Misamiati mipya ya Kiswahili sanifu

Kuperemba-kusimamia, fuatilia hotuba ya bajeti mkulo:serikali itaperemba mashirika yote yaliyobinafsishwa kujua ubora wake. Sasa kama ni kutongoza haitaleta maana..

Mkuu, Kuna baadhi ya maneno ya Kiswahili yana maana zaidi ya moja, mfano
kaa, paa,mbuzi, koroma,kina, kima..........Hivyo si ajabu hata neno peremba.
 


Dah!Asante sana mkuu kwa kutukumbusha umuhimu wa lugha yetu.
Ila nisidanganye,kwa staili hii nahisi sikijui kiswahili kama nilivyodhani,asante kwa changamoto.
 
Jamani Bujibuji hatusemi misamiati, neno sahihi na sanifu ni msamiati iwe katika wingi ama umoja.
 
kwa mtazamo wangu-wale wazee wanaotunga misamiati mipya-wanakosea sana-waache maneno yatumike kama yalivyo-mbona wachina wana simplified chinese,standard chinese na traditional chinese-na sisi pia tungeacha tuwe na simplified swahili ambayo itakuwa na mchanganyiko wa maneno ya kiingereza kama password,compyuta n.k, kuliko kulazimisha maneno mapya kama BAOBONYE n.k-bora iwe inajulikana kuwa Tanganyika wanazungumza simplified swahili-na zanzibar na mombasa wanazungumza traditional swahili-kuliko kutaka kubadili kila neno-hii inafanya sisi waswahili wenyewe kushindwa kuijua lugha yetu
 

hyseee! Nimekubali we mkali.
 
computer - tarakilishi
ict - teknohama (teknolojia ya habari na mawasiliano)
frequency - kasimawimbi
scratch card - kadihela
software - maunzi
screen - kiwambo
cpu - kku (kitengo kikuu cha uchakataji)
 
Nyie naona karibuni mtaanza kuandika hata matusi, eti ni misamiati mipya ya kiswahili. Shauri yenu!
 
ni BaoBonye si BaoBonya kwa Kizungu KeyBoard. ni sehemu mojawapo ya Tehama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…