Sababu zinazosababisha ndoa nyingi kuvunjia au wanandoa kuishi pamoja pasipokuwa na ushirika wa ndoa ni nyingi, ndoa nyingi zina mvurugano na michepuko ni mingi na wapo wengine wanaishi pamoja lakini hata hawasemeshani, hakuna upendo wala heshima ya ndoa.
Ndoa ni muunganiko wa mume na mke waliopendana na kuamua kuishi pamoja. Baadhi ya sababu zinazosababisha virugu hizi; kwanza ni namna gani mlivyokutana, ni mpango wa Mungu au yalikuwa matakwa yenu?
Wapo watu wanaoana huku tayari wameshachezeana vya kutosha, mbaya zaidi wengine hata kufanya kinyume halafu wanafunga ndoa! Ndoa kama hizi hapatakuwa na heshima ndani ya nyumba kitakachofuata ni kudharauliana na kutoaminiana, heshima na upendo usipokuwepo hata kama mnaridhishana bado shetani atakuwa anawakumbusha ya enzi zile na hivyo kuwafanya kuchepuka.
Wengine ni tabia au malezi aliyokulia, baada ya kuolewa/kuoa anajikuta hana uhuru au kuna matamanio hayapati kwa mwezie na hii inasababishwa na kutembea na wapenzi wengi kabla ya ndoa hivyo unapokuwa na huyo wako unakuwa unataka ladha ile.
Upendo unapopungua kwenye ndoa nalo ni tatizo, ubinafsi na kiburi huchangia sana tatizo hili. Unapokuta wanandoa kila mmoja anawaza kufanya jambo lake, kila mmoja na mipango yake, baba anajenga Mbeya mama anajenga Tanga, inafika sehemu kila mmoja anasahau kuwa wataishi pamoja bali wataachana muda wowote! Kwa hali hii lazima waangalie nje.
Pamoja na yote hayo, waliomshirikisha Mungu tangu mwanzo na baada ya ndoa, maisha yao ni ya mfano, hakuna kuchepuka na upendo wao hudumu mpaka watawaona wana wa wana wao!