kande kavu
JF-Expert Member
- Sep 17, 2011
- 234
- 86
Habari wana jamii/ NSSF Staff.
Mimi ni mwanachama wa NSSF kwa kipindi cha miaka 15 sasa. Hivi karibuni mfuko wetu huu ulitangaza kuwa utaanza kutoa mikopo kwa wanachama wake kupitia SACCOS tena kwa riba ndogo! Tangazo hilo kama sikosei lilianza kutolewa mwezi wa Mei mwaka huu, ikiwapo utaratatibu wote wa kupata mikopo hiyo (MWANACHAMA-SACCOS).
La kusikitisha, mimi na SACCOS yangu tumekamilisha utaratibu wote tangu mwezi Agosti lakini mkopo hautoki wala hakuna taarifa ya nini kinaendelea mpaka tumeingia mwezi Disemba. Ifahamike kuwa wengine hatukopi ili tucheze ngoma, bali kuimarisha biashara zetu. Hiyo pesa niliyoomba sipewi bure,na kwa kutangaza riba ndogo kuliko ya SACCOSS yangu au mabenki, mlinifanya niweke mipango yangu ya biashara kwa kukopa kwenu! Lakini ona mlivyonipotezea muda na biashara, si bora ningekopa kwenye riba kubwa lakini nikapata mkopo ndani ya siku kumi! Ya nini kuamsha tamaa na matumaini hewa kwa wanachama kama hamko tayari?
MMENIVURUGA!
Mimi ni mwanachama wa NSSF kwa kipindi cha miaka 15 sasa. Hivi karibuni mfuko wetu huu ulitangaza kuwa utaanza kutoa mikopo kwa wanachama wake kupitia SACCOS tena kwa riba ndogo! Tangazo hilo kama sikosei lilianza kutolewa mwezi wa Mei mwaka huu, ikiwapo utaratatibu wote wa kupata mikopo hiyo (MWANACHAMA-SACCOS).
La kusikitisha, mimi na SACCOS yangu tumekamilisha utaratibu wote tangu mwezi Agosti lakini mkopo hautoki wala hakuna taarifa ya nini kinaendelea mpaka tumeingia mwezi Disemba. Ifahamike kuwa wengine hatukopi ili tucheze ngoma, bali kuimarisha biashara zetu. Hiyo pesa niliyoomba sipewi bure,na kwa kutangaza riba ndogo kuliko ya SACCOSS yangu au mabenki, mlinifanya niweke mipango yangu ya biashara kwa kukopa kwenu! Lakini ona mlivyonipotezea muda na biashara, si bora ningekopa kwenye riba kubwa lakini nikapata mkopo ndani ya siku kumi! Ya nini kuamsha tamaa na matumaini hewa kwa wanachama kama hamko tayari?
MMENIVURUGA!