mbari
JF-Expert Member
- Nov 2, 2014
- 509
- 421
UNAMJUA MIGUNA WA NCHINI KENYA
Aligombea Ugavana wa Jiji la Nairobi huko Kenya na akapata kura zaidi ya elfu tisa. Baadae akajitangaza kama Jenerali wa vuguvugu la kuipinga Serikali ya Kenya kupitia Chama kiitwacho (NRM) National Resistance Movement of Kenya.
Ndiye aliyemuapisha Raila Odinga kuwa Rais wa Watu wa Kenya. Kesho yake baada ya kiapo cha Raila Odinga akatangaza Picha zote za Uhuru Kenyatta zishushwe popote zilipo na akapanga kuzichoma moto hadharani.
Usiku wa siku hiyo hiyo, Polisi wakazingira Nyumbani kwake na silaha nzito, wakavunja mlango kwa kuulipua na wakamkamata.
Badala ya kumpeleka Kituo cha Polisi cha kilichopo jirani wakamsafirisha usiku huo huo na kumpeleka Mikoani yaani ni kama wamtoe Dar Es Salaam wampeleke Dodoma halafu wakatae kumpeleka Mahakamani.
Sio hilo tu, pia wakazuia mtu yeyote asimuone wala kuongea naye licha ya Mahakama kutaka afikishwe Mahakamani, mpaka pale Jaji alipotoa Amri kwa Mkuu wa Polisi na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai ndipo wakampeleka Mahakamani wenyewe.
Badala ya kumpeleka mfano Mahakama ya Dar Es Salaam alikotakiwa kupelekwa kwa mujibu wa order ya Mahakama, wakampeleka mfano Mahakama ya Serengeti Mkoani Mara.
Mahakama ya Serengeti ikasema, mrudisheni huyu Miguna Mahakama Kuu ya Dar Es Salaam, kabla hajapelekwa huko, Mahakama kwa mujibu wa malalamiko mengine ya waleta maombi, ikatoa uamuzi aachiwe kwa dhamana ya elfu hamsini.
Polisi badala ya kumuachia Miguna kwa dhamana ili kutii order ya Mahakama, waliendelea kukaidi order hiyo ya Mahakama na usiku wa kuamkia leo inasemekana Miguna amesafirishwa kwa ndege ya Serikali kupelekwa nchini Canada, nchi ambayo ana uraia pacha pia.
Binafsi najiuliza, Miguna alikamatwa na Polisi kwa sababu za makosa ya kijinai au Miguna alikamatwa na watu wa Idara ya Uhamiaji kwa sababu ya kuwa na uraia pacha wa Canada?
Bado najiuliza, Polisi na Dola ya Kenya wanamhofia huyu Miguna kuliko Raila Odinga aliyemuapisha. Huyo (pichani) ndiye Miguna Miguna wa (NRM) National Resistance Movement Of Kenya anayemuunga mkono Rais wa Watu wa Kenya Raila Odinga.
Aligombea Ugavana wa Jiji la Nairobi huko Kenya na akapata kura zaidi ya elfu tisa. Baadae akajitangaza kama Jenerali wa vuguvugu la kuipinga Serikali ya Kenya kupitia Chama kiitwacho (NRM) National Resistance Movement of Kenya.
Ndiye aliyemuapisha Raila Odinga kuwa Rais wa Watu wa Kenya. Kesho yake baada ya kiapo cha Raila Odinga akatangaza Picha zote za Uhuru Kenyatta zishushwe popote zilipo na akapanga kuzichoma moto hadharani.
Usiku wa siku hiyo hiyo, Polisi wakazingira Nyumbani kwake na silaha nzito, wakavunja mlango kwa kuulipua na wakamkamata.
Badala ya kumpeleka Kituo cha Polisi cha kilichopo jirani wakamsafirisha usiku huo huo na kumpeleka Mikoani yaani ni kama wamtoe Dar Es Salaam wampeleke Dodoma halafu wakatae kumpeleka Mahakamani.
Sio hilo tu, pia wakazuia mtu yeyote asimuone wala kuongea naye licha ya Mahakama kutaka afikishwe Mahakamani, mpaka pale Jaji alipotoa Amri kwa Mkuu wa Polisi na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai ndipo wakampeleka Mahakamani wenyewe.
Badala ya kumpeleka mfano Mahakama ya Dar Es Salaam alikotakiwa kupelekwa kwa mujibu wa order ya Mahakama, wakampeleka mfano Mahakama ya Serengeti Mkoani Mara.
Mahakama ya Serengeti ikasema, mrudisheni huyu Miguna Mahakama Kuu ya Dar Es Salaam, kabla hajapelekwa huko, Mahakama kwa mujibu wa malalamiko mengine ya waleta maombi, ikatoa uamuzi aachiwe kwa dhamana ya elfu hamsini.
Polisi badala ya kumuachia Miguna kwa dhamana ili kutii order ya Mahakama, waliendelea kukaidi order hiyo ya Mahakama na usiku wa kuamkia leo inasemekana Miguna amesafirishwa kwa ndege ya Serikali kupelekwa nchini Canada, nchi ambayo ana uraia pacha pia.
Binafsi najiuliza, Miguna alikamatwa na Polisi kwa sababu za makosa ya kijinai au Miguna alikamatwa na watu wa Idara ya Uhamiaji kwa sababu ya kuwa na uraia pacha wa Canada?
Bado najiuliza, Polisi na Dola ya Kenya wanamhofia huyu Miguna kuliko Raila Odinga aliyemuapisha. Huyo (pichani) ndiye Miguna Miguna wa (NRM) National Resistance Movement Of Kenya anayemuunga mkono Rais wa Watu wa Kenya Raila Odinga.