RWETAKA KACHUBO
Member
- Dec 1, 2011
- 10
- 4
Siku za nyuma kidogo nilieleza jinsi waanafunzi wanavyochaguliwa vyuo vya kati hasa vya Afya isivyo kuwa na utaratibu mzuri. Nikaeleza kuwa vyuo hivyo vinachukua wanafunzi wenye points 10 mpaka 18. Mwanafunzi aliyesoma shule ya kata ,ambaye MIAKA yote ameangaika kupata Mwalimu wa Physics kwa mfano,kupata points 10 ni miujiza. Nikaendelea kushauri kuwa vyuo vikiweka vigezo vya kujiunga kwn vyuo ,waanze kuchagua wanafunzi kutoka shule za kata kama wanakidhi vigezo. Leo nitaongelea mikopo ya vyuo vya kati. Baada ya wanafunzi wa shule za kata kutupwa nje kwn mzunguko wa kwanza na vyuo vya Serikali vya kati, wazaz waligeukia vyuo binafsi. Mpka leo majina hayajatoka,na mwisho wa kuomba mkopo ni 30 mwezi huu( kama hawajabadirisha). Sasa hata kama matokeo yatatolewa leo,mzazi aombe RITA kubadiri chet cha kuzaliwa itamchukua kama siku 3( MAANA vyeti vya zamani hawavitaki na huku walivitoa wao). Mwishoe utakuta watoto waliyosoma shule za kata wanatupwa nje ya utaratibu wa utoaji wa mikopo.
Nimejiuliza maswali mengi...labda ni mkakati wa watu fulani kuhakikisha watu wa maisha ya chini wanazidi kuwa nje ya utaratibu wa Elimu? Waziri Adolf kaka yangu ingilia kati.
Nimejiuliza maswali mengi...labda ni mkakati wa watu fulani kuhakikisha watu wa maisha ya chini wanazidi kuwa nje ya utaratibu wa Elimu? Waziri Adolf kaka yangu ingilia kati.