Miongoni mwa neema au bahati kuu watakayoipata watu wa peponi ni kuonana na Mwenyezi Mungu

Miongoni mwa neema au bahati kuu watakayoipata watu wa peponi ni kuonana na Mwenyezi Mungu

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
23,877
Reaction score
31,632
Si kila binadamu atapata bahati ya kumuona Mwenyezi Mungu.

Watakaobahatika kumuona Mwenyezi Mungu ni wale tu waliokidhi vigezo na kufuzu mitihani waliyopewa hapa duniani kubwa zaidi kukamilisha kile walicholetewa duniani ambacho ni kuabudu.

Hii ni kitu special sana, tukija hata kwenye maisha ya kawaida hapa duniani , kila mtu anayule mtu ambaye anatamani kuonana naye ana kwa ana, mfano wapo wenye hamu ya kuwaona mastaa wakubwa ulimwenguni ,iwe ni mastaa wa mipira, miziki, sanaa nk.

Wengine wanalipia pesa ndefu kwenda tu kuwaona hao binadamu wenzao ambao ni mastaa.

Sasa kama hao binadamu ipo hivyo, sasa je kupata bahati ya kuonana na mitume , malaika wa Mwenyezi Mungu je itakuaje?

Je, vipi kuhusu yeye aliyeumba mbingu na ardhi na kuweka vilivyomo itakuwaje ukipata bahati ya kuonana naye?
 
We chalii dini haiendi kibubusa kma hivi ulivoandika
Haya tupe ushahidi wa Qur'an, hadithi na maneno ya maswahaba au mwanachuoni kuthibitisha andiko lako?
 
Kwanini masheikh wenu hawawezi kutamka "mwenyezi Mungu" kwa usahihi? Wanaishia kutamka "mnyazi mngu".
 
We chalii dini haiendi kibubusa kma hivi ulivoandika
Haya tupe ushahidi wa Qur'an, hadithi na maneno ya maswahaba au mwanachuoni kuthibitisha andiko lako?
Endelea kutenda dhambi uone kama utamuona Mwenyezi Mungu.
 
YEES, Kwenye Jerusalem jipya tutauona uso wa MUNGU!

I live for this. Yani me naishi ili nije kumuona MUNGU na si vinginevyo! Hiyo ndo hamu yangu, ndoto yangu, kusudi langu maishani.

I feel closer to him as days goes by. I CANNOT WAIT! !

"Hapana kitu chochote kilicholaaniwa kitakachokuwa katika mji huo. Kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwanakondoo kitakuwa katika mji huo, na watumishi wake watamwabudu.

Watauona uso wake, na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao."

Ufunuo.22.3-4.BHN


"Wapenzi wangu, sisi ni watoto wa Mungu sasa, lakini bado haijaonekana wazi jinsi tutakavyokuwa. Lakini tunajua kwamba, wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwani tutamwona vile alivyo."
1Yohana.3.2.BHN

(By the way I realised wasioamini hawatokuja kumuona MUNGU / Yesu. Hata Mathayo anasema akija, watu wa mataifa wataiona ishara yake! Sijui hiyo ishara ni nini.

Wateule watamuona ni kwasababu watapewa miili mipya mitakatifu inayoweza kuhimili huo utukufu. Ni kama kupewa zile suti za wanaanga ili kujikinga na miale hatari huko juu.

Mpinga Kristo mwenyewe kinachomuua ni Utukufu wa YESU.

"Hapo ndipo Mwovu atakapotokea; lakini Bwana Yesu anapokuja atamuua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa mng'ao wa kuja kwake."
2Wathesalonike.2.8.NENO2025

So nafikri baada ya wasioamini dunia nzima kuona hiyo ishara ya YESU, watagundua ni YESU, lakini hawatomuona mwenyewe! !

Na mpinga Kristo na majeshi yake huko Yerusalemu ambapo ndo YESU atashukia watakufa automatically baada ya kumuona! !

Ndomana Vita inayokuja huko Israeli, vita ya kumaliza vita zote, vita ya Ezekieli 38 inaisha kimuujiza! !

Hiyo ishara ni nini?)
 
Endelea kutenda dhambi uone kama utamuona Mwenyezi Mungu.
Mimi sijakataa ila ukileta mambo ya dini ulete na ushahiddi najua huna elimu hio nfo mana huwezi kuthibitisha ww unalolijua ni umbea tu
 
Mimi sijakataa ila ukileta mambo ya dini ulete na ushahiddi najua huna elimu hio nfo mana huwezi kuthibitisha ww unalolijua ni umbea tu
Endelea kutenda dhambi uone kama utamuona Mwenyezi Mungu.
 
Na kingine, kwanza tukubaliane:

1) Utawala wa YESU wa miaka 1000 bado haujaanza kama Wakatoliki wanavyofundisha

2) Utawala huo ni hapa duniani na sio mbinguni kama Walokole, Wasabato wanavyofundisha

3) Watakaokuwa wanazaliana ndani ya miaka elfu ni wale watakaookoka dhiki kuu, yani watakaomuamini YESU wakati wa Dhiki kuu, na si wateule wa leo, kama Mashahidi wa Yehova wanavyofundisha.

4) Wateule watakuwa mahukani kwenye hekalu halisi la Ezekieli 40-48 hapa duniani, YESU ataishi hapa duniani, atakuwa na ardhi yake hapa duniani, kabla hata ya dunia mpya kuumbwa.
(Maelezo hapa:
Post in thread 'Hivi punde tu Yesu anachukua/nyakua watakatifu wake walioko duniani..in no time..watu watanyakuliwa. Muda umefika' Hivi punde tu Yesu anachukua/nyakua watakatifu wake walioko duniani..in no time..watu watanyakuliwa. Muda umefika)


Basi, hata wale watakaokaokuwa wanazaliana katika ile miaka elfu moja hapa duniani hawatomuona YESU, mpaka miaka 1000 iishe!

Watauona mwanga wake tu unatokea kutoka ndani ya hekalu, maana hata jua kutakuwa hamna!

Watakuwa wanakuja kuabudu hekaluni bila kumuona YESU kama alivyo, kama sisi tunavyomuabudu leo. (Zekaria 14)

Baada ya miaka 1000, Ndipo watakaokuwa upande wa YESU watapewa miili mipya ndipo watamuona! Na watakaomkataa YESU wataondolewa.

Mpango wa MUNGU wa siku 7 / miaka 7000 ya kufundisha / kuchagua wake unakuwa umekamilika.

Ndipo mbingu na dunia mpya zitaumbwa.

(Ubishe kwa maandiko)
 
Back
Top Bottom