Mitandao ya simu mnaibia wateja

Mitandao ya simu mnaibia wateja

Tindo

Platinum Member
Joined
Sep 28, 2011
Posts
69,467
Reaction score
122,778
Ni dhahiri kwa sasa ukiweka bundle linaisha kwa haraka kwenye data, na sababu ni Makampuni ya simu kuibia wateja Mchezo huu umekithiri sana sasa kuelekea uchaguzi.

Ni kosa makampuni ya simu kifanya wizi wa kidola dhidi ya watumiaji
 
hapo una facebook,tiktok instagram.alafu unaweka bando la buku.hakuna maisha hapo
Ni matumizi ya kawaida tu, na hakuna kucheza clip wala nini. Ni wizi ajabu unaendelea.
 
¥∆SS wanaongoza imenilazimu nirudi Airtel
 
Yamenikuta haya juzi 1.4gb iliisha ndani ya dk 5 na sikuwa nadownload chochote. Yas endeleeni kutumixx.
Ndio hizi pesa wanazotumia kuhonga makundi mbalimbali ili kumwaga sifa kwa mama. Wanajua wengi tunatumia bila kujua ulaji halisi wa bundle zetu, hivyo wanachota pesa za watumiaji bila hofu.
 
Yamenikuta haya juzi 1.4gb iliisha ndani ya dk 5 na sikuwa nadownload chochote. Yas endeleeni kutumixx.
Airtel wamenitenda kitendo cha namna hii, Gb 1 inaisha chini ya nusu saa Kwa kuperuz jf
 
Angalia vizuri
mtandao ni 4G au 5G?
4g, na sikuanza kutumia jana au juzi. Nina ufahamu wa kutosha kuhusu mitandao. Na matumizi yangu halisi nayajua. Sijaleta hili lalamiko kwa bahati mbaya.
 
Airtel wamenitenda kitendo cha namna hii, Gb 1 inaisha chini ya nusu saa Kwa kuperuz jf
Hili jambo limeshika kasi sana, na kwakuwa watumiaji tuko kimya, wanachota bila hofu.
 
Ni dhahiri kwa sasa ukiweka bundle linaisha kwa haraka kwenye data, na sababu ni Makampuni ya simu kuibia wateja Mchezo huu umekithiri sana sasa kuelekea uchaguzi.

Ni kosa makampuni ya simu kifanya wizi wa kidola dhidi ya watumiaji
Gentleman,
ni uelewa na ufahamu mdogo tu wa vifaa vya kielectronic mnavyotumia, lakini pia uelewa mdogo kuhusu speed za internet, yaani 3g, 4g, 5g nk,

hata hivyo,
ni muhimu sana kufanya kazi kwa bidii kujiepusha na unyonge wa kiuchmi kulalamikia mambo madogo kama haya 🐒
 
Gentleman,
ni uelewa na ufahamu mdogo tu wa vifaa mnavyotumia lakini pia uelewa mdogo kuhusu speed za internet, yaani 3g, 4g, 5g nk,

hata hivyo,
ni muhimu sana kufanya kazi kwa bidii kujiepusha na unyonge wa kiuchmi kulalamikia mambo madogo kama haya 🐒
Nina ufahamu wa kutosha kuhusu speed za internet. Sibahatishi nisemacho. Hakuna ufahari wa kuibiwa na kusema hujali kisa utakuwa na fedha nyingi.
 
Wakati mwingine tunailaumu mitandao ya simu kwamba wanaiba data kumbe tatizo ni sisi.

Kama unatumia mtandao wa simu kupata huduma za data, fanya yafuatayo ili data yako isiishe upesi:
  1. Zima data taustani (background data) kwa apps ambazo huzitumii mara kwa mara.
  2. Tumia toleo la "lite" la apps kama Facebook Lite, Instagram Lite, nk.
  3. Epuka kuangalia video za HD au kuzipakua bila sababu ya msingi.
  4. Tumia Wi-Fi unapopata nafasi badala ya kutumia data ya simu kila mara.
  5. Zima auto-update ya apps kupitia data; badili iwe Wi-Fi tu.
  6. Funga auto-play ya video kwenye mitandao ya kijamii kama TikTok, Instagram, na Facebook.
  7. Tumia Data Saver Mode ikiwa simu yako inayo.
  8. Fuatilia matumizi ya data kwa kutumia mipangilio ya simu au apps za mtandao wako.
Ni dhahiri kwa sasa ukiweka bundle linaisha kwa haraka kwenye data, na sababu ni Makampuni ya simu kuibia wateja Mchezo huu umekithiri sana sasa kuelekea uchaguzi.

Ni kosa makampuni ya simu kifanya wizi wa kidola dhidi ya watumiaji
 
nimeweka bando la 500 tangu asubuh mb 245.nacheza jf,sofa.score na parimatch nimebakiza mb 150
Kuna kipindi nilikua naweka bando baada ya dakika 10 limekata nikanya research kwenye simu nkagundua kuna apps zinarun background baada ya kuziturn off mambo yakawa fresh.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Back
Top Bottom