Miaka 61 bila huduma ya maji Dar es Salaam

mapesa yamejaa

JF-Expert Member
Dec 29, 2021
1,412
3,403
Kipindi stendi kuu ya mabasi Mbezi inafunguliwa na mzalendo namba moja wa karne ya 21 Mh dk John Pombe Joseph Magufuli alitoa maelekezo ya kwamba barabara kutokea stendi hiyo kwenda mpigi magoe ianze kujengwa kwa kiwango cha lami pamoja na maji yapelekwe huko jimbo la kibamba lote

Na kweli kesho yake tu pilikapilika zikaanza.

Magari yakawa yanapishana tayari kwa ujenzi. Dawasa nao hawakuwa nyuma. Mabomba yakaanza kutandazwa sehemu mbali mbali za jimbo la kibamba kuelekea maeneo ya mbezi misumi,msakuzi na mpigi magoe ambako watu hawajawahi kuona maji toka Nchi ipate uhuru mwaka 1961.

Bahati mbaya haikuchukua mda mrefu mzalendo katutoka.zile shughuli zilizokuwa zinaendelea zikaanza mwendo wa kobe na hatimaye zikafa kabisa hadi leo watu wa kibamba maeneo ya Mpigi Magoe, Msakuzi na kwingineko huduma hizi wanazisikia tu. Inawalazimu kununua maji kwenye visima vya watu binafsi kwa unit shilingi 5000-6000 kwa usawa huu kweli?

Hivi ninyi viongozi mliopewa dhamana mnataka tuwasimamie kwa mijeredi ndo mpeleke hizo huduma? Kama pesa hazitoshi muuze hizo V8 zenu mnunue Vitz. Haiwezekani huduma hizo muhimu zikosekane ndani ya jiji la kibiashara Dar es Salaam. Wananchi tunataka maji, hatutaki V8.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maisha ya mtanzania ni taabu na mateso mpaka mwisho wetu

Haikuwa na haja ya late magu kuwaaambia nni cha kufanya la msingi ni kuwa na mpango mkakati wa muda mrefu na mfupi kwa ajili ya watanzania

Haina haja ya kutegemea hisani ya mtu wala matakwa binafsi zaidi ya kuwa na mpango mmaridhawa
 
mtag Bimkubwa! huwa naona kama ni mzungu flani na msikivu ati!

hivi Her Excellency Mama Samia kuhudhuria birthday ya usiku wa manane ya Sugu ni muhimu kuliko kutembelea kukagua ukosefu wa maji na barabara huko Mbezi kwenu??

mbunge na Diwani wenu chama gani? tuanzie hapo kwanza!
 
Hiyo barabara ni mradi wa watu kupiga pesa kila baada ya miezi kadhaa.
Mimi ni victim wa haya yote

Naishi Mbezi Makabe mwaka jana mwanzoni nilifunga bomba tena kwa gharama kubwa maji yakatoka kama miezi mitatu mfululizo kufika mwezi August ukaanza mgao hadi napoandika hapa maji hayatoki ukiuliza sababu kwanini hayatoki huambiwi wapumbavu Dawasa wamehongwa na wenye Canter za kuuza maji kwa madumu ili wauze maji,hilo la barabara hizo za jimbo la ubungo stuff wa halmashauri kupitia TARURA na TANROAD ndo wanakopigia hela.

Tujiulize,leo TMA wakitoa utabiri wa kunyesha mvua kubwa Dar kesho grader zinaingia site kuchonga barabara ikija kunyesha hiyo mvua barabara zote zinavurugika so wanakuwa wanajua kabisa awamu hii ya mvua tukichonga barabara hii mpaka mvua ije kukata itakuwa haifai tena so tumeshachukua fungu tukae tena tukisubiri msimu unaokuja kama wana nia nzuri kwanini wasizichonge kipindi hiki cha kiangazi?

Mbunge amekaa kimya hatumsikii hata akikohoa huko bungeni angalao angezungumzia hili la wizi wa pesa za umma kuchonga barabara zinazoharibika hata vifaa vya kazi havijatoka site.
 
mtag Bimkubwa! huwa naona kama ni msikivu ati!

hivi Her Excellency Mama Samia kuhudhuria birthday ya usiku wa manane ya Sugu ni muhimu kuliko kutembelea kukagua ukosefu wa maji na barabara huko kwenu??

mbunge na Diwani wenu chama gani? tuanzie hapo kwanza!
Hakuna kitu hapa tukubali tumepigwa na kitu kizito tena chenye ncha!
 
Jamaa miyeyusho sana, wanaharibu barabara makusudi.

Kwny ishu ya maji Dawasa wana mabomba ila unaambiwa hayatoshi inabidi ununue na wakikuwekea maji hayatoki pia.
 
Kipindi stendi kuu ya mabasi Mbezi inafunguliwa na mzalendo namba moja wa karne ya 21 Mh dk John Pombe Joseph Magufuli alitoa maelekezo ya kwamba barabara kutokea stendi hiyo kwenda mpigi magoe ianze kujengwa kwa kiwango cha lami pamoja na maji yapelekwe huko jimbo la kibamba lote

Na kweli kesho yake tu pilikapilika zikaanza.

Magari yakawa yanapishana tayari kwa ujenzi. Dawasa nao hawakuwa nyuma. Mabomba yakaanza kutandazwa sehemu mbali mbali za jimbo la kibamba kuelekea maeneo ya mbezi misumi,msakuzi na mpigi magoe ambako watu hawajawahi kuona maji toka Nchi ipate uhuru mwaka 1961.

Bahati mbaya haikuchukua mda mrefu mzalendo katutoka.zile shughuli zilizokuwa zinaendelea zikaanza mwendo wa kobe na hatimaye zikafa kabisa hadi leo watu wa kibamba maeneo ya Mpigi Magoe, Msakuzi na kwingineko huduma hizi wanazisikia tu. Inawalazimu kununua maji kwenye visima vya watu binafsi kwa unit shilingi 5000-6000 kwa usawa huu kweli?

Hivi ninyi viongozi mliopewa dhamana mnataka tuwasimamie kwa mijeredi ndo mpeleke hizo huduma? Kama pesa hazitoshi muuze hizo V8 zenu mnunue Vitz. Haiwezekani huduma hizo muhimu zikosekane ndani ya jiji la kibiashara Dar es Salaam. Wananchi tunataka maji, hatutaki V8.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ccm ni mafiiii
 
Mabomba ndio yameanza kuwekwa sasa.... Na wakazi wameanza kusainishwa form...

But hii ndio BONGO,, na hizo ndio FLEVA zenyewe... Bongo Fleva
 
Mabomba ndio yameanza kuwekwa sasa.... Na wakazi wameanza kusainishwa form...

But hii ndio BONGO,, na hizo ndio FLEVA zenyewe... Bongo Fleva
Siyo kila sehemu mkuu,area ninayoishi mimi maji yalikuwa yanatoka ni hujuma wanafanya wapemba na wachagha wenye vi-Canter vya maji ya madumu kuhonga engineers wa Dawasa wasifungue maji ili wao watuuzie na madumu yao machafu.

Nime-plan kuchimba kisima nivune maji ya mvua tu maana nchi hii hakuna mtetezi zaidi ya kuishi jinsi hali inavyotaka.
 
Back
Top Bottom