Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Dr. Ian McCormack ni daktari aliyefufuka baada ya kufa kwa masaa kadhaa. Daktari huyu alikuwa anapenda maisha ya anasa na kuogelea. Siku moja alipokuwa akiogelea baharini, aling’atwa na mdudu mwenye sumu kali. Alilazwa hospitalini, madaktari wakajitahidi kuokoa maisha yake lakini haikuwezekana. Akafa.
Kwa mujibu wa taaluma ya udaktari, mtu anahesabika amekufa endapo anatimiza vigezo vifuatavyo (hasa katika mazingira ya hospitali):
Baada ya kufufuka, Dr. Ian alishuhudia kwamba alionyeshwa kuzimu na baadaye akaonyeshwa mbinguni. Kwa neema ya Mungu, alipewa nafasi ya kuwa hai tena. Baada ya tukio hilo, maisha yake yalibadilika kabisa. Aliacha maisha ya dhambi, akatubu na kumwamini Yesu. Ushuhuda wake ulirekodiwa na Televisheni maarufu(TBN).
Leo hii Dr. Ian anahubiri Injili katika nchi nyingi duniani. Anapohubiri, anasisitiza juu ya wokovu unaopatikana kwa neema kwa njia ya Yesu Kristo, na kwamba alionja rehema ya Mungu ya kuendelea kuishi baada ya kufa. Wanaosema hakuna mbingu, mtafuteni Dr. Ian atawashuhudia zaidi.
Kwa mujibu wa taaluma ya udaktari, mtu anahesabika amekufa endapo anatimiza vigezo vifuatavyo (hasa katika mazingira ya hospitali):
- Hana mapigo ya moyo (cardiac arrest).
- Hapumui (respiratory arrest).
- Pupils hazijibu mwanga (fixed and dilated).
- Mwili wake unakuwa baridi au mwepesi. Hii mara nyingi hutokea ndani ya dakika chache baada ya moyo kusimama.
Baada ya kufufuka, Dr. Ian alishuhudia kwamba alionyeshwa kuzimu na baadaye akaonyeshwa mbinguni. Kwa neema ya Mungu, alipewa nafasi ya kuwa hai tena. Baada ya tukio hilo, maisha yake yalibadilika kabisa. Aliacha maisha ya dhambi, akatubu na kumwamini Yesu. Ushuhuda wake ulirekodiwa na Televisheni maarufu(TBN).
Leo hii Dr. Ian anahubiri Injili katika nchi nyingi duniani. Anapohubiri, anasisitiza juu ya wokovu unaopatikana kwa neema kwa njia ya Yesu Kristo, na kwamba alionja rehema ya Mungu ya kuendelea kuishi baada ya kufa. Wanaosema hakuna mbingu, mtafuteni Dr. Ian atawashuhudia zaidi.