Mijadala ya siasa maofisini

Mijadala ya siasa maofisini

mshamu

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2011
Posts
418
Reaction score
134
Hapa ofisini kwetu jamani imezidi na watu wanajadili siasa mpaka wengine wajiita makamanda. Vipi huko kwenu kati ya magamba na makamanda mambo yakoje? Kwetu hapa ukijulikana ni gamba utakosa raha.
 
Hapa ofisini kwetu jamani imezidi na watu wanajadili siasa mpaka wengine wajiita makamanda. Vipi huko kwenu kati ya magamba na makamanda mambo yakoje? Kwetu hapa ukijulikana ni gamba utakosa raha.

Ofisi niliyopo ukiona Mtu sio Kamanda basi ni hafuatilii Siasa, hakunaga Gamba kabisa (Big-up my HRM).
 
Kasome sheria ya utumishi wa umma halafu urudi utuambie umeelewa nini
Hapa ofisini kwetu jamani imezidi na watu wanajadili siasa mpaka wengine wajiita makamanda. Vipi huko kwenu kati ya magamba na makamanda mambo yakoje? Kwetu hapa ukijulikana ni gamba utakosa raha.
 
dah!! hapa kwetu tunawaza business tu. hatuna habari na siasa wala muda nao.
 
Kwetu watu wanaoshabikia magamba ni wale ambao siku zao za ajira zinahesabika, nina maana baada ya mwaka 1 hivi watakua tayari wamesajiriwa kwenye pension, vijana wachache sana na ukweli hata wenyewe hua wanaona aibu kabisa kujionesha kama wapo magambani!
 
Hapa hakuna Magamba ukimuondoa mkuu wa idara ambaye anastaafu 2016 Makamanda tumeshamiri kila kitengo na kadi zetu kwenye madroo hakuna cha sheria ya utumishi wa umma wala nini.....hakuna aliye muoga mpaka kwenye vikao wanajua na madiwani wanalijua hawana jeuri ya kukataza wanabaki kulalamika tu kwenye kamati zao za siasa
 
Kwetu hali pia ni ile ile, kuna dingi flan alikua gamba damu lakini baada ya kupata elimu ya uraia kutoka kwangu amejitambua na yupo mstari wa mbele ktk kueneza elimu hiyo na kuyakataa magamba. Tupo ktk shirika moja la umma
 
Tafuteni Ofisi zenu mkajadili siasa zenu , tunafuatilia kwa kina na mtu akibainika hana kazi sheria ziko wazi.
 
inategemea unafanya kazi idara gani/serikalini au private sector. mimi ofisini kwetu haturuhusiwi.
 
ni mwendelezo wa kutojitambua tu au ulimbukeni au stereo typeship au mtindo au fashion chagua tu kwa utulivu utapata where you belong
 
inategemea unafanya kazi idara gani/serikalini au private sector. mimi ofisini kwetu haturuhusiwi.

Poleni sana ila kama upo jf naamini wewe utakuwa na taarifa za kutosha kuhusu siasa mara moja moja muwe mnapeana elimu ya uraia kujua maisha yanendaje. Mimi najatahidi hata kuwapa jinsi ya kusoma jf huku kuna uhuru wa hoja.
 
Tafuteni Ofisi zenu mkajadili siasa zenu , tunafuatilia kwa kina na mtu akibainika hana kazi sheria ziko wazi.


Acha kutishia nyau we gamba kafie mbele na sharia zako,kwani Dr.Slaa huwa anapata wapi data?
 
Kasome sheria ya utumishi wa umma halafu urudi utuambie umeelewa nini

Ofisini kwetu makamanda wengi.hizo sheria za utumishi tupa kuleee!! mbona pale kiongozi wa CCM kata ya Lupiro wilayani Mahenge in Mwalimu wa sekondari. pyuuuuu double standard
 
Kwetu ni full gwanda hata sasa niko kwenye PC ya ofisi na post JF,tena ngoja ni mwite mkuu wa Idara yangu aje asome hii komenti.
 
Back
Top Bottom