Ualimu ni sehemu nyeti huwezi kulinganisha na sehemu ulizozitaja.Wote uliowataja wanatokana na mwalimu, hivyo mwalimu akiwa mbovu kila kitu kinakuwa kibovu.Mhe. Bashe kwanza hongera sana kwa kuingia bungeni baada ya kufanyiwa figisu nyingi 2010 na hatimaye ukaenguliwa eti wewe si mtanzania. Na kwa kipindi kifupi tu jina lako limeanza kuingia vichwani mwa watanzania wachache wanofuatilia bunge manane ya usiku.
Nakuja hapa kukutaka utengue kauli yako iliyonukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari kwamba "ualimu ni kichaka cha waliofeli". Binafsi sijakusikia wala kukuona moja kwa moja kwa kuwa hilo bunge lenu linalooneshwa manane ya usiku wala sina habari nalo. Lkn kwa kuwa hujakanusha nukuu hii iliyoenea katika vyombo vyote vya habari bila shaka uliitoa kauli hii.
Kauli hii inawezekana uliitoa kwa dhamira njema kabisa lkn hukufikiria madhara yake kwa ualimu na walimu. Maana inatweza na kudhalilisha ualimu na walimu. Kwa mtu wa hadhi yako unayesifika kuwa mwanasiasa machachari unayechipukia unapaswa kuwa makini kabla ya kufungua kinywa chako.
Jiulize maswali yafuatayo mhe. Bashe.
1. Kufeli maana yake nn?
2. Taasisi nyingine za serikali hakuna waliofeli?
Elimu ni uwezo wa kutambua na kupambana/kukabiliana na changamoto zilizopo ktk mazingira. Anaye elimika anapaswa kuwa huru kifikra na kiuchumi.
Kimsingi elimu ktk taifa letu haimpi msomi ujuzi na uwezo wa kutambua na kupambana na changamoto zinazomzunguka. Tumeshuhudia mkuu wa mkoa aliyekuwa mstari wa mbele kuhimiza vijana wajiajiri akilia njaa baada ya kuondolewa kwenye nafasi hiyo.
Yawezekana hata wewe Bashe unajiona mwenye kufaulu kwasabb tu umepata ubunge. Nje ya ubunge huna mbinu ya kupata mlo au kuendesha maisha
Tunaona maprofesa wakililia mikataba ya kuendelea na kazi hata baada ya kufikia umri wa kustaafu. Hii ni ishara tosha kuwa hawana ujuzi na uwezo wa kupambana nje ya ajira.
Lkn kama taasisi nyingine zina waliofaulu. Inakuwaje walimu waliofeli wakaingia kwenye ajira ili hali mifumo ya kuajiri serikalini imeshikwa na walioelimika??
Mhe. Bashe ulikuwa too specific katika kauli yako. Ingekuwa vema ungesema "serikalini ni kichaka cha waliofeli".
-bungeni hakuna waliofeli?
-polisi hakuna waliofeli?
-mahospitalini hakuna waliofeli?
- jeshinini hakuna waliofeli?
- wizarani hakuna waliofeli?
-tra, pccb, ewura, n.k hakuna waliofeli huko?
Nionavyo mm watanzania wote wamefeli. Ndiyo maana hata chama chako kikakuzushia kashfa zisizo na miguu kuwa wewe ni msomali ili tu usiwe mbunge. Waliofaulu wanaweza kufanya hivyo?
Lkn waliofaulu wamefanya nn ktk nchi hii? Mm naona kuna walioenda shule na kupata vyeti tu. Ndiyo maana nchi ina kila kitu halafu umaskini umekithiri. Mpk leo nchi inaagiza vijiti vya kuchokonolea meno!!!? Hao waliofaulu wako wapi?
Majengo, yanaanguka hovyo, miji yetu yote haijapangwa, viwanda vinakufa kuna waliofaulu kweli. Kuna watakao kuja na majibu ya watunga sera na sheria. Hawa pia wamefaulu??
Daah!! Niishie hapa.
Wako Kigodoro.
Sina hakika Mkuu. Ngoja waje.Ualimu ni sehemu nyeti huwezi kulinganisha na sehemu ulizozitaja.Wote uliowataja wanatokana na mwalimu, hivyo mwalimu akiwa mbovu kila kitu kinakuwa kibovu.
Let us face the reality! Kuna mwanafunzi aliyepata division 1 or 2 (nadhani hata three??????) akaenda ualimu?
Kigodoro una uhakika nadhani. Form five huwa wanachukua div 1 and 2. Rarely div 3. Fanya homework kidogo. Angalia majina ya wanaokwend ualimu na tafuta pass zao NECTA (siku hizi wanaweka namba, tafuta ya zamani before Exam number system) utauona ukweli. Shule za binafsi wanafuatilia matokeo ya form 4 na six, kama div 4 hawakuajili!Sina hakika Mkuu. Ngoja waje.
Ualimu ni sehemu nyeti huwezi kulinganisha na sehemu ulizozitaja.Wote uliowataja wanatokana na mwalimu, hivyo mwalimu akiwa mbovu kila kitu kinakuwa kibovu.
Let us face the reality! Kuna mwanafunzi aliyepata division 1 or 2 (nadhani hata three??????) akaenda ualimu?
Kwa lipi mkuu ?Hueleweki
2006 nilipata Division One nikachagua kusoma elimu Chuo Kikuu. Ninaipenda fani hii kwani kwangu mimi ni maisha na ndiko ninakopata riziki yangu ya kila siku. Ni upumbavu mkubwa sana kuwadharau walimu wako.Ualimu ni sehemu nyeti huwezi kulinganisha na sehemu ulizozitaja.Wote uliowataja wanatokana na mwalimu, hivyo mwalimu akiwa mbovu kila kitu kinakuwa kibovu.
Let us face the reality! Kuna mwanafunzi aliyepata division 1 or 2 (nadhani hata three??????) akaenda ualimu?
Sekta zingine- Take note hata jeshini wanakwenda waliofeli (sijui siku hizi). Lakini jeshini wana utaratibu wa kuingia kule siyo free kama kwa walimu. Hivyo attention ya jamii haiko huko kwa vile hakuna direct impact kwa mtu wa kawaida. Pili umuhimu wa sekta yenyewe. Huu ni uhai wa taifa kwa kila nyanja even at individual level. Mzazi anataka mtot wake aelimike apate kazi nzuri. Shule za kata wote (???) wanafeli! Lazima watu wapige kelele!Mkuu ngoja niulize kidogo hapa. Kinachofanya ualimu uwe kichaka ni ule umuhimu wa sekta yenyewe, lkn si kwamba huko ndiyo wamejaa waliofeli kuliko sekta nyingine?
Kama jibu lako ni ndiyo kwa swali hili basi tunazungumza lugha moja mimi na wewe.
Kweli, kuna waliofaulu vizuri form six kwa ajili ya ajira na uhaba wa fedha wa wazazi wao wanaamua kusoma ualimu, LAKINI, akimaliza kwa vile pass zake ni nzuri wengi wanatoka!Tatizo letu wengi hatufurahishwi na ukweli,na huwa tunapinga uhalisia.....Ulimuona nani kamaliza kidato cha nne au kidato cha sita mwenye Division 1 au 11 au 111 akaenda kusoma ualimu???? Chunguza,walimu wengi wanaanzia Division 1V ......Na wachache sana wenye ufaulu mzuri huko chuo kikuu waliamua kusomea ualimu ili wapate mkopo......
Hapana sikufundishwa na hao please. Nimemaliza University 1983! Hapakuwa na upuuzi wa sasa. Afterall University ilikuwa moja usingelithubutu kwenda huko bila sifa2006 nilipata Division One nikachagua kusoma elimu Chuo Kikuu. Ninaipenda fani hii kwani kwangu mimi ni maisha na ndiko ninakopata riziki yangu ya kila siku. Ni upumbavu mkubwa sana kuwadharau walimu wako.
Ni sawa na kuzaliwa na mzazi wako, akakuhangaikia katika hatua zako zote za makuzi yako mpaka kufikia hatua ya kujitegemea mwenyewe kisha unaanza kumwona mzazi wako hana thamani yoyote kwako yaani si chochote wala lolote kwako kisa unajua kujitegemea. Ama kweli Tanzania yetu imejaa majuha wengi.
Labda nisaidie jambo moja kama mtaweza kuwapelekea wahusika walifanyie kazi. Ni kwamba elimu ndio moyo na roho ya nchi. Ndio kiwanda cha kutengeneza na kuzalisha bidhaa itokanayo na elimu.
Nchi zinazojua umuhimu wa elimu hazifanyi maigizo tunayofanya. Hao wanarusha satellites anga za mbali watu wao wamesoma na wanathaminiwa sana. Walimu wana heshima ya kutosha. Wanatembea vifua mbele. Watu wengi katika mataifa yao wanatamani kusomea elimu, siyo kama maigizo tunayofanya hapa kwetu.
Hata kama watachukuliwa division four kumbuka ndio hao waliokufundisha mpaka leo unajua kutoa comments kama hizi. Waambie watawala kwamba mfumo wa kutafuta wataalamu wa kutengeneza taifa letu ni mbovu wala sio walimu
Nadhani huyo ni mwalimu anajitetea. Kuna mzazi anaweza kukubali mtoto wake Na div one aende ualimu baadala ya kwenda fomu faivuHueleweki