Umeandika uliojaaliwa kheri kwako.Ila kuna mengi yaakupasa ujifunze kwa sababu wapo waliowahi kufikiri na kuandika kabra mfano shabani Robert ameandika mengi ambayo yangetekelezwa tungeweza kuwa mbali hujayajumuisha,Profesa Shayo amewahi andika kuhusu kuanzishwa kwa kijiji cha sayansi na teknolojia.
Elimu ni fumbo ambalo waafrika tumeshindwa kulifumbua hivyo linahitaji mjadala na sio mtazamo wa mtu mmoja au kikundi cha waunda mtaala/ Sera ambao wengi wao wamechoka kifikra.
Elimu inataka demokrasia na sio jambo la kuwekwa mikononi nwa watu wachache hivyo jamii inatakiwa ishiriki kujiundia mfumo wa elimu kulingana na mahitaji ya sasa na baadae.
Afrika tunakosa kitu kujitambua na kujiamini.tumerithi mifumo,mmojawapo ni wa chama, ukijiunga kazi yako ni kuutetea, hali hii imedumaza fikra pingamizi.Kwa hio hakuna nawazo mbadala yanayokubarika na kufanyiwa kazi bali ya kikundi.
Waafrika tumetafsiri vibaya dhana ya serikali,mtu akiwa kiongozi anajipa mamlaka ya kufikiri kwa niaba ya wengi na kujiona anaakili kuliko anaowaongoza, hii ilianza zamani.