Timu ya Jiji la Mbeya yatesa Morogoro
Imeandikwa na Mwandishi Wetu, Morogoro; Tarehe: 21st February 2011 @ 22:00 Imesomwa na watu: 46; Jumla ya maoni: 0
TIMU ya netiboli ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya, imefanya mauji, kwenye michuano ya ligi daraja la pili inayoendelea kwenye Uwanja wa Jamuhuri wa mjini Morogoro, baada ya kuiangushia kipondo cha mabao 47-16 timu ya Tigo ya jijini Dar es Salaam..
Wakati timu hiyo ikipata ushindi huo katika robo fainali za ligi daraja la kwanza, timu ya netiboli ya Tandahimba ya Mtwara imejikuta ikipata kipigo cha mabao 36-16 kutoka kwa mpinzani wake Ruvu JKT.
Timu nyingine ambayo nayo imeanza vizuri katika mashindano hayo ni Polisi Arusha iliyoitandika mabao 27 -24 Ruangwa ya mkoani Lindi.
Akizungumza na waandishi, Mkufunzi wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta), Mary Protas amesema, timu zote zimeonyesha ushindani mkubwa na hali hii inatokana na wachezaji kufanya mazoezi pamoja na umakini wao pindi wawapo uwanjani.
Alisema, chama kinategemea kupata timu bora zitakazofanikiwa kuingia daraja la kwanza na kwamba kupatikana kwa timu hizo kutaleta changamoto kubwa katika mchezo wa netiboli ambao umekuwa ukisahaulika sana kwa jamii.
Kwa upande wake , kocha wa Hamambe Joyce Mwakifamba, ametamba timu yake kuchukua ushindi na kufanikiwa kuingia ligi daraja la kwanza kwani tangu mashindano yaanze timu hiyo haijawahi kufungwa.
Alisema, siri kubwa ya timu hiyo kujipanga, mazoezi, umakini wa wachezaji pamoja na wadhamini wa timu hiyo ambao ni Halmashauri ya Jiji la Mbeya kuwajali wachezaji kwa kuzingatia posho na malazi.
Timu 11 zilishiriki ligi hiyo, ambapo nane ndizo zilizoingia hatua ya pili ambazo ni Rwangwa, Tigo, Ruvu JKT, Polisi Pwani, Polisi Arusha, Hamambe ya Mbeya, Alliance One na Tandahimb