Mlengo wa Kati
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 2,730
- 492
Malumbano kati ya viongozi wa CCM na Chadema yamendelea kupamba moto, safari hii Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, akitangaza hadharani mshahara aliodai ni wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilson Mukama, kwa madai ya kutaka kuthibitisha kuwa halipwi fedha nyingi.
Kauli ya Nape aliyoitoa jana ni juhudi za kutaka kuusadikisha umma kwamba mshahara wa bosi wake haufui dafu kwa mshahara wa Katibu Mkuu wa (Chadema), Dk. Willbroad Slaa.
Nape alisema kuwa Mukama analipwa mshahara wa Sh. milioni 1.5 na posho ya mwezi ya Sh. 300,000.
Juzi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwanasheria wa Chadema, Mabere Marando, alisema Mukama analipwa mshahara wa Sh. milioni 11 wakati Dk. Slaa analipwa Sh. milioni 7.1, hivyo CCM hawana sababu ya kushangaa mshahara wa Slaa.
Malumbano hayo ya mishahara ya viongozi wa vyama hivyo viwili yanatokana na kauli ya Nape kuwa Dk. Slaa ameshinikiza kulipwa mshahara mnono akieleza msimamo huo unakinzana na wakati akiwa mbunge alipokuwa akishinikiza malipo kwa wabunge yapunguzwe.
Nape alidai kuwa mshahara wa Dk. Slaa ni sawa na wa mbunge.
Hata hivyo, uchunguzi huru wa NIPASHE uliofanywa juu ya mishahara ya viongozi watendaji wa CCM umebaini kuwa makatibu wa CCM wa mikoa wanalipwa mishahara ya Sh. milioni moja baada ya kodi, wakati makatibu wa wilaya wanalipwa Sh. 700,000 baada ya kodi, ilahali Katibu wa UVCCM akitia kibindoni Sh. milioni 1.5.
Kwa vigezo vya mishahara hiyo, ni sawa na kusema kwamba mishahara ya makatibu wa jumuiya na pengine ya makatibu wa mikoa haitofautiani na ile ya katibu mkuu.
Vile vile jana, Nape amekanusha madai yaliyotolewa na Mwanasheria wa Chadema, Marando kwamba yeye (Nape), alikwenda kuomba agombee ubunge Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya chama hicho na wakamkatalia kwa kukosa sifa.
Akizungumza na NIPASHE jana akiwa mkoani Singida, Nape alisema Chadema ndio walimfuata na kumwomba achague jimbo la kugombea kupitia chama hicho.
Waliniambia nichague Jimbo lolote la uchaguzi Dar es Salaam nigombee isipokuwa Ubungo, lakini nikawakatalia, niliwaeleza wazi kuwa mimi kuhama CCM ni sawa na kumsilimisha Papa sasa hiyo kauli ya Marando ni uzushi wa hali ya juu, alisema Nape.
Alidai hata alipohudhuria Baraza Kuu la chama hicho walimuomba avae sare za chama hicho na kisha kumwomba ajiunge na chama hicho, lakini alikataa na hata sare alizijaribu na kuwarudishia hapo hapo.
CCM ni chama kikubwa na kinapata ruzuku kubwa kuliko Chadema, lakini angalia mshahara wa Katibu Mkuu wetu linganisha na Sh. milioni 7.5 anazolipwa Dk. Slaa, Marando ameamua kwa makusudi kuupotosha umma hivyo kama ni muungwana basi aombe radhi kwa Watanzania aliowadanganya, alisema Nape. Alisema mshahara wa Mukama unalipiwa kodi wakati wa Dk. Slaa haukatwi kodi hivyo alimshauri kwanza kujisalimisha kwa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), kulipa kodi anayodaiwa.
Kutolipa kodi ni ufisadi wa hali ya juu, lakini mtu huyu huyu ambaye halipi kodi anajifanya ana uchungu na umaskini wa Watanzania, hata pale ofisini kwake kuna watu wanalipwa mishahara midogo hata haitoshi kujikimu kwa siku kumi, kuna msemo kwamba kabla hujatoa boriti kwenye jicho la mwenzako anza kutoa kwako, alisema Nape.
Tafsiri ya fisadi kwa mujibu wa Ilani yao ni mtu anayeishi kiujanja ujanja, sasa Dk. Slaa anaishi kwa mtindo huo maana huwezi kukwepa kodi inayotumiwa na serikali kuwaletea maisha bora wananchi, kisha mtu huyo huyo ukajifanya unawapenda Watanzania, alisisitiza.
Alisema hata Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, alifanya ufisadi kwa kukiuzia chama magari makuu kuu aina ya Mitsubishi Fuso, ambayo chama kilikuwa kimeyakodisha kwa ajili ya matumizi yake.
Kuhusu madai kuwa alinufaika na fedha za EPA, Nape alisema huko ni kutapatapa kwani hawajawahi kutajwa katika kashfa hiyo tangu ianze miaka mingi iliyopita na wameanza kumpakazia baada ya kuanza kuwashambulia.
Hivi siku zote wanawataja wahusika wa EPA kwanini wasinitaje na mimi, leo hii wameona nimeanza kuanika maovu yao ndipo wanaanza kuhangaika kutafuta mambo ya kutunga, waambie Chadema ukivuliwa taulo chutama usikimbie, walizoea kusema wenzao sasa yamewageuka wanahaha alisema.
Kuhusu madai kuwa anapokea mishahara miwili, wa U-DC na wa CCM, Nape alisema alishakabidhi ofisi hiyo siku nyingi na madai hayo si ya kweli kwani hajawahi kupokea hata mshahara mmoja tangu ateuliwe katikati ya mwezi uliopita.
Tangu niteuliwe sijapata hata mshahara mmoja, inamaana Marando anamaanisha kuwa nalipwa mshahara kila wiki, alihoji Nape.
Alisema gari analotumia hivi sasa ni mali ya CCM tofauti na madai ya Marando kuwa anatumia gari la serikali.
Juzi Marando akiwa na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa chama hicho, Anthony Komu, waliwaambia waandishi wa habari kuwa mashambulizi ya Nape dhidi ya chama hicho yanatokana na chuki na hasira aliyonayo baada ya kukataliwa kugombea ubunge katika jimbo la Ubungo jijini Dar es Salaam.
Kadhalika, chama hicho kilidai kuwa mshahara wa Sh. milioni 7.1 anaolipwa Dk. Slaa na chama hicho ni kiasi kidogo ikilinganishwa na ule wa Mukama wa Sh. milioni 11.
CHANZO: NIPASHE
Kauli ya Nape aliyoitoa jana ni juhudi za kutaka kuusadikisha umma kwamba mshahara wa bosi wake haufui dafu kwa mshahara wa Katibu Mkuu wa (Chadema), Dk. Willbroad Slaa.
Nape alisema kuwa Mukama analipwa mshahara wa Sh. milioni 1.5 na posho ya mwezi ya Sh. 300,000.
Juzi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwanasheria wa Chadema, Mabere Marando, alisema Mukama analipwa mshahara wa Sh. milioni 11 wakati Dk. Slaa analipwa Sh. milioni 7.1, hivyo CCM hawana sababu ya kushangaa mshahara wa Slaa.
Malumbano hayo ya mishahara ya viongozi wa vyama hivyo viwili yanatokana na kauli ya Nape kuwa Dk. Slaa ameshinikiza kulipwa mshahara mnono akieleza msimamo huo unakinzana na wakati akiwa mbunge alipokuwa akishinikiza malipo kwa wabunge yapunguzwe.
Nape alidai kuwa mshahara wa Dk. Slaa ni sawa na wa mbunge.
Hata hivyo, uchunguzi huru wa NIPASHE uliofanywa juu ya mishahara ya viongozi watendaji wa CCM umebaini kuwa makatibu wa CCM wa mikoa wanalipwa mishahara ya Sh. milioni moja baada ya kodi, wakati makatibu wa wilaya wanalipwa Sh. 700,000 baada ya kodi, ilahali Katibu wa UVCCM akitia kibindoni Sh. milioni 1.5.
Kwa vigezo vya mishahara hiyo, ni sawa na kusema kwamba mishahara ya makatibu wa jumuiya na pengine ya makatibu wa mikoa haitofautiani na ile ya katibu mkuu.
Vile vile jana, Nape amekanusha madai yaliyotolewa na Mwanasheria wa Chadema, Marando kwamba yeye (Nape), alikwenda kuomba agombee ubunge Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya chama hicho na wakamkatalia kwa kukosa sifa.
Akizungumza na NIPASHE jana akiwa mkoani Singida, Nape alisema Chadema ndio walimfuata na kumwomba achague jimbo la kugombea kupitia chama hicho.
Waliniambia nichague Jimbo lolote la uchaguzi Dar es Salaam nigombee isipokuwa Ubungo, lakini nikawakatalia, niliwaeleza wazi kuwa mimi kuhama CCM ni sawa na kumsilimisha Papa sasa hiyo kauli ya Marando ni uzushi wa hali ya juu, alisema Nape.
Alidai hata alipohudhuria Baraza Kuu la chama hicho walimuomba avae sare za chama hicho na kisha kumwomba ajiunge na chama hicho, lakini alikataa na hata sare alizijaribu na kuwarudishia hapo hapo.
CCM ni chama kikubwa na kinapata ruzuku kubwa kuliko Chadema, lakini angalia mshahara wa Katibu Mkuu wetu linganisha na Sh. milioni 7.5 anazolipwa Dk. Slaa, Marando ameamua kwa makusudi kuupotosha umma hivyo kama ni muungwana basi aombe radhi kwa Watanzania aliowadanganya, alisema Nape. Alisema mshahara wa Mukama unalipiwa kodi wakati wa Dk. Slaa haukatwi kodi hivyo alimshauri kwanza kujisalimisha kwa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), kulipa kodi anayodaiwa.
Kutolipa kodi ni ufisadi wa hali ya juu, lakini mtu huyu huyu ambaye halipi kodi anajifanya ana uchungu na umaskini wa Watanzania, hata pale ofisini kwake kuna watu wanalipwa mishahara midogo hata haitoshi kujikimu kwa siku kumi, kuna msemo kwamba kabla hujatoa boriti kwenye jicho la mwenzako anza kutoa kwako, alisema Nape.
Tafsiri ya fisadi kwa mujibu wa Ilani yao ni mtu anayeishi kiujanja ujanja, sasa Dk. Slaa anaishi kwa mtindo huo maana huwezi kukwepa kodi inayotumiwa na serikali kuwaletea maisha bora wananchi, kisha mtu huyo huyo ukajifanya unawapenda Watanzania, alisisitiza.
Alisema hata Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, alifanya ufisadi kwa kukiuzia chama magari makuu kuu aina ya Mitsubishi Fuso, ambayo chama kilikuwa kimeyakodisha kwa ajili ya matumizi yake.
Kuhusu madai kuwa alinufaika na fedha za EPA, Nape alisema huko ni kutapatapa kwani hawajawahi kutajwa katika kashfa hiyo tangu ianze miaka mingi iliyopita na wameanza kumpakazia baada ya kuanza kuwashambulia.
Hivi siku zote wanawataja wahusika wa EPA kwanini wasinitaje na mimi, leo hii wameona nimeanza kuanika maovu yao ndipo wanaanza kuhangaika kutafuta mambo ya kutunga, waambie Chadema ukivuliwa taulo chutama usikimbie, walizoea kusema wenzao sasa yamewageuka wanahaha alisema.
Kuhusu madai kuwa anapokea mishahara miwili, wa U-DC na wa CCM, Nape alisema alishakabidhi ofisi hiyo siku nyingi na madai hayo si ya kweli kwani hajawahi kupokea hata mshahara mmoja tangu ateuliwe katikati ya mwezi uliopita.
Tangu niteuliwe sijapata hata mshahara mmoja, inamaana Marando anamaanisha kuwa nalipwa mshahara kila wiki, alihoji Nape.
Alisema gari analotumia hivi sasa ni mali ya CCM tofauti na madai ya Marando kuwa anatumia gari la serikali.
Juzi Marando akiwa na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa chama hicho, Anthony Komu, waliwaambia waandishi wa habari kuwa mashambulizi ya Nape dhidi ya chama hicho yanatokana na chuki na hasira aliyonayo baada ya kukataliwa kugombea ubunge katika jimbo la Ubungo jijini Dar es Salaam.
Kadhalika, chama hicho kilidai kuwa mshahara wa Sh. milioni 7.1 anaolipwa Dk. Slaa na chama hicho ni kiasi kidogo ikilinganishwa na ule wa Mukama wa Sh. milioni 11.
CHANZO: NIPASHE