BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,013
na Salehe Mohamed
Tanzania Daima
RAIS mstaafu Benjamin Mkapa, alimnusuru Rais Jakaya Kikwete kwenye kitanzi cha kung'olewa kwenye wadhifa wa uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima Jumapili limedokezwa.
Kwa mujibu wa wajumbe waliohudhuria kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) kilichomalizika Novemba 24 mwaka huu mkoani Dodoma, walibainisha kuwa baadhi ya wajumbe walijipanga kutoa hoja ya kumtaka Rais Kikwete kuachia wadhifa wake.
Wanasema kuwa walipanga kufanya hivyo kwa madai kuwa katika kipindi cha utawala wa Rais Kikwete chama kimekuwa na migogoro mikubwa na kuifanya serikali iyumbe kila kukicha.
Walibainisha kuwa fursa ya kutoa hoja hiyo haikupatikana baada ya Mkapa kumtaka Rais Kikwete kusitisha hoja ya kuvuana magamba, baada ya kuona upepo mbaya ulikuwa ukimvumia kiongozi huyo.
Inadaiwa Kikwete alikubali ‘msaada' huo wa Mkapa ambapo alisema hoja hiyo imetosha kwa kuwa suala hilo lilirejeshwa kwenye kamati ya maadili, ambayo itapokea ushahidi wa tuhuma za makada hao pamoja na kuwapa fursa ya kuwasikiliza watuhumiwa.
Kwa mujibu wa wajumbe hao wa NEC, waligawanyika makundi mawili, moja likitaka Lowassa atoswe kwenye uongozi huku jingine likipinga kwa madai kuwa tuhuma za kada huyo hazijathibitishwa.
Lowassa alipopata nafasi ya kuchangia hoja hiyo, alieleza kusikitishwa na ufisadi wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambapo alisema kila alichokuwa akikifanya Rais Kikwete alikuwa anakijua kama si kumtuma.
Aliongeza kuwa pamoja na kujua huko kwa Rais Kikwete juu ya kashfa hiyo, bado alishindwa kuwakemea watu waliokuwa wakimhusisha Lowassa na ufisadi wa Richmond, ambao inadaiwa ulifanywa na watendaji wa serikali.
Rais Kikwete na wasaidizi wake mara kadhaa wamekuwa wakikana kiongozi huyo mkuu wa nchi kuijua na kuhusika na mkataba wa Richmond ambao ulifanya Bunge kuunda kamati teule kuchunguza mchakato ulioipa ushindi zabuni ya kampuni hiyo.
Katika kikao hicho cha NEC, Lowassa alibainisha kuwa kama tuhuma zingekuwa zinamng'oa mtu madarakani bila kufanyiwa kazi, basi Rais Kikwete asingekalia kiti cha uenyekiti wa CCM kwani mwaka 2003 alizushiwa tuhuma za ukosefu wa maadili na kada mwenzao, Paul Sozigwa.
Mbunge huyo alisema kama si busara za Mwenyekiti wa CCM wakati huo, Benjamin Mkapa, Rais Kikwete asingeukwaa urais, hivyo ni vema chama kifuate utaratibu waliojiwekea wa kushughulikia tuhuma zinazoelekezwa kwa makada wake.
Baada ya Lowassa kutoa utetezi wake huo, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, alisema halikuwa jambo la busara kuwatuhumu watu na kutangaza tuhuma dhidi yao kabla ya kuthibitishwa kwa tuhuma zenyewe.
Sumaye alionekana kukerwa na ukimya wa Rais Kikwete juu ya kuchafuliwa kwa Lowassa kulikokuwa kukifanywa na Katibu wa Itikadi na Unezi, Nape Nnauye pamoja na Naibu Katibu Mkuu (Bara), John Chiligati.
Sumaye alihoji iwapo kamati ya maadili itabaini kuwa Lowassa hakuwa na hatia, hatua gani zitachukuliwa dhidi ya Chiligati na Nape waliosambaza tuhuma hizo.
Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa kuwa hoja ya kumng'oa Kikwete ilikuwa ikiungwa mkono kichini chini na vigogo wengi ambao hapo awali walikuwa wakidaiwa kumuunga mkono Rais Kikwete.
Vigogo hao inadaiwa hivi sasa wamekuwa wakikerwa na jinsi Rais Kikwete anavyoyashughulikia matatizo ya chama hicho kwa kuendekeza siasa za makundi yanayohasimiana.
Baadhi ya wajumbe wa NEC, wamelidokeza Tanzania Daima kuwa kama Rais Kikwete hatajirekebisha kwa jinsi anavyoshughulikia matatizo ya chama tishio la kung'olewa kwenye unyekiti wa chama hicho litaendelea kumuandamana.
Waliongeza kuwa kwa hali ilivyokuwa ndani ya kikao hicho, Lowassa anaonekana kuwa bado ni tishio kwa vigogo wanaotajwa tajwa kuwania urais mwaka 2015.
Walibainisha kuwa licha ya kuwepo mikakati ya kutaka kiongozi huyo asipate fursa ya kujenga mtandao wa kumsaidia kuingia ikulu, Lowassa anaonekana kuwa imara zaidi kukabiliana na wapinzani wake.
Kabla ya NEC
Awali kulikuwa na tetesi kuwa Rais Kikwete alipokea pendekezo ya kuwang'oa madarakani baadhi ya viongozi wa chama hicho wanaodaiwa kuwa ndio chanzo cha mitafaruku ndani ya CCM.
Miongoni mwa waliokuwa wakisemwa kung'olewa madarakani ni Lowassa, Sitta, Nape, Chiligati na Chenge.
Inadaiwa kuwa baadhi ya makada wa chama hicho walikodishiwa usafiri kutoka kwenye maeneo yao na kulipwa posho ili kwenda kushangilia Lowassa, Chenge na wengineo wanavulia madaraka.
Kundi jingine nalo linadaiwa kupelekwa mkoani Dodoma kwa lengo la kushangilia kung'olewa kwa Sitta, Nape na Chiligati.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaweka wazi kuwa uamuzi wa CCM kulirejesha suala la kujivua gamba kwa kamati kuu ambayo italipeleka suala hilo kwenye kamati ya maadili kutafutiwa ufumbuzi kutazidisha mtafaruku ndani ya chama hicho.
Wameweka wazi kuwa hivi sasa mpasuko utakuwa zaidi ndani ya chama hicho hasa baada ya taarifa kuwa Chiligati na Nape walikuwa wakiwashambulia makada wenzao tofauti na maagizo ya kikao cha NEC kilichofanyika Aprili mwaka huu. Wamedokeza kuwa sasa makundi hasimu yatajiimarisha ili kuhakikisha makada wanaowaunga mkono hawapati adhabu pindi itakapobainika wamekwenda kinyume na maadili ya chama hicho.
Tanzania Daima
RAIS mstaafu Benjamin Mkapa, alimnusuru Rais Jakaya Kikwete kwenye kitanzi cha kung'olewa kwenye wadhifa wa uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima Jumapili limedokezwa.
Kwa mujibu wa wajumbe waliohudhuria kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) kilichomalizika Novemba 24 mwaka huu mkoani Dodoma, walibainisha kuwa baadhi ya wajumbe walijipanga kutoa hoja ya kumtaka Rais Kikwete kuachia wadhifa wake.
Wanasema kuwa walipanga kufanya hivyo kwa madai kuwa katika kipindi cha utawala wa Rais Kikwete chama kimekuwa na migogoro mikubwa na kuifanya serikali iyumbe kila kukicha.
Walibainisha kuwa fursa ya kutoa hoja hiyo haikupatikana baada ya Mkapa kumtaka Rais Kikwete kusitisha hoja ya kuvuana magamba, baada ya kuona upepo mbaya ulikuwa ukimvumia kiongozi huyo.
Inadaiwa Kikwete alikubali ‘msaada' huo wa Mkapa ambapo alisema hoja hiyo imetosha kwa kuwa suala hilo lilirejeshwa kwenye kamati ya maadili, ambayo itapokea ushahidi wa tuhuma za makada hao pamoja na kuwapa fursa ya kuwasikiliza watuhumiwa.
Kwa mujibu wa wajumbe hao wa NEC, waligawanyika makundi mawili, moja likitaka Lowassa atoswe kwenye uongozi huku jingine likipinga kwa madai kuwa tuhuma za kada huyo hazijathibitishwa.
Lowassa alipopata nafasi ya kuchangia hoja hiyo, alieleza kusikitishwa na ufisadi wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond ambapo alisema kila alichokuwa akikifanya Rais Kikwete alikuwa anakijua kama si kumtuma.
Aliongeza kuwa pamoja na kujua huko kwa Rais Kikwete juu ya kashfa hiyo, bado alishindwa kuwakemea watu waliokuwa wakimhusisha Lowassa na ufisadi wa Richmond, ambao inadaiwa ulifanywa na watendaji wa serikali.
Rais Kikwete na wasaidizi wake mara kadhaa wamekuwa wakikana kiongozi huyo mkuu wa nchi kuijua na kuhusika na mkataba wa Richmond ambao ulifanya Bunge kuunda kamati teule kuchunguza mchakato ulioipa ushindi zabuni ya kampuni hiyo.
Katika kikao hicho cha NEC, Lowassa alibainisha kuwa kama tuhuma zingekuwa zinamng'oa mtu madarakani bila kufanyiwa kazi, basi Rais Kikwete asingekalia kiti cha uenyekiti wa CCM kwani mwaka 2003 alizushiwa tuhuma za ukosefu wa maadili na kada mwenzao, Paul Sozigwa.
Mbunge huyo alisema kama si busara za Mwenyekiti wa CCM wakati huo, Benjamin Mkapa, Rais Kikwete asingeukwaa urais, hivyo ni vema chama kifuate utaratibu waliojiwekea wa kushughulikia tuhuma zinazoelekezwa kwa makada wake.
Baada ya Lowassa kutoa utetezi wake huo, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, alisema halikuwa jambo la busara kuwatuhumu watu na kutangaza tuhuma dhidi yao kabla ya kuthibitishwa kwa tuhuma zenyewe.
Sumaye alionekana kukerwa na ukimya wa Rais Kikwete juu ya kuchafuliwa kwa Lowassa kulikokuwa kukifanywa na Katibu wa Itikadi na Unezi, Nape Nnauye pamoja na Naibu Katibu Mkuu (Bara), John Chiligati.
Sumaye alihoji iwapo kamati ya maadili itabaini kuwa Lowassa hakuwa na hatia, hatua gani zitachukuliwa dhidi ya Chiligati na Nape waliosambaza tuhuma hizo.
Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa kuwa hoja ya kumng'oa Kikwete ilikuwa ikiungwa mkono kichini chini na vigogo wengi ambao hapo awali walikuwa wakidaiwa kumuunga mkono Rais Kikwete.
Vigogo hao inadaiwa hivi sasa wamekuwa wakikerwa na jinsi Rais Kikwete anavyoyashughulikia matatizo ya chama hicho kwa kuendekeza siasa za makundi yanayohasimiana.
Baadhi ya wajumbe wa NEC, wamelidokeza Tanzania Daima kuwa kama Rais Kikwete hatajirekebisha kwa jinsi anavyoshughulikia matatizo ya chama tishio la kung'olewa kwenye unyekiti wa chama hicho litaendelea kumuandamana.
Waliongeza kuwa kwa hali ilivyokuwa ndani ya kikao hicho, Lowassa anaonekana kuwa bado ni tishio kwa vigogo wanaotajwa tajwa kuwania urais mwaka 2015.
Walibainisha kuwa licha ya kuwepo mikakati ya kutaka kiongozi huyo asipate fursa ya kujenga mtandao wa kumsaidia kuingia ikulu, Lowassa anaonekana kuwa imara zaidi kukabiliana na wapinzani wake.
Kabla ya NEC
Awali kulikuwa na tetesi kuwa Rais Kikwete alipokea pendekezo ya kuwang'oa madarakani baadhi ya viongozi wa chama hicho wanaodaiwa kuwa ndio chanzo cha mitafaruku ndani ya CCM.
Miongoni mwa waliokuwa wakisemwa kung'olewa madarakani ni Lowassa, Sitta, Nape, Chiligati na Chenge.
Inadaiwa kuwa baadhi ya makada wa chama hicho walikodishiwa usafiri kutoka kwenye maeneo yao na kulipwa posho ili kwenda kushangilia Lowassa, Chenge na wengineo wanavulia madaraka.
Kundi jingine nalo linadaiwa kupelekwa mkoani Dodoma kwa lengo la kushangilia kung'olewa kwa Sitta, Nape na Chiligati.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaweka wazi kuwa uamuzi wa CCM kulirejesha suala la kujivua gamba kwa kamati kuu ambayo italipeleka suala hilo kwenye kamati ya maadili kutafutiwa ufumbuzi kutazidisha mtafaruku ndani ya chama hicho.
Wameweka wazi kuwa hivi sasa mpasuko utakuwa zaidi ndani ya chama hicho hasa baada ya taarifa kuwa Chiligati na Nape walikuwa wakiwashambulia makada wenzao tofauti na maagizo ya kikao cha NEC kilichofanyika Aprili mwaka huu. Wamedokeza kuwa sasa makundi hasimu yatajiimarisha ili kuhakikisha makada wanaowaunga mkono hawapati adhabu pindi itakapobainika wamekwenda kinyume na maadili ya chama hicho.