Mjadala: Magari ya viongozi wetu na dhana ya kubana matumizi

Ubumuntu

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
14,316
10,782
Salaam,

Kama kichwa kinavyojieleza. Kumekuwa na mjadala wa miaka mingi juu ya aina ya magari ambayo viongozi wetu wa kiserikali wanayatumia kwa shughuli zao za kila siku.

Binafsi, nimekuwa nikisema mara kwa mara kwamba viongozi wetu wanaishi kama mastaa wa Hollywood kupitia migongo yetu walipa kodi.

Sasa baada ya kuona namna Rais mpya wa Ufaransa alivyo walk the talk, nikaona ni vyema tuendeleze huu mjadala. Angalia picha nilizoambatanisha hapa. Na pengine tuzidi kuishauri serikali ya Magufuli, ambayo inasisitiza katika dhana ya kubana matumizi.

IMG_5080.JPG


Sina takwimu halisi ya namna gani magari ya viongozi yanaligharimu taifa, ila kwa kutumia uzoefu na common sense, ni rahisi kusema magari hayo yanaligharimu taifa pesa nyingi bila sababu za msingi.

Kuna ulazima gani wa Rais kutumia magari ya kifahari ya aina ya BMW? Katika msafara wake kuna BMW 7 series na BMW X5.
Kuna ulazima gani kwa VP kutumia Mercedes Benz GL Class? Kuna ulazima gani kwa PM na Spika kutumia Mercedes Benz S Class? Kuna ulazima gani kwa mawaziri, manaibu waziri, wakurugenzi, wakuu wa vyuo vya umma, wakuu wa polisi wa wilaya na mikoa, RCs, DC n.k. kutumia Land Cruisers 200 aidha VX au GX?

Hizi gari pamoja na bei ya kununua kuwa aghali, vilevile matunzo yake na utumiaji wa mafuta unaligharimu taifa fedha nyingi.

Kuna kipindi PM Pinda alitoa mwongozo juu ya aina ya magari kwa viongozi. Nakumbuka hadi Waziri Lukuvi akasema viongozi wataanza kutumia Suzuki Grand Vitara ama Toyota Rav4. Vilevile huyu bwana mkubwa wa sasa kwenye kampeni aliongelea juu ya haya magari ya viongozi. Ila bado mambo ni yale yale.

Kwanini inawawia vigumu kwa hawa viongozi kuamua kufanya angalau kama walivyojaribu Kenya kwa mawaziri kuanza kutumia VW Passat? Ingawa sijui kama utaratibu huo bado upo sasa. Hivi Rais akiendeshwa kwenye VW Passat kuna shida gani? Licha ya kujisifu kwamba serikali ya CCM imejenga mabarabara kila kona ya nchi, kwanini bado Land Cruisers zinatumika?

IMG_5081.JPG


Kwa upana zaidi: hivi kuna ulazima wa viongozi wa serikali (pengine ukitoa wakuu wa mihimili ya dola) kupewa magari ya kutumia 24/7?

Ni hayo tu.
 
Hap mkuu sio suala la kununua tu. Ukichukulia mfano ufaransa kila Rais ambaye amekuwepo amekuwa na choice ya gari gani (BRAND)atatumia kulinga na upenzi au ushabiki wakehapo ghalama haihusiki. KWa Rais lazima atumie gari secured mkuu bila kujali Ghalama. Maisha yake yanathamani kuliko Chombo anachotembelea kwa sababu anawakilisha watu zaidi ya mi 50.

Pia. Wapinzani ambao ndio Kipaumbele chao wangekuwa wa kwanza Kuweka pembeni maVX ili kuonyesha wanamaanisha wanachokisema. Mtu anamiliki HAMMER, au Mtu anasema akiingia madarakani atauza Mashangingi wakati hata tunavyoongea nyumbani kwake amepaki hayo hayo mashangingi mtu huyo inatia shaka kumwamini.

Ni kweli Hao wabunge na watumishi wengi wa serikali wanatumia magari ya anasa saana. Kabla ya kukimbilia kuayauza waangalie ni mbadala gani ambao ni cost effective bila kucompromise Usalama in case kuna ajali, Ubora,Uwezo wake kwenye barabara zisizorafiki etc. Unakumbuka CASE ya NAPE NAUYE Kama ingekuwa ni NADIA au NOAH asingetoka mule.
 
Mkuu hicho kichwa cha habari kimenikumbusha dereva wa mkurugenzi anayelala na gari la serikali tabata aamke nalo asubuhi kumchukua boss bunju ili ampeleke kazini posta.

Kwetu kuna mambo huwa sijui kwanini hayaingizwi kwenye vitabu vya Guiness.
 
Hap mkuu sio suala la kununua tu. Ukichukulia mfano ufaransa kila Rais ambaye amekuwepo amekuwa na choice ya gari gani (BRAND)atatumia kulinga na upenzi au ushabiki wake. KWa Rais lazima atumie gari secured mkuu bila kujali Ghalama. Maisha yake yanathamani kuliko Chombo anachotembelea kwa sababu anawakilisha watu zaidi ya mi 50.

Najua kinga ni bora kuliko tiba. But, seriously kati ya Rais wa Ufaransa na wa Tanzania nani anayehitaji hilo secured car? Rais Magufuli anaogopa nini? Vipi kuhusu marais wa nchi kadhaa Ulaya ambao wanatumia tu public commuter trains?

Pia. Wapinzani ambao ndio Kipaumbele chao wangekuwa wa kwanza Kuweka pembeni maVX ili kuonyesha wanamaanisha wanachokisema. Mtu anamiliki HAMMER, au Mtu anasema akiingia madarakani atauza Mashangingi wakati hata tunavyoongea nyumbani kwake amepaki hayo hayo mashangingi mtu huyo inatia shaka kumwamini.

Mimi naongelea kuhusu matumizi ya kodi na pesa za umma. Sijali kama kiongozi hata akinunua Maserati kwa pesa zake. Hiyo ni mipango yake, ili mradi tu pesa kazipata kihalali.

Ni kweli Hao wabunge na watumishi wengi wa serikali wanatumia magari ya anasa saana. Kabla ya kukibilia kuayauza waangalie ni mbadala gani ambao ni cost effective bila kucompromise Usalama in case kuna ajali, Ubora,Uwezo wake kwenye barabara zisizorafiki etc.
Naona una overplay umuhimu wa usalama hapa. Pengine ufafanue usalama gani unauongelea na una husika vipi na gari? Je, kwa Macron kutumia hiyo Peugeot Citroen DS ali-comprise usalama wake?
 
Najua kinga ni bora kuliko tiba. But, seriously kati ya Rais wa Ufaransa na wa Tanzania nani anayehitaji hilo secured car? Rais Magufuli anaogopa nini? Vipi kuhusu marais wa nchi kadhaa Ulaya ambao wanatumia tu public commuter trains?
Kuna watu hizo ndio kazi zao na wameona umuhimu wa kufanya hivyo kulingana na risk analysis zao sio sisi mashabiki mitandaoni. Kitu ambacho hujasema hiyo Peugeot Citroen DS imekuwa customized to meet presidential specifications. Ndio maana Orginal Version haina sehemu ya Kufunguka juu na kusimama.Gharama yake kwa matumizi ya kawaida lazima iwe inatofauti na baada ya customization.

Naona una overplay umuhimu wa usalama hapa. Pengine ufafanue usalama gani unauongelea na una husika vipi na gari? Je, kwa Macron kutumia hiyo Peugeot Citroen DS ali-comprise usalama wake?
Ukienda migodini au watu wa Tafiti wanatumia Landcruser mkonga au navara kulingana na complexity ya maeneo yao ya kazi. Sasa kabla hatujashauri ni aina gani ya gali iwe mbadala wa VX ni vizuri pia kujua Mahitaji ya anaetakiwa kuitumia, Moja Atapita wapi, Barabara ya Vijijini zinaisupport Ref Mkuu wa wilaya Ngara kwenye operation porini. Je incase ya ajali ni Secured zaidi Ref ajali ya Nape. Hapo tutaweza kuja na Proporsal au wazo zuri la gari gani ni mbadala wa VX.
Sijui sana mambo ya magari, Kuna mjadala humu tujiwahi kujadili wiki chache zimepita nilidhani Zile deffender au Landcruiser mkonga ni mbadala tosha. Wataalamu wa hayo mambo wakachambua na kuonyesha ni gharama kuliko Vx.
Kwa vyovyote vile kama kuna alternative ya VX ambayo itakidhi mahitaji ni mtu mwenye matatizo ndiye atakayekupinga...
 
Kwanza hujazingatia utofauti wa mazingira Kati ya Ulaya na Africa (TZ). Huwezi kutembelea starlet utegemee ikufikishe jimboni kwako Ileje ndani kule. Haiwezakani

Viongozi wetu hawawezi kutumia public transportation kwa sababu zile zile za utofauti uliopo wa kimazingira na miundombinu Kati ya Ulaya na TZ.

Hao Ulaya kama hapo France wanatumia hayo magari sababu miundombinu inaruhusu na wengi wanatumia sababu ni brands za nchini mwao. Na wengi wanayatumia kwa mwendo mfupi tu wakienda mbali Kidogo tu wanaruka. Unataka tufanye hivyo kwamba Rais Dar to Bagamoyo aruke ili awaridhishe kwa kutumia vitz awapo mjini.

I fully sapoti viongozi kutumia lc200 au watumie range Rover kabisa zipo njema on and off road.
 
Kabla ya kukimbilia kuayauza waangalie ni mbadala gani ambao ni cost effective bila kucompromise Usalama in case kuna ajali, Ubora,Uwezo wake kwenye barabara zisizorafiki etc. Unakumbuka CASE ya NAPE NAUYE Kama ingekuwa ni NADIA au NOAH asingetoka mule.

Mbona solution ni ndogo tu hapo. Uingereza wana mfumo wa government car pool. Kiongozi atatumia gari kwa kuikodi kwa utaratibu wa muda au/na umbali. Hivyo kunakuwa hakuna haja ya kiongozi kusafiri na gari ya serikali kutoka London kwenda Newcastle. Ataenda kwa public transport, kisha akifika Newcastle atakodi gari kutoka government car pool na kulitumia akiwa hapo. Akimaliza anarudi zake London kwa train.

Serikali inajitapa kuwekeza katika ujenzi wa barabara inashindwa nini kutumia mfumo huo? Waziri akipanda basi atakuwa siyo waziri? Sasa kwa viongozi kupata hizo privileges, hawawezi kuisukuma serikali katika kuwekeza kwenye public transport iliyo bora kabisa. Ni sawa na viongozi kupeleka watoto wao kwenye private schools na siyo public schools, na incentives za ku-push for excellence kwenye public education.
 
Mbona solution ni ndogo tu hapo. Uingereza wana mfumo wa government car pool. Kiongozi atatumia gari kwa kuikodi kwa utaratibu wa muda au/na umbali. Hivyo kunakuwa hakuna haja ya kiongozi kusafiri na gari ya serikali kutoka London kwenda Newcastle. Ataenda kwa public transport, kisha akifika Newcastle atakodi gari kutoka government car pool na kulitumia akiwa hapo. Akimaliza anarudi zake London kwa train.

Serikali inajitapa kuwekeza katika ujenzi wa barabara inashindwa nini kutumia mfumo huo? Waziri akipanda basi atakuwa siyo waziri? Sasa kwa viongozi kupata hizo privileges, hawawezi kuisukuma serikali katika kuwekeza kwenye public transport iliyo bora kabisa. Ni sawa na viongozi kupeleka watoto wao kwenye private schools na siyo public schools, na incentives za ku-push for excellence kwenye public education.
proxy

Zungumzia tanzania.
Barabara tunazojisifia zinakidhi mahitaji kwa asilimia chini ya 50.
asilimia kubwa ya sehemu muhimu leo haziendeki hadi kiangazi kianze.
KUJITAPA ubora wa barabara KULNGINISHA NA wakati uliopita sio KUlinganisha na LONDON mkuu
111332.jpg

HAPO VITS LABDA UIBEBE. Suggest right altenative mkuu. Hakuna anependa kuyaona haya magari ya gharama kama yana mbadala wenye kukidhi mahitaji
 
Back
Top Bottom