Wakati mwingine tunailaumu mitandao ya simu kwamba wanaiba data kumbe tatizo ni sisi.
Kama unatumia mtandao wa simu kupata huduma za data, fanya yafuatayo ili data yako isiishe upesi:
- Zima data taustani (background data) kwa apps ambazo huzitumii mara kwa mara.
- Tumia toleo la "lite" la apps kama Facebook Lite, Instagram Lite, nk.
- Epuka kuangalia video za HD au kuzipakua bila sababu ya msingi.
- Tumia Wi-Fi unapopata nafasi badala ya kutumia data ya simu kila mara.
- Zima auto-update ya apps kupitia data; badili iwe Wi-Fi tu.
- Funga auto-play ya video kwenye mitandao ya kijamii kama TikTok, Instagram, na Facebook.
- Tumia Data Saver Mode ikiwa simu yako inayo.
- Fuatilia matumizi ya data kwa kutumia mipangilio ya simu au apps za mtandao wako.