Ng'wamapalala
JF-Expert Member
- Jun 9, 2011
- 6,811
- 6,506
Let's be honest. Hivi unafikiri ni wangapi wana katiba ya chama au tayari wameishaisoma.
Hawa hawa wanaobeza na kubwabwaja kama sikosei wengi wao hawajui hata katiba ya chama ikoje achilia mbali kanuni, maadili, miongozo, taratibu na itifaki za chama.
Hawa hawa wanaobeza na kubwabwaja kama sikosei wengi wao hawajui hata katiba ya chama ikoje achilia mbali kanuni, maadili, miongozo, taratibu na itifaki za chama.
Mkuu Kitila,
Huyu mwanachama wenu anatakiwa kuelemishwa kama ulivofanya hapa chini na sio kubezwa kama wanavyofanya wengine hapa.
Mwanachama amefanya la maana kuwakilisha tatizo walilo nalo huko kwao. Inawezekana tatizo ni matokeo ya wao wenyewe kutokuelewa mifumo ya uongozi. Lakini kwasababu ameamua kulisema tatizo lao; mimi ningetegemea CHADEMA wenye uelewo wamwelemishe huyu jamaa kwa lugha isiyo na kubeza au vijembe. Kwamba hata yeye kama ameweza kufikisha ujumbe hapa tayari ni kiongozi na awakusanye wenzake wote ili waunde uongozi hapo hapo walipo.
Uelewo wa watu wetu bado mdogo sana, sio kwenye masuala ya siasa tu bali hata kwenye masuala ya uchumi wao. Kuna fursa zingine wanazo lakini wanashindwa kuzitumia. Ni vizuri tuwe wapole na kuwaelemisha na sio kuwabeza au kuwatumia maneno makali.
Ni ushauri kwa mzee mwenzangu maana sisi wa zamani tulikuwa na hamu ya kuelemishnaa na kufundishana hapa JF.