Mikopo kwa graduates

Mikopo kwa graduates

Afande Nyati

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2012
Posts
2,385
Reaction score
1,414
Wakuu nimeckia taarifa za chini ya kapet kwamba TIB wanatoa mikopo kwa graduates dhamana vyeti. Kwa mwenye taarifa juu ya hili atujuze pls.
 
Duh hapo ukishindwa kulipa wanabeba vyeti sijui wateanda kuviuza au itakuaje?
 
hao jama washenzi kuchukua mkopo mpk uwe biashara si chini ya 40m. hiyo labda kwa Tanzania ya mbinguni ndo mtapata la sivyo zitakuwa km walizo piga kina ruge.
 
hao jama washenzi kuchukua mkopo mpk uwe biashara si chini ya 40m. hiyo labda kwa Tanzania ya mbinguni ndo mtapata la sivyo zitakuwa km walizo piga kina ruge.

Samahani mkuu hebu andika vizuri na udadavue kidogo yaani nimetoka patupu ila nahisi una jambo lenye mashiko
 
Unazungumzia TIB investment bank? kama ni hao ni bora ukaenda branches zao ambazo nafkir kwa tanzania zko mikoa 6 pamoja na ya zanzibar uko utapata full information.... ni wewe kueleza tu uko mkoa gan usaidiwe uende wap
 
TIB KUTOA MIKOPO KWA VIJANA; ZOEZI KURATIBIWA NA BARAZA LA TAIFA LA UWEZESHAJI (NEEC)

Baraza la taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi, (NEEC), na TIB Development bank, wametialiana saini makubaliano ambayo yatatoa fursa kwa vijana wahitimu wa vyuo vikuu na vya kati kupata fursa ya mikopo kwa nia ya kujiajiri wenyewe.
Katika makubaliano hayo TIB itatoa mikopo hiyo ambapo kwa kuanzia kiasi cha shilingi bilioni 1 kimetengwa kwa ajili ya mpango huo utakaoratibiwa na NEEC ambayo itakuwa na jukumu la kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana hao ikiwa ni pamoja na kusaidia namna ya kutayarisha andiko, (Proposal), la miradi kwa nia ya kuomba mikopo.
Kwa mujibu wa taarifa ya pamoja ya taasisi hizo mbili, mikoipo hiyo itatolewa Tanzania Bara na inalenga kusaidia miradi ya kilimo, uzalishaji, biashara na huduma kwa lengo la kuwawezesha vijana katika harakati za kukuza uchumi wa taifa.
Taarifa hiyo pia ilifafanua kuwa mikopo hiyo itatolewa kwa vyama vya ushirika (Cooperatives), na mtu mmoja mmoja (Individual), Viwango vya mikopo itakayotolewa kwa mujibu wa taarifa hiyo ni shilingi zisizozidi milioni 200 kwa SMEs na washirika au ushirika, wakati shilingi zisizozidi milioni 50 kwa kijana mhitimu wa chuo kikuu mjasiriamali ambaye awe amefaulu mafunzo hayo ya kuwaandaa wajasiriamali yatakayokuwa yakitolewa na NEEC.
Picha ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NEEC), Dkt. Anacleti Kashuliza, (Kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TIB, Peter Noni, wakionyesha waandishi wa habari mikataba hiyo baada ya kuisaini.Noni wa TIB, (Kulia) na Dkt. Kashuliza wa NEEC, wakibadilishana hati hizo baada ya kusainiKatibu mtendaji wa baraza la taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi, NEEC, Dkt. Anacleti Kashuliza, (waliokaa kushoto) na mkurugenzi mtedaji wa benki ya maendeleo TIB, Peter Noni, wakisaini makubaliamo hayo. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni afisa wa sheria wa NEEC, Esther Barikie Mbaga, Mwenyekiti wa bodi ya NEEC, Omar Issa, mkurugenzi wa mfuko wa uwezeshaji wa TIB, Prisca V. Chang'a, na mwanasheria na katibu wa bodi ya TIB, Martha J.J.Maeda"Vijana wasajili kampuni zao kwwnye mamlaka zinazohusika ili iwe rahisi kuaminiwa na benki" Peter Noni"Kuwawezesha wananchi kiuchumi ndio njukumu letu kuu" Dkt. Anacleti KashulizaShahidi upande wa TIB, ambaye ndiye mwanasheria wa benki hiyo, Martha J.J.Maeda, "akimwaga wino"Afisa wa sheria wa NEEC, Esther Barikiel Mbaga, akithibitisha kwa kuweka saini yake kuwa makubaliano hayo ni ya kisheria na halaliBaadhi ya viongozi wa TIB, wakifurahia jamboPicha ya pamoja ya waliohudhuria hafla hiyo
 
Nasubiri kwa hamu maana mtaa umenichocha! Nitawapelekea vyeti vyangu japo nilipata GPA ya 1:8.
 
Ni jambo zuri,anyejua mikoa ambayo tayari hawa jamaa wanatari kuanza,watuandikie hapa ili tujitupe huko maana mtaan kugumu!
 
safi inapendeza!
TIB KUTOA MIKOPO KWA VIJANA; ZOEZI KURATIBIWA NA BARAZA LA TAIFA LA UWEZESHAJI (NEEC)

Baraza la taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi, (NEEC), na TIB Development bank, wametialiana saini makubaliano ambayo yatatoa fursa kwa vijana wahitimu wa vyuo vikuu na vya kati kupata fursa ya mikopo kwa nia ya kujiajiri wenyewe.
Katika makubaliano hayo TIB itatoa mikopo hiyo ambapo kwa kuanzia kiasi cha shilingi bilioni 1 kimetengwa kwa ajili ya mpango huo utakaoratibiwa na NEEC ambayo itakuwa na jukumu la kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana hao ikiwa ni pamoja na kusaidia namna ya kutayarisha andiko, (Proposal), la miradi kwa nia ya kuomba mikopo.
Kwa mujibu wa taarifa ya pamoja ya taasisi hizo mbili, mikoipo hiyo itatolewa Tanzania Bara na inalenga kusaidia miradi ya kilimo, uzalishaji, biashara na huduma kwa lengo la kuwawezesha vijana katika harakati za kukuza uchumi wa taifa.
Taarifa hiyo pia ilifafanua kuwa mikopo hiyo itatolewa kwa vyama vya ushirika (Cooperatives), na mtu mmoja mmoja (Individual), Viwango vya mikopo itakayotolewa kwa mujibu wa taarifa hiyo ni shilingi zisizozidi milioni 200 kwa SMEs na washirika au ushirika, wakati shilingi zisizozidi milioni 50 kwa kijana mhitimu wa chuo kikuu mjasiriamali ambaye awe amefaulu mafunzo hayo ya kuwaandaa wajasiriamali yatakayokuwa yakitolewa na NEEC.
Picha ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NEEC), Dkt. Anacleti Kashuliza, (Kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TIB, Peter Noni, wakionyesha waandishi wa habari mikataba hiyo baada ya kuisaini.Noni wa TIB, (Kulia) na Dkt. Kashuliza wa NEEC, wakibadilishana hati hizo baada ya kusainiKatibu mtendaji wa baraza la taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi, NEEC, Dkt. Anacleti Kashuliza, (waliokaa kushoto) na mkurugenzi mtedaji wa benki ya maendeleo TIB, Peter Noni, wakisaini makubaliamo hayo. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni afisa wa sheria wa NEEC, Esther Barikie Mbaga, Mwenyekiti wa bodi ya NEEC, Omar Issa, mkurugenzi wa mfuko wa uwezeshaji wa TIB, Prisca V. Chang'a, na mwanasheria na katibu wa bodi ya TIB, Martha J.J.Maeda"Vijana wasajili kampuni zao kwwnye mamlaka zinazohusika ili iwe rahisi kuaminiwa na benki" Peter Noni"Kuwawezesha wananchi kiuchumi ndio njukumu letu kuu" Dkt. Anacleti KashulizaShahidi upande wa TIB, ambaye ndiye mwanasheria wa benki hiyo, Martha J.J.Maeda, "akimwaga wino"Afisa wa sheria wa NEEC, Esther Barikiel Mbaga, akithibitisha kwa kuweka saini yake kuwa makubaliano hayo ni ya kisheria na halaliBaadhi ya viongozi wa TIB, wakifurahia jamboPicha ya pamoja ya waliohudhuria hafla hiyo
 
wadau hizo update za mafunzo ya ujasiriamali from NEEC tutapata vipi bse wanasema ili uweze kupata mkopo lazima upate hayo mafunzo.

plz mwenye kujua zaidi anisaidie.
 
wadau hizo update za mafunzo ya ujasiriamali from NEEC tutapata vipi bse wanasema ili uweze kupata mkopo lazima upate hayo mafunzo.

plz mwenye kujua zaidi anisaidie.

Hi ni taarifa, bado aijawa oficial na wamesema wataanza na mafunzo na daresalama kwanza ndipo wataenda kwingne.... watatoa matangazo pind mambo yakikamilika kwa iyo tusitue taarifa za uongo, nimepita mlimani city leo nimewaulizia, and if you are serious go and visit their branch for mor detalsand dont hesitate to ask them: Dar es Salaam Branch - Building 3, Mlimani City OfficePark, Sam Nujoma Road, Dar es Salaam
2.Mwanza Branch - 3rd Floor, PPF Plaza Building, Mwanza
3.Arusha Branch - Central Plaza Building, Sokoine Road, Arusha
4.Mbeya Branch - 28 Jakaranda Street, Mbeya
5.Dodoma Branch - Dodoma
6.Zanzibar Branch - Zanzibar
 
Vikikopa vikundi vitano mil 200 kila kimoja zimekwisha. Wakikopa mil 50 ni vijana 20 tu watapata.

yani hapo kuna usanii usanii,,mi naona wanataka wapige hela za mafunzo ua ujasiriamali tuu
 
Kama wameshatiana saini makubaliano ya mpango huo inamaana fedha nazo zipo na sio ajabu wale wakusubiri hadi matangazo official wakaskia fedha zimekwisha. Graduate apate 50ml wakat mfanyakaz mwenye mkataba 5yrs anaruhusiwa kukopa labda hadi 30ml tuu. Usanii lazima ufanyike hapo
 
Back
Top Bottom