Michango kwenye makundi ya WhatsApp

J C

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2013
Posts
3,139
Reaction score
2,635
Wadau hili limekaaje unatakuta wameku add kwenye group la shule ya Msingi, Sekondari, Chuo, Ukoo, Mtaa, La Nzengo, La Ofisini N.k.

Sasa kivumbi kinakuja zinapostiwa nyuzi za watu kufiwa na kufa. Daftari linaanza kupita la mchango kwa picha ya marehemu kuwekwa juu kabisa. Hili limekaaje wadau?

Ni jinsi gani unaweza kuhimili hii michango? Nina uhakika gani kuwa nami nikiweka picha ya marehemu nitaweza kuchangiwa kama wenzangu nilivyowachangia?

Karibu kwa mchango wa kimawazo.
 
Mkuu unataka tukwambie nini cha kufanya? Mbona ni rahisi sana.
 
Reactions: J C
Since nianze kutumia WhatsApp ni magroup mawili tuu ndo niliyounganishwa, chuo na 0'level classmates. Sijawahi kukutana na hayo ya ukoo, office nk.bt mshua namsikiaga analalamika kuhusu michango ya harusi na vifo kwenye hayo magroup hadi anataman kuleft ila anachohofia ni kutengwa cz ukisoma group description zao unaweza kudhani hawa watu sio ndugu kwa jinsi sheria zilivyo za kibabe 😁...😂
 
Reactions: J C
Mimi huu upuuzi ndo siutaki. Kwanza huwa najiambia bila whatsapp kila mtu angekuwa kivyake. Hii WhatsApp group ni kutiana umasikini tu. Watu tuliosoma wote primary group la nini. Inshort sina group la msingi mpaka chuo. Hata la kazini simo. Nilishawahi kuadiwa kipindi kile unaadiwa tu bila idhini yako.

Nili left. Mara mtu niliemaliza nae form six eti kazaa mchango. Kwanza sitaki kudweli kwenye past. I prefer physical contacts. Mtu hatujaonana miaka 10 eti kajifungua umchangie. Binafsi nikijifungua wala sifikirii mtu tuliesoma wote chuo yupo Katavi huko eti anichangie.
 
🤣😂
Na mkome wasapu wasapu mnajiunga mavitu mengine hamjui hata ya kazi gani nawe umo tu ndo mpambane na hali zenu..😎
 
Reactions: J C
Word

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bila kupepesa macho, wewe ni antisocial
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…