JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 3,177
- 7,472
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime, akihojiwa na Kituo cha UTV, leo Jumanne Oktoba 14, 2025 amesema:
“Sheria ipo wazi wanaotaka kuandamana kinyume cha Sheria watachukuliwa hatua, Jeshi la Polisi tupo imara na tupo tayari kuwalinda Watanzania wema kwa nguvu tulizojaliwa na Mwenyezi Mungu pamoja na uwezo tuliowezeshwa na Serikali ya Awamu ya Sita.
“Watakaoandamana tutawashughulikia kwa mujibu wa sheria, kama kuna changamoto ichukuliwe hatua kwa mujibu wa Sheria.
“Watanzania wasiwe na hofu yoyote ile, Serikali yao imeliwezesha Jeshi la Polisi na Vyombo vingine vya Usalama kusimamia usalama.”
“Wapiga kura wajitokeze kwa wingi kupiga kura wakimaliza warejee nyumbani, wasiwe na hofu, wanaosambaza hofu ni Wahalifu wa kwenye Mtandao, wanaeneza propaganda.
“Sisi tupo imara, pia ushirikiano tunaopata Jeshi la Polisi amani itatawala, watapiga kura na walioshinda watatangazwa.”
“Sheria ipo wazi wanaotaka kuandamana kinyume cha Sheria watachukuliwa hatua, Jeshi la Polisi tupo imara na tupo tayari kuwalinda Watanzania wema kwa nguvu tulizojaliwa na Mwenyezi Mungu pamoja na uwezo tuliowezeshwa na Serikali ya Awamu ya Sita.
“Watakaoandamana tutawashughulikia kwa mujibu wa sheria, kama kuna changamoto ichukuliwe hatua kwa mujibu wa Sheria.
“Watanzania wasiwe na hofu yoyote ile, Serikali yao imeliwezesha Jeshi la Polisi na Vyombo vingine vya Usalama kusimamia usalama.”
“Wapiga kura wajitokeze kwa wingi kupiga kura wakimaliza warejee nyumbani, wasiwe na hofu, wanaosambaza hofu ni Wahalifu wa kwenye Mtandao, wanaeneza propaganda.
“Sisi tupo imara, pia ushirikiano tunaopata Jeshi la Polisi amani itatawala, watapiga kura na walioshinda watatangazwa.”