Miamba dhoofu chanzo cha maporomoko Hanang

TAJIRI MKUU WA MATAJIRI

JF-Expert Member
Dec 1, 2010
5,947
10,809
SERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa una miamba dhoofu iliyonyonya maji ndio chanzo cha maporomoko yaliyoleta maafa katika eneo hilo la Hanang mkoani Manyara.

Maporomoko hayo ya matope yamesababisha vifo vya watu 65 na majeruhi zaidi ya 100 huku mamia ya wanachi wilayani Hanang wakipoteza mifugo, mashamba na makazi yao kwa ujumla.

"Sehemu iliyonyonya maji ilizua mgandamizo na sehemu ya Mlima ikashindwa kuhimili mgandamizo na hivyo kusababisha kumeguka kwa sehemu hiyo na kutengeneza tope ambalo ndio lilianza kuporomoka kufuata mkondo wa mto Jorodom uliozoa mawe na miti na kushambulia makazi ya binadamu yaliyokuwa pembezoni mwa mto huo," - Msemaji wa Serikali, Mobhare Matinyi
 
Kamati ishakula fungu lake (Pesa) , na sasa ni muda wa kutupa taarifa.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Labda serikali ya CCM inadhani ni CHADEMA walikwea juu ya mlima Hanang na kuachilia tope na maji hata kusababisha maporomoko (landslide) na kuleta maafa ya vifo na uharibifu wa mali..

Yaani hii serikali chini ya CCM itafika wakati watakuja kuunda tume ya uchunguzi ili kuchunguza kwanini jua huwa linachomozea mashariki na kuzamia magharibi...
Screenshot_20231205-233604.png


Yaani serikali na viongozi waliochoka, utawajua Kwa matendo yao tu. Yaani PM amesahau kabisa kuwa TMA walishatoa onyo kupitia utabiri wa hali ya hewa kuwa Kuna mvua kubwa zinakuja na watu wanaoishi maeneo hatarishi wachukue tahadhari..
 
Sawa,lakini ingefaa angesikia eye-witness reports.

"Ile haikuwa mvua. Ile ilikuwa sijui ni kitu gani"

"Mto wa matope ulikuja. Pembeni kulikuwa kuna vitu vinang'aa,sijui ni vitu gani".

"Nipo hapa toka 1956. Ile haijatokea. Ile ilikuwa volcano."

Huyu mtaalamu angeoanisha maneno yake na hizi eye-witness reports.
 
Back
Top Bottom