Ooh okay....basi una chembechembe za hao ndugu zetu.
Sema hao jamaa wanapenda sifa na status fulani.....mfano apo uliposema "ulimwalika professor kutoka chuo fulani"......palikuwa hapana ulazima sana,ingetosha kusema ulimwalika mtu au jamaa ili kuficha code au kabila lako...ahahahaa
Hapana,
Hizo fikra zako ni fikra za fake modesty na unyonge unyonge fulani, usiri usiri fulani usio na tija wala ulazima. Maisha ya kupangiana pangiana cha kusema bila hata kujuana. Maisha ya jealous people.
Ni fikra za jamii za watu wachawi wachawi, waoga waoga, ambazo mimi nishapita huko.
Fikra zangu ni za uwazi zaidi.
Yani ni za kuniwezesha hata kukutana na huyo Profesa hapa akasoma code akanijia halafu akafurahia kukutana nami hapa.
Kwa hivyo, tuna falsafa tofauti za maisha.
Wewe una falsafa za inferiority complex. Ukimsikia mtu anaelezea experience yake, ya kawaida tu, unaona anajigamba.
Kwa sababu wewe ni masikini sana, ninaposema masikini sana, simaanishi masikini wa mali tu, wewe ni masikini hata wa mawazo.
Yani ni mchoyo wa fadhila hata kimawazo tu, umeshindwa kunipa "the benefit of the doubt" kwamba, labda, labda, huyu mtu alivyotaja "Profesa wa UDSM" alikuwa ana point hapa, point yake nini? Labda alimaanisha kutoa mizani kwamba Ubalozi wa Marekani unasumbua sana, kiasi kwamba, hata mtu ambaye sehemu nyingine anaweza kuwahishwa kwa kuheshimiwa, mtu kama Profesa wa UDSM, alivyofika Ubalozi wa Marekani hajafagiliwa wala nini, kawa processed kama mtu wa kawaida tu.
Point yangu haikuwa ku brag kwamba nimemualika Profesa wa UDSM. Uprofesa ni kitu cha kawaida sana na UDSM wala haipo katika rankings za dunia. Ingawa hata nikiamua ku brag hivyo ni haki yangu, kwa sababu nilimualika kweli. What's wrong with saying so if it's true?
Point yangu ilikuwa kuonesha humility kwamba Ubalozi wa Marekani TZ hata ukiwa Profesa wa UDSM hawakufagilii, unawekwa kwenye mstari kama mtu mwingine tu.
Ila, wewe kwa akili yako ya inferiority complex ya kibongobongo, hukuweza kuona hilo.
Wabongo mna visa sana
Nyuzi kama hizi watu wengi walio nje wanaziona wanazichunia tu. Kwa sababu ya vimajungu majungu na vi inferiority complex kama hivi.
Halafu tunakuja watu tunafunguka kwa roho safi tu, tukitaka kusaidiana, mnakuja kuwa prove right watu wanaouchuna.
Acheni majungu ya kijinga.
Mimi nikiamua kujigamba sijigambi kwenye thread ya mtu.
Naanzisha thread yangu.
Halafu sijigambi kirahisirahisi.
Najigamba kwa vina na mizani
Nakutoa lindi la kina kinzani kizani
Najigamba kwa stanza
Kaa kwanza, sikiliza rhymes kaa Kwanza
Unit, unique
Dar Mwanza, nikipita mtaani utajibanza
Oysterbay Ghuba Chaza
Nishapanda bei faza
Hunishiki, acha kuendekeza dhiki
Huu muziki, stereo hauhitaji kiki
Shall I continue...?