Songambele
JF-Expert Member
- Nov 20, 2007
- 4,725
- 2,606
Du pole sana inaonekana ulianza hii mada bila tafiti ya kutosha kuhusu kahama, kwanza kahama ni Hub ya biashara inaunganisha Shinyanga, Mwanza, Kagera, Geita, Kigoma, Tabora, Rwanda na Burundi. Soko kubwa hapa ni watu by then katika halmashauri zilizokuwa zinaongoza kwa mapato ilikuwa Ilala, Makambako na Kahama. Mji huu ni maarufu kwa uchimbaji wa dhahabu. Pia ni mji wa pili kwa mapato kati ya halmashauri za wilaya, ikitanguliwa na Kinondoni na kufuatiwa na Mufindi.Watanzania kuna nyakati tuambizane ukweli, mji kama Kahama ukitoa ule mgodi wa Buzwagi nini kinabaki pale Kahama? Kuna raia humu watataja car wash, guest house, bajaji, frame, saloon, maduka ya nguo na kadhalika, na sio Kahama tu nenda Geita then ondoa ule mgodi hakuna kinacho bakia pale Geita, kwamba ni kitu strong kwa uchumi. Kahama kidogo sana vile viwanda vya mpunga vile ndio unaweza sema kuna kitu pale ila sio zile hoteli na frame.
Hii iko kwenye miji mingi nchi hii, uwekezaji mwingi ni wa vitu kama hotel, car wash, frame na maduka ya nguo. Je, hizi tunaweza shindanisha na biashara za wachina?
Buzwagi ni mgodi mdogo na ulifungwa kitambo, Kuna Giant Kahama Mining (Bulyanhulu) Kakola huko. Wilaya ya Kahama imevunjwa na kupatikana Msalala, Kahama na Ushetu. Vile viwanda na stores mpunga usizipuuzie hata kidogo pale unachakatwa mpunga kutoka Tabora, Kigoma, mpanda, Sumbawanga na Mbeya. Sekta hiyo imeajiri watu wengi na kuuza mchele mwingi Moshi, Arusha, Nairobi, Kigali, Kampala mpaka Sudan.
Hotel zilikuwepo kabla ya huo mgodi, wachimbaji wadogo wako wengi mno kahama kuliko sehemu yeyote TZ kama sio Afrika, Hata bus za kwenda mbali zinalalia huko