SEHEMU YA II
Mara zote wabunge waliokwmisha suala la tume huru ya uchaguzi ni CCM
Walifanya hivyo wakijua muundo wa sasa ambapo wana serikali, ingekuwa vema tume ibaki ilivyo
Wapinzani pamoja na jitihada zao, wakakubali kwenda katika uchaguzi bila kujifunza kutoka chaguzi za nyuma
Hili ni kosa, kwasababu tayari walikuwa na nguvu kubwa kutoka katika jamii iliyotaka kuona haki ikitendwa
Uchaguzi ukatangazwa na kampeni kuanza. Kkumekuwepo na hali zilizotia shaka juu ya integrity na credibility ya ya uchaguzi.
Mathalan lilipotokea tatizo upande mmoja tume ilikemea, kwa upande mwingine tume ilikaa kimya
Hali ikapelekea baadhi ya vyama kuanza kutangaza matokeo na asilimia za ushindi.
Kisheria hilo ni kosa, na hatujui kwanini Tume ya uchaguzi haikuliona kama kosa?
Fursa za kampeni kwa kutumia vyombo vya habari zilitia shaka sana.
Kwamba, mamlaka husika zenye udau na tume ya uchaguzi zilikaa kimya pale upendeleo ulipoonekana wazi
Matumizi mabaya ya vyombo vya umma ilikuwa kawaida
Hali iliyozidisha mashaka ni pale zilizpokuwepo habari za kuashiri hujuma kama uwepo wa kura na maboksi feki
Inawezekana ilikuwa ni uvumi, Tume ilikuwa na wajibu wa kuwaondoa wananchi wasi wasi, mengi yalipita kimya kimya
Kwa mfano, mwenyekiti wa NCCR amedai kukamata masanduku feki na kuyafikisha Polisi
Siku iliyofuata ushahidi ukwa umepotea kwa mujibu wake.
Hilo ni jambo zito katika kuaminika kwa uchaguzi. Tulitegemea Tume ilitolee kauli!
Kutangazwa kwa matokeo
Hapa ndipo palipo na sintofahamu. Kazi ya tume kama ilivyosema ni kujumlisha kura.
Hilo si jambo la siri kwasababu tayari zilishapigwa na kutangazwa vituoni.
Hakukuwa na tatizo kwa vyama vya siasa kujiridhisha kwa matokeo yaliyotolewa. Inafanyika duniani kote.
Hoja hapa ni kuwa kujumlisha kura hakubadili matokeo wala kuiondolea Tume nguvu ya kutangaza matokeo hayo
Zaidi inajenga imani na utaratibu mzima. Nakala kutoka kwa mawala zipo, iweje kuwe na sita sita kutoka Tume
Utangazaji wa matokeo ungefanyika kwa wakati mmoja. Kwamba, Tume imekamilisha zoezi ambalo halikutarajiwa kuchukua muda kutokana na kuimarika kwa mawasiliano nchini.
Hata ilipobidi kutangaza, ilitakiwa kusiwe na hofu, shaka au walakini.
Matokeo yakatolewa kidogo kidogo( Rejea uzi huu)
https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=860405.... yakianzia pembezoni
Maeneo yote yalioonekana kuwa na hali 'isiyopendeza' yakawekwa viporo
Tulitegemea utaratibu huo wa reja reja uendelee hadi mwisho
MATOKEO
Ghafla Tume ikawa imekamilisha matokeo na kutangaza mshindi. Matokeo yaliyopatikana siku moja kwa ujumla!
Palipokuwa na matatizo , Tume haikuwa na nafasi ya kujibu, kufafanua au kueleza matatizo yaliyoletwa mbele na vyama.
Ikiwa nakala za mawakala zipo, kipi kigumu kwa Tume kuoanisha taratkimu mbali mbali na zao ili kupata muafaka?
Hili la kuvuta muda na kisha kutangaza ghafla linaondoa kile kinachosemwa kuaminika kwa zoezi na wasimamiaji
Uchelewaji wa kutangaza matokeo ulikwenda sambamba na ule wa ZEC!
Kwanini kulikuwa na uharaka wa kutangaza matokeo baada ya kusuasua?
Inaendelea...