Mgosi Mbena
JF-Expert Member
- Nov 28, 2023
- 544
- 664
Kwa kawaida Watu au waafrica tunapozungumzia maendeleo tunaongelea vitu kama Ajira,Miladi wawekezaji kutoka nje,mikubwa,Au kugundulika kwa rasilimali kama mafuta,dhahabu au gesi .
Lakini kamwe hatuangali mifumo na nguzo hizi zinazotengeneza na kukuza uchumi.
Nguzo ya kwanza : UAMINIFU
Uaminifu wa watu,taasisi na jamii huongeza na kukuza uchumi kwa kuchochea biashara na ujasiria mali,
Jamii ya watu wasio waaminifu ni ngumu sana kufanya nao biashara, kuagiza mizigo,kulipia bidhaa.
Kwa sababu hiyo mtu lazima awepo ana kwa ana ndio mfanye biashara kwa kuogopa kutapeliwa.
Kuna watu wengi sana nchini wanaogopa kufanya biashara ya kutoa bidhaa mahali ilipo kupeleka sehemu nyingine bila kuepo eneo la tukio.
Mfano: mwaka 2013 Nilimtumia mtu (Namfaham) shilingi 270000 anitumie Karoti kutoka mbeya hadi Dodoma. Jamaa alipotumiwa hela akatokomea.
Leo hii ukisahau simu au laptop mahali dk0 huioni.
Sehemu iliyojaaa :Wizi,Utapeli, uzurumishi hamna biashara au uwekezaji unaweza kukua hapo
Nguzo ya pili :MUDA
Muda ni kiungo kizuri sana kama nchi na jamii inataka kuendelea.Jamii ambayo haijali muda ni ngumu sana kuendelea kwani maendeleo hupimwa na muda pia!
Ukitazama vikao: watu hufika saa moja baada ya muda husika, Harusi au sherehe watu huja masaa3 baada ya muda tajwa. Kila mradi unaofanyika lazima upilize deadline..
Kifupi sehemu ambayo muda si kipaumbele hata Kusonga mbele( si kipaumbele pia)
Nguzo ya tatu : MTAZAMO WA UJASIRIA MALI
Kuwepo jamii zenye mtazamo huu huchochea ubunifu na biashara! Sehemu ambayo kila mtu anawaza kuajiriwa ni ngumu sana kuwa na jamii iliyoendelea kwani hamna nchi inajengwa na Ajira tu.
Ni wajasiriamali ndio huanzisha safari zinazozalisha ajira.Kama hakuna hawa basi kila mtu atakua analia na ajira
Nguzo ya Nne: Uwezo wa kutatua matatizo!
Badala ya kuajiri watu kuzingatia vyeti watu watazamwe kwa uwezo wa kutatua matatizo! Leo tuna watu kwene idara nyeti wasio na uwezo wa kutatua matatizo ya taasisi, jamii, badala yake wao ni sehemu ya matatizo!
Hii ndio msingi wa maendeleo wenyewe
Lakini kamwe hatuangali mifumo na nguzo hizi zinazotengeneza na kukuza uchumi.
Nguzo ya kwanza : UAMINIFU
Uaminifu wa watu,taasisi na jamii huongeza na kukuza uchumi kwa kuchochea biashara na ujasiria mali,
Jamii ya watu wasio waaminifu ni ngumu sana kufanya nao biashara, kuagiza mizigo,kulipia bidhaa.
Kwa sababu hiyo mtu lazima awepo ana kwa ana ndio mfanye biashara kwa kuogopa kutapeliwa.
Kuna watu wengi sana nchini wanaogopa kufanya biashara ya kutoa bidhaa mahali ilipo kupeleka sehemu nyingine bila kuepo eneo la tukio.
Mfano: mwaka 2013 Nilimtumia mtu (Namfaham) shilingi 270000 anitumie Karoti kutoka mbeya hadi Dodoma. Jamaa alipotumiwa hela akatokomea.
Leo hii ukisahau simu au laptop mahali dk0 huioni.
Sehemu iliyojaaa :Wizi,Utapeli, uzurumishi hamna biashara au uwekezaji unaweza kukua hapo
Nguzo ya pili :MUDA
Muda ni kiungo kizuri sana kama nchi na jamii inataka kuendelea.Jamii ambayo haijali muda ni ngumu sana kuendelea kwani maendeleo hupimwa na muda pia!
Ukitazama vikao: watu hufika saa moja baada ya muda husika, Harusi au sherehe watu huja masaa3 baada ya muda tajwa. Kila mradi unaofanyika lazima upilize deadline..
Kifupi sehemu ambayo muda si kipaumbele hata Kusonga mbele( si kipaumbele pia)
Nguzo ya tatu : MTAZAMO WA UJASIRIA MALI
Kuwepo jamii zenye mtazamo huu huchochea ubunifu na biashara! Sehemu ambayo kila mtu anawaza kuajiriwa ni ngumu sana kuwa na jamii iliyoendelea kwani hamna nchi inajengwa na Ajira tu.
Ni wajasiriamali ndio huanzisha safari zinazozalisha ajira.Kama hakuna hawa basi kila mtu atakua analia na ajira
Nguzo ya Nne: Uwezo wa kutatua matatizo!
Badala ya kuajiri watu kuzingatia vyeti watu watazamwe kwa uwezo wa kutatua matatizo! Leo tuna watu kwene idara nyeti wasio na uwezo wa kutatua matatizo ya taasisi, jamii, badala yake wao ni sehemu ya matatizo!
Hii ndio msingi wa maendeleo wenyewe