Michango ya wabunge, bungeni

balibabambonahi

JF-Expert Member
Apr 5, 2015
14,416
12,511
Kwa siku mbili hizi za Jana na Leo nimepata nafasi ya kufuatilia bunge mubashara toka Dodoma. Nimetazama na kusikiliza lakini ile radha ya bunge haipo kabisa.

Kuna wenye hoja lakini kwa jinsi wanavyoziwasilisha ni kwa kiwango kisichokidhi viwango vya bunge.

Kuna aliyekuwa na hoja ya kuhalalisha pombe za kienyeji lakini uwasilishaji wake uliifanya hoja kuonekana haina mashiko.Eti akalazimika kwenda na vyombo bungeni!.

Ilikuwa ni hoja kuntu lakini ikawasilishwa kwa kiwango cha chini. Kuna mbunge mmoja alishindwa kujua kwamba mbunge akiongea jambo ndani ya bunge ana Kinga kwa mujibu wa ibara ya 100 ya katibu yetu,yeye alienda kumkosoa mwenzake nje ya bunge.

Leo Kuna mbunge wa viti maalumu toka Arusha alipokuwa akichangia, kila baada ya maneno mawili au matatu lazima ataje Mheshimiwa spika.

Kuna yule aliyesema eti tunafundisha kwamba sisi tulitokana na sokwe, akaomba profesa awasaidie mbona hakuna continuation wa manyani na masokwe kuwa binadamu.Hapa nikagundua nadharia ya Evolution haikueleweka.

Nimpongeze Mheshimiwa Kishimba mbunge wa Kahama aliyeomba elimu mbadala, hiyo nadhani ndiyo iliyo hoja ya msingi.
 
Hili la kuomba maelezo eti kwanini hakuna continuation ya manyani kubadilika ndilo limenifanya nizidi kuona wabunge wetu wengi ni vilaza na wavivu wa kutafuta maarifa.

Hoja hii imekuwepo duniani kwa miaka dahali, na kuna maelezo mengi tu ya ufafanuzi wa hoja hii yamekwisha tolewa jambo Evolution ni very complicated and highly debated topic! na kibaya zaidi hawajui kuwa inapoongelewa hii evolution haisemi ni kwa sababu waaAfrika ni weusi inaongelea chimbungo la binadamu wote including hao wazungu, na wala haisemi kuwa Binadamu ametokana Nyani, bali ni kuwa Binadamu na Manyani hasa Chimpanzee wametokana na common ancestor! na ndio maana kijenetiki binadamu anafanana na sokwe kwa 98%!

Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa! Mshikeni sana huyo elimu na wala msimuache aende zake! Itafuteni Elimu hata kama ni Uchina!
 
Hili la kuomba maelezo eti kwanini hakuna continuation ya manyani kubadilika ndilo limenifanya nizidi kuona wabunge wetu wengi ni vilaza na wavivu wa kutafuta maarifa. Hoja hii imekuwepo duniani kwa miaka dahali...
Na theory inaanza na cell zilizokuwa zinakaa kwenyeaji,maji yalipopungua ndo cell Ikatengeneza early mammals.Hizi mammals zikikaa kwenye misitu na zilikuwa na mikia zikifanana na apes wa Leo.

Mabadiliko yakazaa viumbe wa aina mbili ,moja ndo asili ya binadamu na ya pili ndiyo asili ya nyani,chimpanzee nk tunaowaona Leo.Asili ya binadamu siyo nyani bali wote wawili asili yao ni moja.Hii ni historia ya form one.
 
Back
Top Bottom