Mkurya mweupe
JF-Expert Member
- Aug 10, 2023
- 227
- 742
Serikali kupitia bodi ya Mikopo waliahidi kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaotakiwa kujiunga na vyuo kwa ngazi ya diploma kuwa mwaka huu wanafunzi hao pia watanufaika na mikopo hiyo, baadae bodi ya Mikopo ilitoa tangazo katika mitandao yake ya kijamii kuwa, utaratibu kwa wanafunzi wa vyuo vya Kati, utatolewa ili waweze kuomba mikopo hyo, lakini siku zinazidi kusonga na bado bodi ya Mikopo haijatoa utaratibu kwa wanafunzi hao Kama wanatakiwa waombe mikopo au bado, hivyo bodi ya Mikopo na serikali mnaombwa mtoe ufafanuzi kuhusu hilo suala hasa Mwigulu Nchemba akiwasilisha bajeti alisoma serikali huu mwaka itaanza kutoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya Kati ? Lakini mpaka sasa hivi bodi ya Mikopo bado ipo kimya.