nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,860
- 5,803
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"][/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"]Monday, 19 December 2011 20:51
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
Mussa Juma, Arusha
WABUNGE wa Mkoa wa Arusha, wamekwama kuunda umoja wao kutokana na makundi na migogoro iliyopo baina yao na hivyo kukwama kuwa na sauti ya pamoja bungeni.
Mbunge wa Viti Maalumu wa CCM, Mary Chatanda akizungumza katika kikao cha 30 cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Arusha, alimuomba ,mkuu wa mkoa huo, Magesa Mulongo kusaidia kushawishi wabunge hao kuanzishwa umoja huo.
Mkoa wa Arusha una jumla ya wabunge 11 ambapo kati yao wabunge wa Chadema ni wanne na CCM ina wabunge saba na kabla ya uchaguzi uliopita Mwenyekiti alikuwa ni Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa.
Akizungumza katika kikao hicho, Chatanda ambaye pia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, alisema kutokuwa na umoja wao kunasababisha kushindwa kuwa na sauti ya pamoja bungeni katika kutoa hoja zinazohusiana na maendeleo ya Arusha na kuzitetea.
"Mwenyekiti(mkuu wa mkoa) tusaidie kuundwa kwa umoja huu ili tuweze kukaa kwa pamoja kwani wenzetu bungeni wamekuwa na vikao vyao na kukaa na kukubaliana kwa maslahi ya mikoa yao, kuna mengi yanayokwamisha lakini sipendi kuyataja," alisema Chatanda.
Akijibu hoja hiyo, Mkuu wa Mkoa Arusha, Mulongo alisema kuwa na umoja wa wabunge ni jambo muhimu sana kwani utasaidia kusukuma mbele masuala ya maendeleo ya mkoa.
Alisema kwa hali ilivyo sasa mgawanyiko wa wabunge hao, unaweza pia kuathiri utendaji kwani pia unaibua mgawanyiko miongoni mwa watendaji wa Serikali.
Alisema atajitahidi kuwashawishi Wabunge wa Mkoa wa Arusha kuwa na umoja wao na ikishindikana atatoa taarifa katika kikao kijacho cha bodi ya barabara ya mkoa."Mimi nitajitahidi kukutana na wabunge lakini watakayosema nitakuja kuwaambia hapa, ni vyema wajue migogoro yao kama ipo haina manufaa kwa wananchi kwani wao wanataka maendeleo," alisema Mulongo.
Mkuu huyo wa mkoa pia aliwataka wabunge hao, kujenga tabia ya kuhudhuria vikao vya maendeleo ya mkoa kama cha bodi ya barabara na kamati ya ushauri ili wajue kero za wananchi na kuzifikisha bungeni.
"Mimi bado ni mgeni lakini naona hata mahudhurio ya vikao sio mazuri sana," alisema Mulongo.
Mkoa wa Arusha ni mmoja wa mikoa ambayo imeathiriwa sana makundi ya ndani ya CCM ambayo pia yalichangia chama hicho kupoteza viti kadhaa vya udiwani na ubunge
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TR]
[TD="class: contentheading"][/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"]Monday, 19 December 2011 20:51
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
WABUNGE wa Mkoa wa Arusha, wamekwama kuunda umoja wao kutokana na makundi na migogoro iliyopo baina yao na hivyo kukwama kuwa na sauti ya pamoja bungeni.
Mbunge wa Viti Maalumu wa CCM, Mary Chatanda akizungumza katika kikao cha 30 cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Arusha, alimuomba ,mkuu wa mkoa huo, Magesa Mulongo kusaidia kushawishi wabunge hao kuanzishwa umoja huo.
Mkoa wa Arusha una jumla ya wabunge 11 ambapo kati yao wabunge wa Chadema ni wanne na CCM ina wabunge saba na kabla ya uchaguzi uliopita Mwenyekiti alikuwa ni Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa.
Akizungumza katika kikao hicho, Chatanda ambaye pia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, alisema kutokuwa na umoja wao kunasababisha kushindwa kuwa na sauti ya pamoja bungeni katika kutoa hoja zinazohusiana na maendeleo ya Arusha na kuzitetea.
"Mwenyekiti(mkuu wa mkoa) tusaidie kuundwa kwa umoja huu ili tuweze kukaa kwa pamoja kwani wenzetu bungeni wamekuwa na vikao vyao na kukaa na kukubaliana kwa maslahi ya mikoa yao, kuna mengi yanayokwamisha lakini sipendi kuyataja," alisema Chatanda.
Akijibu hoja hiyo, Mkuu wa Mkoa Arusha, Mulongo alisema kuwa na umoja wa wabunge ni jambo muhimu sana kwani utasaidia kusukuma mbele masuala ya maendeleo ya mkoa.
Alisema kwa hali ilivyo sasa mgawanyiko wa wabunge hao, unaweza pia kuathiri utendaji kwani pia unaibua mgawanyiko miongoni mwa watendaji wa Serikali.
Alisema atajitahidi kuwashawishi Wabunge wa Mkoa wa Arusha kuwa na umoja wao na ikishindikana atatoa taarifa katika kikao kijacho cha bodi ya barabara ya mkoa."Mimi nitajitahidi kukutana na wabunge lakini watakayosema nitakuja kuwaambia hapa, ni vyema wajue migogoro yao kama ipo haina manufaa kwa wananchi kwani wao wanataka maendeleo," alisema Mulongo.
Mkuu huyo wa mkoa pia aliwataka wabunge hao, kujenga tabia ya kuhudhuria vikao vya maendeleo ya mkoa kama cha bodi ya barabara na kamati ya ushauri ili wajue kero za wananchi na kuzifikisha bungeni.
"Mimi bado ni mgeni lakini naona hata mahudhurio ya vikao sio mazuri sana," alisema Mulongo.
Mkoa wa Arusha ni mmoja wa mikoa ambayo imeathiriwa sana makundi ya ndani ya CCM ambayo pia yalichangia chama hicho kupoteza viti kadhaa vya udiwani na ubunge
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]