Michango ya harusi too much

kinshwi

Member
Joined
Aug 22, 2016
Posts
48
Reaction score
173
Wakuu hivi ni namna gani unaweza kuepuka kuchangia harusi hasa hawa wanoomba michango randomly kisa tu ulisoma naye unaamka unajikuta kwenye group na wengine wako na audacity unakuta hadi amount ya mchango ameshakujazia.

Imenilazima kuweka private setting za WhatsApp nisiaddiwe kwenye magroup hovyo lakini bado haitoshi.

Kazini nako unakuta sawa ni staff mwenzio lakini huna personal relationship naye ya aina yoyote na pengine yupo branch ya sehemu tofauti na ulipo na hata hamfahamiani lakini mkeka unawekwa kwenye official group la ofisi ili tu wasiochangia waonekane watu wa ovyo.
 
Kausha tuu sio Dhambi,kuoa sio lazima sherehe ni kwenda Msikitini au kanisani,kwisha kazi!Hii misherehe ni uzushi tuu!
 
Mkuu kuwa muwazi ! Ukiombwa michango sema huna !! Upuuzi huu , mm sichangi kabisa mambo ya harusi sujui sherehe ! Huwezi kukaa kuplani mambo yako uje ushirikishe watu wakusaidie, kama huwezi acha !

Michango muhimu Kama misiba ndo huwa natoa tu
 
Haya mambo yalisha pitwa na wakati, mtu akitaka kufunga ndoa tunamsupport... Lakini akitaka kufanya harusi hizo ni shida zake na nivizuri akajiandaa yeye mwenyewe.
Lakini pia.... kufanya kazi pamoja haimaanishi ninyi ni marafiki ama watu wa karibu, kumbuka kazi ndio imewakutanisha.
Kusoma pamoja haimaanishi ninyi ni marafiki maana daada ya shule kila mmoja aliendelea na maisha yake na wala hamkua na mahusiano kwenye shida na raha.
 
Kama una hela changa,kama huna kaa kimya
 
Kuna wengine hata hauwafahamu ila kisa unafahamiana na anaowafahamu anakuja kukubwagia kadi ya mchango
 
Shida sio michango bali ni michango isiyo rafiki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…