Millioni 12 kukata rufaa ya ubunge?

Sungurampole

JF-Expert Member
Nov 17, 2007
984
205
Nimesoma Citizen ya 1.4.11 kuhusu rufaa ya mgombea ubunge wa Tarime Mwita Waitara. Analalamika kuwa ametakiwa na mahakama kuu kuwasilisha TZS 12m/= ndani ya siku 14 sivyo kesi itafutwa. Nilitafakari na mwisho kuishia kujiuliza hivi tuko sawa hapa? Haki ya mtanzania iko wapi kama ili aidai inabidi awe na 12m/=? Hata ungesema 2m/= au 1m/= bado tutakua wengi tutakao kuwa tumebanguliwa na sheria hii. Wataalamu wa haki na katiba msemaje kuhusu hili?
 
hii kiboko, ndio haya haya leo tunahitaji katiba mpya na sio viraka.

M12 anatoa wapi? Lazima uwe fisadi na si rahisi kwa mtanzania wa kawaida kwani vipato vyetu tunavijua.

ushauri kwa ndugu yangu Mwita, piga harambee tutakuchangia...kwani nguvu ya umma ndio njia pekee iliyobaki kupambana na ufisadi. Tuatachie hio ripoti ya mahakama kama ushahidi ,na weka akaunti yako humu tukuchangie.

nchi yetu sote ila tunanyanyasana sana..kama wengine ni watoto wa kambo vile, mi sielewi.
 
Back
Top Bottom