Mhariri wa Nipashe ana ajenda na kazi maalum

uhindi

Member
Dec 5, 2014
9
4
Kwa miezi kadhaa sasa mhariri wa Nipashe amekuwa akiendesha kampeni maalum na si bila ya maelekezo ya Dkt Reginald Mengi ya kuhakikisha kwamba Profesa sospeter Muhongo ama anafukuzwa kazi au anajiuzulu. Hili la akaunti ya Escrow limekuja tu katika kipindi ambacho tayari kulikuwapo na kampeni maalum ya kumlazimisha kukimbia nafasi yake hiyo.

Hakuna toleo linalotoka bila ya kuwa na habari ya ukurasa wa mbele kumshambulia Profesa Muhongo. Hakuna urazini hata kidogo kwani katika kampeni ya propaganda ambayo lengo lake ni kumng'oa Muhongo kila silaha hutumika.

Kumekuwapo na maelekezo maalumu kutoka kwa Dkt Mengi kwamba gazeti hilo liongoze vita hadi ushindi yaani ushindi wa Nipashe na ITV ni kung'oka kwa Muhongo na asipong'oka vita hiyo ni ya kudumu.

Muhongo kosa lake ni kuwa mkweli tu na kumwambia Mzee Mengi kwamba gharama za kuwekeza katika utafutaji wa mafuta katika bahari ni kikubwa kwa makampuni ya hapa nchini yaani kwa wazawa. Ukweli ambao Bwana Mengi hautaki hata kidogo kuusikia.

Lakini ndiyo ukweli wenyewe kuwekeza katika utafutaji wa mafuta na gesi kwenye bahari bila ya kushirikiana na makampuni ya wenye fedha kubwa si rahisi kwa makampuni ya humu ndani.

Ni vita ambayo Dkt Mengi anataka ashinde kwa njia yoyote ile iwe kwa kusema ukweli au uongo na haijaanza katika hili la mafuta na gesi hata kwenye suala la uchimbaji mkubwa alizua sokomoko kubwa miaka kadhaa iliyopita na Muhongo hakuwapo.

Bwana Mengi anatumia vibaya vyombo vyake vya habari na anasahau kwamba masafa ni ya umma na kibali cha gazeti ni kwa ajili ya kuhudumia jamii na wala si kikundi cha watu iwe kiuchumi au kisiasa.

Mhariri wa Nipashe anakiuka misingi ya uhariri na uandishi wa habari na kwa kushirikiana na Bwana Mengi ataitumbukiza nchi hii kwenye machafuko.
 
Ni kweli yupo katika operesheni maalum ambayo Mengi ameipatia jina Operesheni Delete Muhongo. Badala ya kutuhabarisha yanayojiri nchini na duniani kazi imekuwa ni kupambana na Muhongo.
 
Mkuu, mwenye agenda sio mhariri bali mmiliki wa hayo magazeti. Taarifa zinaonyesha kwamba amekuwa akiwashinikiza wahariri wake kuandika anayoyataka yeye, na hasa kama ana ugomvi na watu wengine.
 
Unaonekana umetumwa na sijui umelipwa sh ngap acha kuingilia uhuru wa vyombo vya habar kama ameandika pumba wasomaji watachuuja wenyewe taarifa.
 
Na mhariri wa UHURU, MZALENDO na JAMBO LEO bila kusahau na mkurugenzi na wanahabari wa TBC huwa wana ajenda gani? maana wao siku zote wanaitetea CCM hata kama imefanya kitu kibaya kinachohatarisha amani ya nchi.

Tafadhali rudi kwenye mada umetoka nje samahani
 
Na mhariri wa UHURU, MZALENDO na JAMBO LEO bila kusahau na mkurugenzi na wanahabari wa TBC huwa wana ajenda gani? maana wao siku zote wanaitetea CCM hata kama imefanya kitu kibaya kinachohatarisha amani ya nchi.[/QUOTE

Achana na hayo magazeti ya CCM. Kwani sasa Nipashe ni la upinzani? Au Mengi ni mpinzani? Anapaswa kuheshimu uhuru wa uhariri wa habari. Huyo mzee ndio maana anakimbiwa na wafanyakazi kila siku.
 


Kwa miezi kadhaa sasa mhariri wa Nipashe amekuwa akiendesha kampeni maalum na si bila ya maelekezo ya Dkt Reginald Mengi ya kuhakikisha kwamba Profesa sospeter Muhongo ama anafukuzwa kazi au anajiuzulu. Hili la akaunti ya Escrow limekuja tu katika kipindi ambacho tayari kulikuwapo na kampeni maalum ya kumlazimisha kukimbia nafasi yake hiyo.
Hakuna toleo linalotoka bila ya kuwa na habari ya ukurasa wa mbele kumshambulia Profesa Muhongo. Hakuna urazini hata kidogo kwani katika kampeni ya propaganda ambayo lengo lake ni kumng'oa Muhongo kila silaha hutumika.
Kumekuwapo na maelekezo maalumu kutoka kwa Dkt Mengi kwamba gazeti hilo liongoze vita hadi ushindi yaani ushindi wa Nipashe na ITV ni kung'oka kwa Muhongo na asipong'oka vita hiyo ni ya kudumu.
Muhongo kosa lake ni kuwa mkweli tu na kumwambia Mzee Mengi kwamba gharama za kuwekeza katika utafutaji wa mafuta katika bahari ni kikubwa kwa makampuni ya hapa nchini yaani kwa wazawa. Ukweli ambao Bwana Mengi hautaki hata kidogo kuusikia. Lakini ndiyo ukweli wenyewe kuwekeza katika utafutaji wa mafuta na gesi kwenye bahari bila ya kushirikiana na makampuni ya wenye fedha kubwa si rahisi kwa makampuni ya humu ndani.
Ni vita ambayo Dkt Mengi anataka ashinde kwa njia yoyote ile iwe kwa kusema ukweli au uongo na haijaanza katika hili la mafuta na gesi hata kwenye suala la uchimbaji mkubwa alizua sokomoko kubwa miaka kadhaa iliyopita na Muhongo hakuwapo.
Bwana Mengi anatumia vibaya vyombo vyake vya habari na anasahau kwamba masafa ni ya umma na kibali cha gazeti ni kwa ajili ya kuhudumia jamii na wala si kikundi cha watu iwe kiuchumi au kisiasa.
Mhariri wa Nipashe anakiuka misingi ya uhariri na uandishi wa habari na kwa kushirikiana na Bwana Mengi ataitumbukiza nchi hii kwenye machafuko

mkuu kichwa yako maji
 
Na mhariri wa UHURU, MZALENDO na JAMBO LEO bila kusahau na mkurugenzi na wanahabari wa TBC huwa wana ajenda gani? maana wao siku zote wanaitetea CCM hata kama imefanya kitu kibaya kinachohatarisha amani ya nchi.
Ukweli ulio mchungu zaid
 
Na mhariri wa UHURU, MZALENDO na JAMBO LEO bila kusahau na mkurugenzi na wanahabari wa TBC huwa wana ajenda gani? maana wao siku zote wanaitetea CCM hata kama imefanya kitu kibaya kinachohatarisha amani ya nchi.[/QUOTE

Achana na hayo magazeti ya CCM. Kwani sasa Nipashe ni la upinzani? Au Mengi ni mpinzani? Anapaswa kuheshimu uhuru wa uhariri wa habari. Huyo mzee ndio maana anakimbiwa na wafanyakazi kila siku.

Hujitambui we bure kabisa
 
mimi ndio Mhariri wa Nipashe , Mzee Mengi hatushinikizi, bali sisi wenyewe kwa uzalendo wa taifa hili changa tumeamua kufanya kazi ya UMMA.
 
So long as ni vita dhidi ya wezi,wa Tanzania tunamtakia kila heri.
Akimalizana na Muhongo tunaomba aanze na Proff wa Ki China
 
Umeona ee...mimi nilikuwa nasema na nitasema siku zote kuwa huyu mengi anatumia vibaya vyombo vayke vya habari. kama unakumbuka kadhia ya Mheshimiwa Adam malima ilikuwa hivihivi magazeti yanamshambulia lakini mwisho wa siku ukweli ukabainika mengi akabwaga manyanga. sasa amekomaa na profesa muhongo kwa akili yake anadhani akimtoa uwaziri atakuwa amemmaliza lakini hajui kuwa atakuwa amemjenga zaidi


Kwa miezi kadhaa sasa mhariri wa Nipashe amekuwa akiendesha kampeni maalum na si bila ya maelekezo ya Dkt Reginald Mengi ya kuhakikisha kwamba Profesa sospeter Muhongo ama anafukuzwa kazi au anajiuzulu. Hili la akaunti ya Escrow limekuja tu katika kipindi ambacho tayari kulikuwapo na kampeni maalum ya kumlazimisha kukimbia nafasi yake hiyo.
Hakuna toleo linalotoka bila ya kuwa na habari ya ukurasa wa mbele kumshambulia Profesa Muhongo. Hakuna urazini hata kidogo kwani katika kampeni ya propaganda ambayo lengo lake ni kumng'oa Muhongo kila silaha hutumika.
Kumekuwapo na maelekezo maalumu kutoka kwa Dkt Mengi kwamba gazeti hilo liongoze vita hadi ushindi yaani ushindi wa Nipashe na ITV ni kung'oka kwa Muhongo na asipong'oka vita hiyo ni ya kudumu.
Muhongo kosa lake ni kuwa mkweli tu na kumwambia Mzee Mengi kwamba gharama za kuwekeza katika utafutaji wa mafuta katika bahari ni kikubwa kwa makampuni ya hapa nchini yaani kwa wazawa. Ukweli ambao Bwana Mengi hautaki hata kidogo kuusikia. Lakini ndiyo ukweli wenyewe kuwekeza katika utafutaji wa mafuta na gesi kwenye bahari bila ya kushirikiana na makampuni ya wenye fedha kubwa si rahisi kwa makampuni ya humu ndani.
Ni vita ambayo Dkt Mengi anataka ashinde kwa njia yoyote ile iwe kwa kusema ukweli au uongo na haijaanza katika hili la mafuta na gesi hata kwenye suala la uchimbaji mkubwa alizua sokomoko kubwa miaka kadhaa iliyopita na Muhongo hakuwapo.
Bwana Mengi anatumia vibaya vyombo vyake vya habari na anasahau kwamba masafa ni ya umma na kibali cha gazeti ni kwa ajili ya kuhudumia jamii na wala si kikundi cha watu iwe kiuchumi au kisiasa.
Mhariri wa Nipashe anakiuka misingi ya uhariri na uandishi wa habari na kwa kushirikiana na Bwana Mengi ataitumbukiza nchi hii kwenye machafuko
 
Si busara kutumia gazeti la umma kwa ajili ya kufanikisha au kuamua ugomvi kati ya watu wawili. Sio sahihi hata kidogo kwa Mengi kutumia magazeti anayomiliki kwa aili ya kupambana na watu anaogombana nao katika mambo yake ya biashara na kama anataka kuingia kwenye siasa basi na atangaze rasmi.
 
Back
Top Bottom