Microfinance ni mkombozi kwa Watumishi wa Serikali nchini

Microfinance ni mkombozi kwa Watumishi wa Serikali nchini

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,606
Tuwe wakweli tu ndugu zanguni.


Mikopo midogo midogo kwenye taasisi za fedha mtaani zinasaidia sana Watumishi wa Umma katika kusolve matatizo yao madogo madogo na makubwa pia.

Wamekuwa waelewa sana kwa watumishi.

Wanakaa na ATM kadi na namba ya siri ya mhusika then wanakupa pesa kwa riba ya 20 hadi 40%. Lakini inasaidia sana.

Ni bora utatue tatizo kubwa hata kama kwa riba kubwa kuliko ukose kabisa halafu madhara yawe makubwa kuliko.

Unachukua 100,000 then unarejesha 140,000 kwa siku 30, naona ni swala la kawaida kabisa. Riba ya 40,000 kutatua tatizo lako zito ni kitu kidogo sana.

Serikali ijue kabisa hawa ndo mkombozi wa watumishi wa umma. Watu wamechoka sana.
 
Acha upotoshaji. Mkombozi wa kweli kwa watumishi wa umma ni saccoss zao, vicoba, na salary advance. Na siyo hao matapeli wa kalamu.

Zaidi ya hapo mtumishi wa umma, akope benki, na kuanzisha miradi ya kumuondolea utegemezi kwenye mshahara. Aachane kabisa na hizi takataka zenye riba kandamizi.

Mtumishi wa umma aliyejiongeza, kamwe hawezi kukopa laki 1 kwa Ma Loan Sharks!
 
Umetumwa,nenda kijijini kafuate madeni
Usitafute busara za serikali, mkitaka kufanikiwa boresheni mikataba na mshushe riba muongeze muda!
 
Back
Top Bottom