Mhe Sitta, Utaweka wapi sura yako?

Mhe Sitta, Utaweka wapi sura yako?

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,410
Reaction score
14,119
Uchu wa madaraka unapopitiliza kwa kujaribu hata kukwepa matakwa ya wananchi wenyewe waliowaweka wanansiasa madarakani, mwisho wake ni aibu.

Mh Sitta pamaoja na sifa yake ya "Speed and Standards" lakini spidi ya safari hii ilikuwa inaeleekea kuzimu.
Pamoja na maoni ya Tume ya Warioba , ambayo ni maoni ya wananchi, juhudi nyingi zimewekwa kuyaondoa maoni hayo na kuweka maoni ya wanasiasa.


Pamoja na UKAWA kuwa ni wa vyama vya upinzani, lakini katika hili wameonyesha kidogo uzalendo wa kupigania maoini ya wananchi.
Pamoja na hili tunamshukuru Mh JKikwete kwa kuliona hili ili nchi isiingie mtafaruku usio wa lazima.
Hata wana CCM kama Mwigulu Nchemba waliliona hili na mapema.

Hivyo basi ni aibu iliyoje kufikia sasa kuwa hela ya kodi za wananchi imeliwa , na muda mrefu sana umetumika na hakuna cha maana cha kuonyesha kwa matumizi haya ambayo yangeepukwa kwa kutikia maanani maoni ya wananchi.

Maoni ya wananchi mengi sana hayakuwa kichama wala kidini wala kwa manufaa ya kikundi chochote.
Ni mategemeo yetu kuwa walioshinikiza kuendelea na mchakato mufilisi wawajibike kisheria au kisiasa kwa hili.

Na Benedict Luhenga,MAELEZO Dodoma
VIONGOZI Wakuu wa Vyama vya siasa vyenye Wabunge
vinavyounda Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) wamekuwa katika mashauriano ya
zaidi ya mwezi mmoja tangu tarehe 2 Agosti mwaka huu huku wakishauriana juu ya
mwenendo wa mchakato wa Katiba Mpya na jinsi ya kuwa na uchaguzi ulio huru na
wa haki hapo mwakani

Akiongea kwa niaba ya viongozi wengine wa kituo hicho,
Mwenyekiti wa TCD, Mhe. John Cheyo amesema kuwa Katika mashauriano hayo
yaliyochukua sura ya Kamati ya Makatibu Wakuu, Kamati ya Wenyeviti wa Vyama vya
CCM, CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi katika hatua tofauti.

Mhe. Cheyo ameeleza kuwa kamati zote zilitoa taarifa
zao kwenye vikao vya Viongozi Wakuu wa Vyama (Summit) ya TCD ambayo wajumbe
wake ni Wenyeviti, Makamu Wenyeviti na Makatibu Wakuu wa Vyama wanachama.

< Mhe. Cheyo aliongeza kuwa katika kutafuta maridhiano,
Wenyeviti na Makatibu Wakuu wa Vyama walifanya mashauriano na Mhe. Rais Dkt.
Jakaya Mrisho Kikwete siku ya tarehe 31 Agosti mwaka huu, hivyo tarehe Nane
Septemba, 2014 hapa Dodoma wakatoa tamko lao

Pamoja na kazi ya msingi inayofanywa na Bunge Maalum
la Katiba, mchakato wa Katiba unaoendelea sasa hauwezi kutupa Katiba
itakayotumika katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwa kuwa muda hautoshi kukamilisha
mchakato na kufanya mabadiliko yatakayohitajika ya Sheria, Kanuni na Taasisi
mbalimbali zitakazohitajika", alisema Mhe. Cheyo

Mhe. Cheyo aliendelea kwa kusema kuwa, kwa mujibu wa
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba mwisho wa mchakato ni kura ya maoni
itakayofanyika mwezi Aprili 2015

"Kama itabidi kura irudiwe kwa mujibu wa Sheria
iliyotajwa, kura itarudiwa mwezi Juni au Julai 2015, muda ambao Bunge la Jamhuri
ya Muungano linatakiwa livunjwe kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba 2015 na
ili Katiba Mpya itumike katika uchaguzi Mkuu utakaokuja, itabidi uhai wa Bunge
na Serikali uongezwe zaidi ya 2015, jambo ambalo hatuliungi mkono", alisisitiza
Mhe. Cheyo.
Akiongelea juu ya Tangazo la Serikali GN Na 254, Mhe.
Cheyo amesema kuwa Bunge Maalum la Katiba kwa sasa linafanya kazi kwa mujibu wa
Tangazo la Serikali (Government Notice) Na 254 lililotolewa na Mhe. Rais
Kikwete tarehe 1 Agosti, 2014

"Tangazo hilo litatumika hadi tarehe 4 Oktoba, 2014
ambapo Katiba inayopendekezwa inategemewa kupatikana, Wajumbe walikubaliana
hatua hii iachwe ifikiwe", alisema Mhe. Cheyo

Kuhusiana na Kura ya maoni, Mhe. Cheyo ameeleza kuwa
kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba baada ya Bunge hilo kumaliza
kutunga Katiba, ingefuata hatua ya kura maoni kuthibitisha Katiba

"Kwa kutambua kuwa hatua ya kura ya maoni italazimisha
uchaguzi mkuu 2015 kualishwa, basi hatua hii iailishwe, na mchakato wa Katiba
uendelee baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2015", alisema Mhe. Cheyo

Sambamba na hayo, Mhe. Cheyo ameishauri Serikali
kuchukua hatua za kisheria ili matayarisho kwa ajili ya Uchaguzi wa Vijiji,
Vitongoji na Mitaa, yaanze haraka iwezekanavyo ili uchaguzi ufanyike mapema
hapo mwakani

Aidha, amegusia kuhusu Mabadiliko ya 15 ya Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 akasema kuwa, kwa vile Uchaguzi Mkuu wa
2015 utafanyika kwa kutumia Katiba ya 1977, kuna umuhimu kufanya mabadiliko
kidogo (minimum reforms) katika Katiba pamoja na sheria ya Uchaguzi
yatayowezesha nchi kufanya uchaguzi huru na wa haki

"Tayari mambo yafuatayo yamekubaliwa, kuwa na Tume
Huru ya Uchaguzi kusimamia uchaguzi, Mshindi wa Uchaguzi wa Rais ashinde kwa
zaidi ya asilimia 50% (50%+1)", alisema Mhe. Cheyo

Viongozi hao Wakuu wa Vyama wamempongeza Mhe. Rais
Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa ujasiri wake na imani yake katika kuimarisha
demokrasia nchini na kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba Mpya ya nchi.
 
Mpaka sasa SITTA ameibuka kidedea, unachokifanya ni kutapatapa, hivi kama TCD na JK wamekubaliana bunge liendelee mpaka oktoba 4 , nani mshindi?
 
Sasa km mchakato utahairishwa hao mbuzi huko dodoma wanaendelea kujadili nini yaani njaaa mbaya 'hicho wanachojadili kitatupwa na mchakato utaanza upya kwa sheria mpya kwa kuwa makosa yameonekana ni kujaza wanasiasa na kugeuza bunge la jmhuri kuwa la katiba sasa wanajadili nini hao mbuzi waliobaki mjengoni
 
Imekuaje leo mwanaCCM unakubaliana na UKAWA au hii sredi kuna mtu ameandika kwa niaba yako?
 
Ataificha sura yake kwa mkewe na familia yake tu.
 
Mbona anazungukazunguka? Toboa bungw limehailishwa mpaka 2016 back.hao weu watoke huko ddm haraka
 
Pigo siyo kwa Sitta maana yeye alipewa maelekezo kasimamie moja, mbili, tatu.........hicho kikundi kilichotoa maelekezo ya mpaka Raisi afungue Bunge baada ya Rasimu kuwasilishwa na kufutilia mbali tovuti ya Tume ingefaa hiyo majina yao yawekwe wazi ili Watanzania wawafahamu.

Mimi wa kwanza ni Waziri wa Katiba na Sheria - Asha Rose Migire, Tovuti iko wizarani kwake
 
Mpaka sasa SITTA ameibuka kidedea, unachokifanya ni kutapatapa, hivi kama TCD na JK wamekubaliana bunge liendelee mpaka oktoba 4 , nani mshindi?

Mkuu hii ni sheria uliyounda bunge hilo ambayo inaweza kutenguliwa tu na mahakama au BJMT...Aidha Sitta kwa kutumia mawazo yake mgando aliomba hadi tarehe 29 october eti awe amemaliza kazi yote ya katiba ibaki kura ya wananchi! Huu uwehu wa ajabu hivi ndo Sitta alikuwa ameujaza kichwani mwake!!!
 
Mpaka sasa SITTA ameibuka kidedea, unachokifanya ni kutapatapa, hivi kama TCD na JK wamekubaliana bunge liendelee mpaka oktoba 4 , nani mshindi?[/QUOTE


stupid, unachekelea kodi yako kuliwa Kama sad aka? Sad
 
Mpaka sasa SITTA ameibuka kidedea, unachokifanya ni kutapatapa, hivi kama TCD na JK wamekubaliana bunge liendelee mpaka oktoba 4 , nani mshindi?

Ila umburula mwingine inamaana wewe huelew tu,? unafkria kwa kutumia nn mkuu? Hata bondia hupgwa na kuanguka chini mara kadhaa nakuumia lakini refaree akimuuliza unaweza kuendelea hukubali kuendelea hata kama anajua kabisa keshapgwa na hata ajitahid vip hawez kushnda. Ndvyo yanavyofanya maccm hayatak yaonekane yamechemka.
 
Halooo me mbona kama sielewi hilo azimio aiseeeee,
Kama wamekubaliana vikao vya BMK kuendelea mpaka Octoba 4, then mchakato uhairishwe mpaka baada ya uchaguzi mkuu hapo mwakani
Nini cha maana wananchi tulichokivuna kwenye mazungumzo ya Kikwete na TCD, ikiwa kinachoendelea sasa bungeni sio mjadala unaotokana na rasimu iliyoandaliwa na Tume ya Warioba?

Kama BMK itaendelea mpaka ipatikane katiba iliyopendekezwa, je hiyo si itakuwa batili kwa mujibu wa UKAWA?
Si itakuwa haijatokana na rasimu ya pili iliyoandaliwa na Tume ya Warioba!

Kama UKAWA wamekubali hili, ni wazi wametusaliti sisi wananchi ambao tulikuwa tunasapoti msimamo wao; pia hakukuwa na umuhimu wowote wa wao kususia vikao, ilhali wanakubali kile kitakachozalishwa na mijadala waliyoisusia?

NIMECHANGANYIKIWA HAPA!
 
Sitta mjanja,,baada ya kuikoroga CCM si atajirudia tu ktk chama chake cha CCJ yeye na wenzake akina Nape, Kirango nk&#8230;kwa hiyo hapa walioumia ni CCM na wananchi ndio zaidi
 
Ni kweli Sita aliingizwa mkenge,mkuu wa kaya ndiye chanzo cha sakata lote hili,na sasa watu wanampongeza kwa kitu ambacho alijua mwisho wa siku kitakwama na yeye ndiye mkwamuaji,watanzania fungueni macho
 
Its a BIG SHAME TO HON. MZEE SITTA.
Afu naona vibaya au ndo ilivo kuwa kaishaanza KUINAMA?
 
Mkuu hii ni sheria uliyounda bunge hilo ambayo inaweza kutenguliwa tu na mahakama au BJMT...!
Kama ulimsikiliza vizuri Humphrey Polepole katika lile bandiko la "Nilichosema kuhusu katiba chanel 10). utakuwa umegundua kuwa Rais anweza kufuta uteuzi wa wajumbe wote wa BMK kwa kuwa ndiye aliyewateua (mwenye mamlaka ya kuteua ana mamlaka pia ya kutengua) Na rais akiamua kutengua basi kunakuwa hakuna wajumbe; na BMK linakufa kifo cha ghafla!
Bandiko hilo ni https://www.jamiiforums.com/katiba-...channel-10-television-juu-ya-katiba-mpya.html
 
Halooo me mbona kama sielewi hilo azimio aiseeeee,
Kama wamekubaliana vikao vya BMK kuendelea mpaka Octoba 4, then mchakato uhairishwe mpaka baada ya uchaguzi mkuu hapo mwakani
Nini cha maana wananchi tulichokivuna kwenye mazungumzo ya Kikwete na TCD, ikiwa kinachoendelea sasa bungeni sio mjadala unaotokana na rasimu iliyoandaliwa na Tume ya Warioba?

Kama BMK itaendelea mpaka ipatikane katiba iliyopendekezwa, je hiyo si itakuwa batili kwa mujibu wa UKAWA?
Si itakuwa haijatokana na rasimu ya pili iliyoandaliwa na Tume ya Warioba!

Kama UKAWA wamekubali hili, ni wazi wametusaliti sisi wananchi ambao tulikuwa tunasapoti msimamo wao; pia hakukuwa na umuhimu wowote wa wao kususia vikao, ilhali wanakubali kile kitakachozalishwa na mijadala waliyoisusia?

NIMECHANGANYIKIWA HAPA!
Umepewa nafasi ya kufanya uchaguzi na kupata wajumbe wapya kwa bmk lijalo. Ni juu yako kuwaondoa hao waliopindisha mawazo ya wananchi na kuweka ya kwao. Hii ni fursa nzuri - tuitumie.
Usisahau pia kuwa tutakuwa na rais mwingine ambaye si lazima aje na mawazo kama ya JK. Kumbuka mbunge mmoja aliwahi kusema " anayeshikila nguvu za dola (instruments of power) ndiye mwenye uwezo wa kusema katiba mpya iwepo na ikawa au sitaki katiba mpya na ikawa. Alitoa mfano wa Afrika ya kusini
 
Ni kweli Sita aliingizwa mkenge,mkuu wa kaya ndiye chanzo cha sakata lote hili,na sasa watu wanampongeza kwa kitu ambacho alijua mwisho wa siku kitakwama na yeye ndiye mkwamuaji,watanzania fungueni macho

Sita kama mwanasesere tu!
 
Back
Top Bottom