Song of Solomon
JF-Expert Member
- Aug 5, 2021
- 2,733
- 5,490
Kujiajiri ni pale mtu anakua na wazo na kuamua kulifanyia kazi ili aweze kuongeza kipato chake yeye bnafsi bila kuambiwa au kusukumwa na mtu yeyote.
Kujiajiri Kuna husiana na kufanya shughuri ya ujasiriamali bila kupewa na mtu uifanye ni wewe unaanza kufanya ukiona inaleta faida.
Kujiajiri ni jambo linalohitaji maandalizi ya muda mrefu na kuna mambo ya msingi kuyafahamu ili kuongeza ufanisi ndo maana tunasoma ujasiriamali...
Namna ya kujiajiri
Tengeneza wazo rahisi linalo weza kutekelezeka kirahisi.....
Kama unataka kuwa mjasiliamali ni vyema ukawa umechagua eneo moja maalumu la kulitafutia ufumbuzi na ambalo rahisi kutekelezeka na pia kuwa makini na hilo jambo unalotaka kulifanyia kazi uwe na uzoefu nalo au Elimu japo hata kidogo, kwani huwezi kutibu ugonjwa usiojua hata unakaa wapi
Tambua jamii inahitaji nini kama unataka kuwa mjasiriamali ni lazima uwe na uwezo wa kuchemsha akili yako (UBUNIFU) katika kuyasoma mazingira uliyopo yanahitaji kitu gani na wewe ili uje na utatuzi wake. Lenga eneo moja ambalo unaona kweli lina uhitaji na unaweza ukaja na utatuzi wake..
Tengeneza lengo.
Kutengeneza lengo la biashara ni hatua muhimu katika hatua za kuwa mjasiriamali..... Lengo hili uliweke katika maandishi na litakusaidia katika kuwashawishi watu kukusaidia mtaji. Mara utakapokuwa umeandika lengo usikae bila kutafuta Namna ya kulitimiza
Hudhuria semina
Wewe kama unataka kuwa mjasiriamali ni lazima utenge muda wako kuhudhuria semina mbali mbali, zinazohusiana na shughuli unazotaka kuja kufanya au unazofanya.....
Jiunge na wajasiriamali
Ikiwa unataka kuwa mjasiliamali ni muhimu kutafuta eneo ambalo wajasiriamali wengi wanakutana kujadiliana,Katika mazingira kama haya utakuwa kama yai linaloatamiwa na kuku ili lije kutoa kifaranga kwa kupata mawazo chanya kwao.
Fanyia kazi hatari unayoifahamu
Sifa ya mjasiriamali wa kweli, ni yule asiyeingia kichwa kichwa kutaka kutatua tatizo pasipo kupiga hesabu za kutosha za hatari iliyopo. Mjasiriamali, kweli huwa anachukua hatari za jamii na kujibebesha yeye lengo kujifunza ili kubolesha.
Nidhamu
Kujiajiri ni ujasiriamali unaohusu faida, ukiwa mtumiaji rafu wa mapato huwezi kukua mpaka ufikie unapohitaji, na utaona kazi ngumu mno inatakiwa utulivu katika kutumia rasilimali wezeshe kwa faida ili usikate tamaa.
Nidhamu ni msingi katika ukuaji wa ujasiriamali.
Kujiajiri Kuna husiana na kufanya shughuri ya ujasiriamali bila kupewa na mtu uifanye ni wewe unaanza kufanya ukiona inaleta faida.
Kujiajiri ni jambo linalohitaji maandalizi ya muda mrefu na kuna mambo ya msingi kuyafahamu ili kuongeza ufanisi ndo maana tunasoma ujasiriamali...
Namna ya kujiajiri
Tengeneza wazo rahisi linalo weza kutekelezeka kirahisi.....
Kama unataka kuwa mjasiliamali ni vyema ukawa umechagua eneo moja maalumu la kulitafutia ufumbuzi na ambalo rahisi kutekelezeka na pia kuwa makini na hilo jambo unalotaka kulifanyia kazi uwe na uzoefu nalo au Elimu japo hata kidogo, kwani huwezi kutibu ugonjwa usiojua hata unakaa wapi
Tambua jamii inahitaji nini kama unataka kuwa mjasiriamali ni lazima uwe na uwezo wa kuchemsha akili yako (UBUNIFU) katika kuyasoma mazingira uliyopo yanahitaji kitu gani na wewe ili uje na utatuzi wake. Lenga eneo moja ambalo unaona kweli lina uhitaji na unaweza ukaja na utatuzi wake..
Tengeneza lengo.
Kutengeneza lengo la biashara ni hatua muhimu katika hatua za kuwa mjasiriamali..... Lengo hili uliweke katika maandishi na litakusaidia katika kuwashawishi watu kukusaidia mtaji. Mara utakapokuwa umeandika lengo usikae bila kutafuta Namna ya kulitimiza
Hudhuria semina
Wewe kama unataka kuwa mjasiriamali ni lazima utenge muda wako kuhudhuria semina mbali mbali, zinazohusiana na shughuli unazotaka kuja kufanya au unazofanya.....
Jiunge na wajasiriamali
Ikiwa unataka kuwa mjasiliamali ni muhimu kutafuta eneo ambalo wajasiriamali wengi wanakutana kujadiliana,Katika mazingira kama haya utakuwa kama yai linaloatamiwa na kuku ili lije kutoa kifaranga kwa kupata mawazo chanya kwao.
Fanyia kazi hatari unayoifahamu
Sifa ya mjasiriamali wa kweli, ni yule asiyeingia kichwa kichwa kutaka kutatua tatizo pasipo kupiga hesabu za kutosha za hatari iliyopo. Mjasiriamali, kweli huwa anachukua hatari za jamii na kujibebesha yeye lengo kujifunza ili kubolesha.
Nidhamu
Kujiajiri ni ujasiriamali unaohusu faida, ukiwa mtumiaji rafu wa mapato huwezi kukua mpaka ufikie unapohitaji, na utaona kazi ngumu mno inatakiwa utulivu katika kutumia rasilimali wezeshe kwa faida ili usikate tamaa.
Nidhamu ni msingi katika ukuaji wa ujasiriamali.