Sungurampole
JF-Expert Member
- Nov 17, 2007
- 984
- 205
Nimesoma Citizen ya 1.4.11 kuhusu rufaa ya mgombea ubunge wa Tarime Mwita Waitara. Analalamika kuwa ametakiwa na mahakama kuu kuwasilisha TZS 12m/= ndani ya siku 14 sivyo kesi itafutwa. Nilitafakari na mwisho kuishia kujiuliza hivi tuko sawa hapa? Haki ya mtanzania iko wapi kama ili aidai inabidi awe na 12m/=? Hata ungesema 2m/= au 1m/= bado tutakua wengi tutakao kuwa tumebanguliwa na sheria hii. Wataalamu wa haki na katiba msemaje kuhusu hili?