa wa uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima Jumapili limedokezwa.

Kwa mujibu wa wajumbe waliohudhuria kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) kilichomalizika Novemba 24 mwaka huu mkoani Dodoma, walibainisha kuwa baadhi ya wajumbe walijipanga kutoa hoja ya kumtaka Rais Kikwete kuachia wadhifa wake.

Wanasema kuwa walipanga kufanya hivyo kwa madai kuwa katika kipindi cha utawala wa Rais Kikwete chama kimekuwa na migogoro mikubwa na kuifanya serikali iyumbe kila kukicha.

Walibainisha kuwa fursa ya kutoa hoja hiyo haikupatikana baada ya Mkapa kumtaka Rais Kikwete kusitisha hoja ya kuvuana magamba, baada ya kuona upepo mbaya ulikuwa ukimvumia kiongozi huyo.

Inadaiwa Kikwete alikubali ‘msaada' huo wa Mkapa ambapo alisema hoja hiyo imetosha kwa kuwa suala hilo lilirejeshwa kwenye kamati ya maadili, ambayo itapokea ushahidi wa tuhuma za makada hao pamoja na kuwapa fursa ya kuwasikiliza watuhumiwa.

Kwa mujibu wa wajumbe hao wa NEC, waligawanyika makundi mawili, moja likitaka Lowassa atoswe kwenye uongozi huku jingine likipinga kwa madai kuwa tuhuma za kada huyo hazijathibitishwa.

Lowassa alipopata nafasi ya kuchangia hoja hiyo, alieleza kusikitishwa na ufisadi wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambapo alisema kila alichokuwa akikifanya Rais Kikwete alikuwa anakijua kama si kumtuma.

Aliongeza kuwa pamoja na kujua huko kwa Rais Kikwete juu ya kashfa hiyo, bado alishindwa kuwakemea watu waliokuwa wakimhusisha Lowassa na ufisadi wa Richmond, ambao inadaiwa ulifanywa na watendaji wa serikali.

Rais Kikwete na wasaidizi wake mara kadhaa wamekuwa wakikana kiongozi huyo mkuu wa nchi kuijua na kuhusika na mkataba wa Richmond ambao ulifanya Bunge kuunda kamati teule kuchunguza mchakato ulioipa ushindi zabuni ya kampuni hiyo.

Katika kikao hicho cha NEC, Lowassa alibainisha kuwa kama tuhuma zingekuwa zinamng'oa mtu madarakani bila kufanyiwa kazi, basi Rais Kikwete asingekalia kiti cha uenyekiti wa CCM kwani mwaka 2003 alizushiwa tuhuma za ukosefu wa maadili na kada mwenzao, Paul Sozigwa.

Mbunge huyo alisema kama si busara za Mwenyekiti wa CCM wakati huo, Benjamin Mkapa, Rais Kikwete asingeukwaa urais, hivyo ni vema chama kifuate utaratibu waliojiwekea wa kushughulikia tuhuma zinazoelekezwa kwa makada wake.

Baada ya Lowassa kutoa utetezi wake huo, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, alisema halikuwa jambo la busara kuwatuhumu watu na kutangaza tuhuma dhidi yao kabla ya kuthibitishwa kwa tuhuma zenyewe.

Sumaye alionekana kukerwa na ukimya wa Rais Kikwete juu ya kuchafuliwa kwa Lowassa kulikokuwa kukifanywa na Katibu wa Itikadi na Unezi, Nape Nnauye pamoja na Naibu Katibu Mkuu (Bara), John Chiligati.

Sumaye alihoji iwapo kamati ya maadili itabaini kuwa Lowassa hakuwa na hatia, hatua gani zitachukuliwa dhidi ya Chiligati na Nape waliosambaza tuhuma hizo.

Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa kuwa hoja ya kumng'oa Kikwete ilikuwa ikiungwa mkono kichini chini na vigogo wengi ambao hapo awali walikuwa wakidaiwa kumuunga mkono Rais Kikwete.

Vigogo hao inadaiwa hivi sasa wamekuwa wakikerwa na jinsi Rais Kikwete anavyoyashughulikia matatizo ya chama hicho kwa kuendekeza siasa za makundi yanayohasimiana.

Baadhi ya wajumbe wa NEC, wamelidokeza Tanzania Daima kuwa kama Rais Kikwete hatajirekebisha kwa jinsi anavyoshughulikia matatizo ya chama tishio la kung'olewa kwenye unyekiti wa chama hicho litaendelea kumuandamana.

Waliongeza kuwa kwa hali ilivyokuwa ndani ya kikao hicho, Lowassa anaonekana kuwa bado ni tishio kwa vigogo wanaotajwa tajwa kuwania urais mwaka 2015.

Walibainisha kuwa licha ya kuwepo mikakati ya kutaka kiongozi huyo asipate fursa ya kujenga mtandao wa kumsaidia kuingia ikulu, Lowassa anaonekana kuwa imara zaidi kukabiliana na wapinzani wake.

Kabla ya NEC

Awali kulikuwa na tetesi kuwa Rais Kikwete alipokea pendekezo ya kuwang'oa madarakani baadhi ya viongozi wa chama hicho wanaodaiwa kuwa ndio chanzo cha mitafaruku ndani ya CCM.

Miongoni mwa waliokuwa wakisemwa kung'olewa madarakani ni Lowassa, Sitta, Nape, Chiligati na Chenge.

Inadaiwa kuwa baadhi ya makada wa chama hicho walikodishiwa usafiri kutoka kwenye maeneo yao na kulipwa posho ili kwenda kushangilia Lowassa, Chenge na wengineo wanavulia madaraka.

Kundi jingine nalo linadaiwa kupelekwa mkoani Dodoma kwa lengo la kushangilia kung'olewa kwa Sitta, Nape na Chiligati.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaweka wazi kuwa uamuzi wa CCM kulirejesha suala la kujivua gamba kwa kamati kuu ambayo italipeleka suala hilo kwenye kamati ya maadili kutafutiwa ufumbuzi kutazidisha mtafaruku ndani ya chama hicho.

Wameweka wazi kuwa hivi sasa mpasuko utakuwa zaidi ndani ya chama hicho hasa baada ya taarifa kuwa Chiligati na Nape walikuwa wakiwashambulia makada wenzao tofauti na maagizo ya kikao cha NEC kilichofanyika Aprili mwaka huu. Wamedokeza kuwa sasa makundi hasimu yatajiimarisha ili kuhakikisha makada wanaowaunga mkono hawapati adhabu pindi itakapobainika wamekwenda kinyume na maadili ya chama hicho.
 
Kafanya lipi la maana zaidi ya unduli na udikteta!? Kudharau katiba, bunge, mahakama, ofisi ya CAG, wizi, ufisadi, dhuluma kwa wakulima, wafanyakazi na wafanyabiashara, ubadhirifu, uongo, utekaji, utesaji na UUAJI.

Janga kubwa la Taifa huyu na ni mkosi mkubwa sana kwa Watanzania kuwa na mwendawazimu eti ndiyo kiongozi wa nchi!!!
Hebu nenda deep kidogo, Boss. Katiba ipi na mambo gani hayo?
Ukiamua kutukana kwa hasira utakosa wafuasi. Hebu taja moja baada ya jingine maana ukisema vyeti feki utumbuaji na mengine, sisi tutasema aendelee!
 
Kilichoandikwa ni ukweli mtupu na huo mpasuko ndani ya chama cha mafisadi bado ni mkubwa tu wa kambi ya membe na nduli wa Ikulu’ wa kambi ya Nape na Bashe wabaki Bungeni 2020 na kambi ya dikteta wa Ikulu eti hao hawastahili kurudi kwa kuwa wana NONGWA!!! Kusema ukweli kuhusu huyo nduli kushindwa kwenye kila kitu nchini na hivyo kutostahili kupewa awamu nyingine inaonekana ni NONGWA!

Kweli ccm kumejaa mafisi yenye njaa kali sana.

Hili gazeti tangu zamani lilikuwa la kufungia maandazi
 
Hebu nenda deep kidogo, Boss. Katiba ipi na mambo gani hayo?
Ukiamua kutukana kwa hasira utakosa wafuasi. Hebu taja moja baada ya jingine maana ukisema vyeti feki utumbuaji na mengine, sisi tutasema aendelee!
Kipi ambacho hukijui au unataka kutupotezea muda tu ?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Kilichoandikwa ni ukweli mtupu na huo mpasuko ndani ya chama cha mafisadi bado ni mkubwa tu wa kambi ya membe na nduli wa Ikulu’ wa kambi ya Nape na Bashe wabaki Bungeni 2020 na kambi ya dikteta wa Ikulu eti hao hawastahili kurudi kwa kuwa wana NONGWA!!! Kusema ukweli kuhusu huyo nduli kushindwa kwenye kila kitu nchini na hivyo kutostahili kupewa awamu nyingine inaonekana ni NONGWA!

Kweli ccm kumejaa mafisi yenye njaa kali sana.
umaarufu wake umeporomoka hadi 41% hii ni taarifa ya leo .
 
Back
Top Bottom