Miungano yenye nguvu thabiti na ushawishi zaidi duniani

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,634
46,276
1. Umoja wa Ulaya (EU)
Huu ndio mfano wa umoja wa nchi bora zaidi kuwahi kutokea duniani. Wana pesa yao yenye nguvu na heshima duniani. Wana vigezo thabiti vya kujiunga na umoja huo, hakuna vikwazo vya kusafiri na kufanya kazi/biashara. Kinachovutia zaidi ni nchi haiwi mwanachama tu kwa sababu iko Ulaya, Uturuki na nchi nyingine zimejaribu mara kadhaa kujiunga ila zimegonga mwamba.

2. NAFTA/USMCA
Umoja wa kiuchumi wa nchi tatu za Marekani, Canada na Mexico umerahisisha na kukuza biashara kati ya mataifa hayo kwa muda mrefu huku kila mmoja akifaidika nao.

3. OPEC
Umoja wa nchi zinazozalisha mafuta kwa wingi duniani uko imara sana. Huenda sababu kubwa ajenda yao kubwa huwa ni moja tu, kuhakikisha bei ya mafuta inakuwa na faida kwao. Wakikutana ujue ni kicheko au kilio kwa watumiaji wa mafuta duniani na wakiamua jambo lao hakuna anayefanya udanganyifu au usaliti.

4. NATO
Huu ndio umoja imara zaidi katika kulinda maslahi ya ulinzi ya wanachama wake. Article 5 ya katiba ya Umoja huo imeweka comittement ya juu zaidi ya wanachama kwamba shambuli kwa mwanachama mmoja ni shambuliz kwa wote.

5. G7
Club ya nchi tajiri na zenye maendeleo makubwa zaidi ya viwanda(US, Canada, UK, Ufaransa, Japan, Ujerumani, Italia na EU kama mualikwa) ni ushirikiano wa mataifa saba tajiri kiviwanda na yenye mrengo mmoja hasa unaohusu "Western values". Wakiamua jambo linalohusu fedha huwa hawashindwi kitu au kurudi nyuma.

6. FIFA

Shirikisho la mpira duniani ni umoja imara sana. Wanachama wake wana nidhamu kwa kila kitu, iwe jambo lenye manufaa au vinginevyo. Viongozi na kamati zake zikishaamua jambo hakuna mwanachama anaweza kukengeuka.

Kimkakati kabisa waliweka kanuni ya mambo yanaohusu mpira kutopelekwa mahakamani ili wawe na utawala wao na mambo yote yaishie katika vyombo vyaka.
 
#4
20230411_222939.jpg
 
1. Umoja wa Ulaya (EU)
Huu ndio mfano wa umoja wa nchi bora zaidi kuwahi kutokea duniani. Wana pesa yao yenye nguvu na heshima duniani. Wana vigezo thabiti vya kujiunga na umoja huo, hakuna vikwazo vya kusafiri na kufanya kazi/biashara. Kinachovutia zaidi ni nchi haiwi mwanachama tu kwa sababu iko Ulaya, Uturuki na nchi nyingine zimejaribu mara kadhaa kujiunga ila zimegonga mwamba.
Ni sababu gani zilipelekea Uingereza kujitoa EU ?
 
CCM huu ni muungano wa Tanu na ASP huu Muungano umedumu miaka 40 + sasa,na hautegemewi kuvunjika.
Unaona sababu ni nini zimelepekea huo muunganiko kudumu muda mrefu hadi sasa ? Na mpaka miaka hiyo ijayo ?
 
Una maanisha nyie Watanzania mnaipenda CCM ?
Binafsi hapana,ila ninakumbuka nilipokuwa shule ya msingi miaka ya tisini katikati hapo tulikuwa tunaimbishwa naapa naahidi mbele ya chama mapinduzi nitakulinda mpaka kufa. Yaani ideology ya chama cha mapinduzi ndo chama tulipandikizwa tangu utotoni, na hata vyama vingi vilipokuja tuliambiwa vyama vingi vitaleta vita.
 
Binafsi hapana,ila ninakumbuka nilipokuwa shule ya msingi miaka ya tisini katikati hapo tulikuwa tunaimbishwa naapa naahidi mbele ya chama mapinduzi nitakulinda mpaka kufa. Yaani ideology ya chama cha mapinduzi ndo chama tulipandikizwa tangu utotoni, na hata vyama vingi vilipokuja tuliambiwa vyama vingi vitaleta vita.
Ok
 
Ni sababu gani zilipelekea Uingereza kujitoa EU ?
Sababu kuu ni suala la Uhamiaji. Uingereza ilikuwa inapinga sera za umoja wa ulaya wa kuwakaribisha wahamiaji hasa kutoka Afrika na Afghanstan, Syria, Yemen sera ambayo iliongozwa na Kansela Angela Merkel wa Ujeruman. Zaidi ya wahamiaji Milioni 6 waliingia nchi za Ulaya hasa Italia, Ujeruman na Ugriki. Uingereza ikaona huu uhuni dawa yake ni kujitoa.
 
1. Umoja wa Ulaya (EU)
Huu ndio mfano wa umoja wa nchi bora zaidi kuwahi kutokea duniani. Wana pesa yao yenye nguvu na heshima duniani. Wana vigezo thabiti vya kujiunga na umoja huo, hakuna vikwazo vya kusafiri na kufanya kazi/biashara. Kinachovutia zaidi ni nchi haiwi mwanachama tu kwa sababu iko Ulaya, Uturuki na nchi nyingine zimejaribu mara kadhaa kujiunga ila zimegonga mwamba.

2. NAFTA/USMCA
Umoja wa kiuchumi wa nchi tatu za Marekani, Canada na Mexico umerahisisha na kukuza biashara kati ya mataifa hayo kwa muda mrefu huku kila mmoja akifaidika nao.

3. OPEC
Umoja wa nchi zinazozalisha mafuta kwa wingi duniani uko imara sana. Huenda sababu kubwa ajenda yao kubwa huwa ni moja tu, kuhakikisha bei ya mafuta inakuwa na faida kwao. Wakikutana ujue ni kicheko au kilio kwa watumiaji wa mafuta duniani na wakiamua jambo lao hakuna anayefanya udanganyifu au usaliti.

4. NATO
Huu ndio umoja imara zaidi katika kulinda maslahi ya ulinzi ya wanachama wake. Article 5 ya katiba ya Umoja huo imeweka comittement ya juu zaidi ya wanachama kwamba shambuli kwa mwanachama mmoja ni shambuliz kwa wote.

5. G7
Club ya nchi tajiri na zenye maendeleo makubwa zaidi ya viwanda(US, Canada, UK, Ufaransa, Japan, Ujerumani, Italia na EU kama mualikwa) ni ushirikiano wa mataifa saba tajiri kiviwanda na yenye mrengo mmoja hasa unaohusu "Western values". Wakiamua jambo linalohusu fedha huwa hawashindwi kitu au kurudi nyuma.

6. FIFA
Shirikisho la mpira duniani ni umoja imara sana. Wanachama wake wana nidhamu kwa kila kitu, iwe jambo lenye manufaa au vinginevyo. Viongozi na kamati zake zikishaamua jambo hakuna mwanachama anaweza kukengeuka.

Kimkakati kabisa waliweka kanuni ya mambo yanaohusu mpira kutopelekwa mahakamani ili wawe na utawala wao na mambo yote yaishie katika vyombo vyaka.
Muungano wa USA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom