Michael Satta Aanza Kuwatesa Wananchi Wake, ZAMBIA.

Michael Satta Aanza Kuwatesa Wananchi Wake, ZAMBIA.

B.G TANTAWI

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
496
Reaction score
379
Mageuzi ni muhimu sana lakini mageuzi hayo hayo yanaweza kuleta machungu kwa wananchi, Rais wa Zambia Michael Sata alikuwa mpinzani, alipambana sana na chama tawala ili kuweza kuingia Ikulu katika Uchaguzi mkuu, lakini ni majuzi tu hapa ndipo alishinda.

Sasa wananchi wake wameanza kulalamika, kwanza anaminya demokrasia, hataki vyama vya siasa vimkosoe kwa kumkumbusha kuhusu ahadi zake. Sasa wananchi wake hawana imani tena na Serikali yao.

Wakati mwingine mabadiliko ya Utawala katika Nchi ni hatari sana, unaweza kusema angalau chama kile kingekuwepo tu.

Source, BBC. LONDON.
 
Ni kama chama kimoja nchini kinachojiita cha demokrasia lakini hawafanyi uchaguzi mpaka eti chama kiwe imara. Watu wa namna hiyo ukiwapa nchi lazima ujute.
 
Mdomo huuuhuuuu uliponza Baba nanihiii juzijuzi, aliongea vapour mbele ya wanaume
 
mkuu kuna wale majamaa wakija kushika nchi, tutaambiwa watu wote tulale maana jamaa wanapita na msafara wao..
 
Issue ya Zambia inakuwaje source iwe bbc london.Napata picha ya ukoloni mamboleo.go sata goo
 
Hii ni sawa na kusema ugumu wa maisha unaowakabili wananchi kwa sasa ni heri tusingedai uhuru kwa wakoloni. Hizi ni fikra potofu sana mkuu, je huyo rais toka aingie madarakani ni miaka mingapi sasa? Ikiwa TZ baada ya 50 yrs ya uhuru bado kuna wananchi wanaishi kwenye nyumba za nyasi, hakuna zahati jirani, shule duni, hakuna maji n.k unadhani itawachukua watawala wapya miaka mingapi kubadili mfumo mpya ulioota mizizi kwa zaidi ya nusu karne? mwisho ni mawazo ya ajabu sana kufikiri kwamba ni bora usidai mabadiliko kutokana na maisha duni ya sasa kwa hofu kwamba unaweza usifanikiwe!! Ndiyo maana kuna msemo: WOGA WAKO NDIYO UMASIKINI WAKO!!
 
biology inakuambia kila kitu kina madhara hapa duniani, madhara yanapokuwa mengi kuliko faida basi hicho kitu huwa sumu na hakifai, ila madhara yanapokuwa machache sana kuliko faida, hicho kitu kinafaa kwa matumizi. maana yake ni kuwa hakuna kitu au mwanadamu aliyekamili hata obama wapo wanaona hafai.
 
Kama ndivyo usemavyo jiulize swali hili"kwanini iliwekwa/imewekwa/inawekwa "mifuto(corection pen/fluid) darasani,maofisini au hata nyumbani kwako?"nijibu tafadhari.
 
Hii ni
sawa na kusema ugumu wa maisha unaowakabili wananchi kwa sasa ni heri
tusingedai uhuru kwa wakoloni. Hizi ni fikra potofu sana mkuu, je huyo
rais toka aingie madarakani ni miaka mingapi sasa? Ikiwa TZ baada ya 50
yrs ya uhuru bado kuna wananchi wanaishi kwenye nyumba za nyasi, hakuna
zahati jirani, shule duni, hakuna maji n.k unadhani itawachukua watawala
wapya miaka mingapi kubadili mfumo mpya ulioota mizizi kwa zaidi ya
nusu karne? mwisho ni mawazo ya ajabu sana kufikiri kwamba ni bora
usidai mabadiliko kutokana na maisha duni ya sasa kwa hofu kwamba
unaweza usifanikiwe!! Ndiyo maana kuna msemo: WOGA WAKO NDIYO UMASIKINI
WAKO!!

hii hoja ilitosha kufunga mjadala, safi sana mkuu
 
Back
Top Bottom