unapounganisha vitu viwili kinatokea kitu kimoja! Huu ndo muungano lakini unapounganisha vitu viwili na vikaendelea kuwa viwili basi kuna kasoro! Maana yake ni kuwa kuna kiunganishi ambacho ama kimeua asili yake na kuvaa asili mpya ama kumekumbatia asili mbili! Kwa maana nyingine lazima muungano huo utasababisa kimoja kupooza na kingine kuwa na nguvu. Ili kuondoa dhoofu hiyo tunashauri kuwa kila kiunganishi kiwe na uhalisi wake baada ya hapo kuwepo na ushirikiano tu. Ushirikiano huu tutakaoubatiza muungano utakuwa wa kushirikiana baadhi ya mambo fulanifulani na sii yote. Sioni hofu inatoka wapi! Kimsingi ukiangalia waziri mkuu hafanyi mambo ya muungano wa tanzania. Ukichunguza kwa makini utajua tu kuwa kuna nchi iliyofichika ambayo tunawafumba watu macho kwa lazima ili waamini hivyo! Huu sio ukweli!
Hivi kiukweli neno tanganyika lilikwenda wapi? Kumbuka mkataa kwao mtumwa! Kwa nini tanganyika ife?
Asante mh ali mohamed kessy kwa kuliona hili.